STK ONE
JF-Expert Member
- Dec 31, 2011
- 627
- 184
Nakipenda sana kipindi cha akina Zembwela na Michael Baruti. Zembwela anapenda kusema kuwa "Yasiyowezekana nchi nyingine yoyote ile, Tanzania yanawezekana." Naomba kuongeza kitu, "Yasiyowezekana nchi nyingine yoyote ile hapa duniani, Tanzania chini ya CCM ya Kikwete, Yanawezekana." Mfano kuiba twiga kwenye ndege, kukodisha ardhi kwa Tsh. 200/- kwa mwaka kwa miaka 99. Haya hayawezekani sehemu yoyote ile duniani, ni TANZANIA TU, TENA CHINI YA CCM NA KIKWETE.
Nimepatwa na uchungu mkubwa sana kutokana na thread ambayo imepostiwa na COMMITED inyohusu kuchukuliwa kwa ardhi ya Mpanda kwa gharama nafuu kuliko unafuu wenyewe. Nakumbuka ilikuwa mwezi wa kwanza au wa kumi na mbili hivi, baada ya Pinda kuzomewa na wananchi wa Mpanda mjini mwishoni mwa mwaka jana, aliamua kumualika Kikwete kwenda mpanda akiambatana na akina Idd Simba wakiambatana na wazungu wa Agrisol zaidi ya mia moja. Pinda alizomewa baada ya wananchi kupinga kitendo cha serikali kupitia yeye (Pinda) kuibinafsha ardhi iliyokuwa inakaliwa na wakimbizi katika maeneo ya Katumba na Mishamo wilayani Mpanda.
Kuzomewa kwa Pinda kulikuja baada ya yeye kutaka kuwadanganya wananchi kuwa kulikuwa na faida kubwa katika kuwekeza katika ardhi ambayo nimeitaja hapo juu. Lakini kabla ya Pinda, Mbunge wa Mpanda mjini (CHADEMA) Said Alfi, alikuwa amewaambia wananchi kila kitu ambacho kilikuwa ndani ya mkataba wa Agriso na Serikali. Kwa hiyo PInda alipofika Mpanda alitaka kuwadanganya wananchi na ndiyo chanzo cha Kuzomewa. Hili lilipelekea Pinda kumualika Kikwete kuwaleta wale wazungu Mpanda, kwani aliamini kuwa akiwa peke yake asingeweza kusikilizwa.
Pinda tangu uchaguzi wa 2010 amekuwa akidharauliwa na kuchukiwa sana Mpanda mjini. Japo wanasema kuwa nabii hakubaliki nyumbani, lakini kwa Pinda ni too much. Hasira za wananchi wa Mpanda mjini juu ya Pinda, zilianza baada ya Pinda kuchangia kwa asilimia zote kuchakachua matokeo ya Ubunge Sumbawanga mjini, kwa kumpa ushindi Aish (CCM) ilihali aliyekuwa ameshinda ni mgombea wa CHADEMA. Lakini hili la kuwaleta wawekezaji kwenye ardhi ya Mpanda kwa bei ya kutupa, limewaongezea hasira sana wananchi wa Mpanda na kwa hili, Pinda hawezi kusimama kwa amani kwenye majukwa ya Mpanda mjini na kuhutubia, anaogopa kuzomewa tena.
Naiona 2015 mbali sana. Nimewahi kuandika hapa jamvini kuwa kuing'oa CCM madarakani kupitia sanduku la kura ni kazi kubwa sana. Mimi kwa mtazamo wangu, bado naamini kuwa CCM itaondoka madarakani kwa shinikizo la wananchi wenyewe. Kama ambavyo anasema Nape kila siku kuwa CCM itatawala milele, namuunga mkono. Kama wanaharakati na wanaCHADEMA tunategemea kuing'oa CCM madarakani kwa njia ya kura, itachukua muda mrefu sana karibia na MILELE ambayo anaisema Nape.
Najiuliza kama viongozi wa CCM na serikali yao wana akili timamu. Kuuza ardhi ya wananchi kwa hekta moja TSH 200/- kwa mwaka, na Tsh 500/- kwa kila ekari itakayolimwa, ni akili za mtu anayefikiria kweli???? Hii 200 ambayo haiwezi kununua ndoo ya maji ya lita 20 ndiyo ambayo tunalipwa wananchi wa Mpanda kwa mwaka??? Inaumiza sana. Hapa Mpanda kuna eneo linaitwa KAKESE. Eneo hili ni maarufu sana kwa kilimo cha Mpunga, huku tunakodishiwa ekari moja kwa TSH. 50,000/- kwa msimu mmja wa kilimo. Najiuliza, hivi tungewaleta wawekezaji wa ndani ya nchi, wakalima kwa kutumia mbegu asilia, na kuwakodishia ekari moja kwa Tsh. 50,000/- tungelishindwa kuendesha mashamba haya na kuongeza tija ya chakula? Kwa nini ngozi nyeusi tumekuwa tukitegemea sana wazungu kutukomboa katika kila kitu?
Hivi kweli CCM inaamini kwa dhati kuwa tatizo la chakula litamalizwa na hawa wazungu ambao wanaingia kwa malengo yao? Pinda alituambia kuwa vijana wataajiriwa na kwamba wazungu wataongeza chakula. Lakini Mpanda hatuna shida ya chakula. Hadi sasa tunavuna mahindi ya mwaka huu, bado kuna magari kibao yanabeba mahindi kutoka Mpanda kwenye mikoa ya Tabora, Shinyanga hadi Mwanza. Tunahitaji wazungu kwa lipi? Kweli 200/- kwa mwaka....Pinda akili zake zina akili kweli? Tena bila aibu anajiita mtoto wa mkulima???? Shame on you Mizengo. Pinda hakulelewa na wazaze wake awe na akili za ajabu namna hii.
2015 ni mblai sana. Kama kweli tunampango wa kuikomboa nchi hii, tuchukue hatua. Nimewahi kumwandikia Dr. Slaa kupitia jamvi hili kuwa Kuiondoa CCM madarakani ni ndoto kubwa sana ambayo haiwezi kutokea katika miaka ya hivi karibuni bila kuamua kutumia nguvu ya umma. Viongozi wa CCM watatutukana sana, Tutatawaliwa na Baba, mtoto hadi mjukuu wa ukoo mmoja na hatutakuwa na lolote la kufanya. japo wengi tunauona mwisho kuwa uko karibu, lakini karibu ambayo tunaiona sisi, ni miaka mingi sana.
Mmarekani amewekeza sana hapa Nchini. Kuiondoa CCM madarakani ni kuhatarishi maslahi ya Marekani hapa nchini. Nafikiri mnakumbuka jinsi hoja ya DOWANS ilivyoisha baada ya Symbion kununua mitambo ile tena alikuja Hilaly Clinton na kuisifia sana. Hadi leo, hata wale ambao walikuwa wanapiga kelele kuhusu Dowans wametulia kabisa. Hata hawa AGRISOL ni wamarekani, migodi mingi imewekezwa na wamarekani. Kwa hiyo Mmarekani atatumia kila namna anayoweza kuhakikisha kuwa Vibaraka wake wanaendelea kubaki Madarakani ili aendelee kuchuma.
Bajeti yetu bado ni tegemezi kwa kiasi kikubwa. serikali haina uwezo wa kukataa kusaini mikataba ya miaka 99 kwa shilingi 200 kwa hekari kama huu wa AGRISOL wa mpanda, kwa sababu watanyimwa nyongeza kwenye bajeti. Tunafanaya nini?
Tumelalamika sana. Tumeongea mengi sana. Tumesema mengi pia. Nini tunafanya kuhakikisha kuwa hali hii haiendelei? Kama tutaendelea kusema U-CCM na U-CHADEMA wetu kwenye mambo ya msingi kama ARDHI, tutalipoteza Taifa hili na siyo Mwna CCM walla Mwana CHADEMA ambaye atabaki salama. Wengi wanaoshabikia CCM huko Arumeru mashariki, hawa wanaoshabikia CHADEMA ni MASIKINI wa kutupwa. Hawana mbele wala nyuma. Hakuna mwenye matumaini hata mmoja. Usione watu wamevaa Kofia za CCM na matshirt ya kijani na njano ukadhani wanapenda, hawana ALTERNATIVE. Hata ambao tunavaa kofia za CHADEMA, hatuna namna nyingine. Tukiendelea kusema CCM, na mimi CHADEMA, ardhi inayochukuliwa na maliasili zinazoporwa siyo za CCM wala siyo za CHADEMA, wala hata siyo za CUF, ni za WATANZANIA. Kuna siku CCM itapita, CHADEMA, CUF, NCCR na vyama vingine vyote vitapita, lakini TAIFA la TANZANIA lisimama milele. Hata kama maliasili zote zitachukuliwa na wazungu, milima ikianguka na nyumba zote na sisi wote kupita, bado TANZANIA itabaki MILELE NA MILELE.
Tuna kufa masikini, kuishi kwa shida, hatuna matumaini ya kesho na ugumu wa maisha, siyo kwa wana CCM wala siyo kwa wana CHADEMA, wote tumepigika, wote tunanunua kwenye maduka yale yale, wote tunatibiwa kwenye hospitali zilizochoka na madaktari waliokata tamaa. Hata polisi wengi, ukiwatoa akina SAID MWEMA na wenzake wachache, hata wanajeshi, ukiwatoa akina DAVID MWAMUNYANGE na wenzake wachache, wote wanaishi maisha mgumu kama rais wengine. Angalia nyumba za askari polisi, niliwahi kuhisi pengine wanajeshi wanamakazi mazuri, nikiwa Morogoro mwaka mmoja, nikafika Mzinga, kwenye kambi za jeshi na kwenye kiwanda cha KUTENGENEZA SILAHA. Hali ni ile ile, nyumba mbovu, tena niliyefika kwake, alikuwa na cheo cha SAJENTI. Ana nyumba ya chumba kimoja na sebule, tena imechoka mno. Nashindwa kuelewa wanajeshi wamelishwa nini hata wavumillie maisha magumu namna hii?
MWISHOOO....CCM kuondoka madarakani kupitia sanduku la kura, ni NDOTO, tena TUNAOTA MCHANA tukiwa hatuna hata LEPE LA USINGIZI. Tukiendelea kuimba U - CCM, U - CHADEMA, U - CUF na U - NCCR mageuzi, tutabaki kuwa mtaji wa matajiri wa ulaya na Marekani. Hadi siku ambayo tutaamua kuweza tofauti za dini zetu, kabila zetu, itikadi za SIASA na mengine mengi kando na kulipigania TAIFA letu na maliasili zake. Sina haja ya kusema Mungu ibariki Tz, MUNGU katubariki kila kitu, ni kitu gani ambacho hatuna hapa Tz? Tukisema Mungu tubariki, na wasomali, Sudani kusini, watasemaje? Tunashndwa na Rwanda ambayo imetoka vitani na sasa tunaiona kwa mbali....AIBU SANA.
Tumeshabarikiwa, tuchukue hatua kuiondoa CCM madarakni na viongozi wake wabinafsi, tusipofanya hivyo, ataingia, LOWASA au HUSSEIN MWINYI 2015, kama ilivyo kwa SIOI SUMMARI huko ARUMERU.
NAOMBA KUWAKILISHA......
Nimepatwa na uchungu mkubwa sana kutokana na thread ambayo imepostiwa na COMMITED inyohusu kuchukuliwa kwa ardhi ya Mpanda kwa gharama nafuu kuliko unafuu wenyewe. Nakumbuka ilikuwa mwezi wa kwanza au wa kumi na mbili hivi, baada ya Pinda kuzomewa na wananchi wa Mpanda mjini mwishoni mwa mwaka jana, aliamua kumualika Kikwete kwenda mpanda akiambatana na akina Idd Simba wakiambatana na wazungu wa Agrisol zaidi ya mia moja. Pinda alizomewa baada ya wananchi kupinga kitendo cha serikali kupitia yeye (Pinda) kuibinafsha ardhi iliyokuwa inakaliwa na wakimbizi katika maeneo ya Katumba na Mishamo wilayani Mpanda.
Kuzomewa kwa Pinda kulikuja baada ya yeye kutaka kuwadanganya wananchi kuwa kulikuwa na faida kubwa katika kuwekeza katika ardhi ambayo nimeitaja hapo juu. Lakini kabla ya Pinda, Mbunge wa Mpanda mjini (CHADEMA) Said Alfi, alikuwa amewaambia wananchi kila kitu ambacho kilikuwa ndani ya mkataba wa Agriso na Serikali. Kwa hiyo PInda alipofika Mpanda alitaka kuwadanganya wananchi na ndiyo chanzo cha Kuzomewa. Hili lilipelekea Pinda kumualika Kikwete kuwaleta wale wazungu Mpanda, kwani aliamini kuwa akiwa peke yake asingeweza kusikilizwa.
Pinda tangu uchaguzi wa 2010 amekuwa akidharauliwa na kuchukiwa sana Mpanda mjini. Japo wanasema kuwa nabii hakubaliki nyumbani, lakini kwa Pinda ni too much. Hasira za wananchi wa Mpanda mjini juu ya Pinda, zilianza baada ya Pinda kuchangia kwa asilimia zote kuchakachua matokeo ya Ubunge Sumbawanga mjini, kwa kumpa ushindi Aish (CCM) ilihali aliyekuwa ameshinda ni mgombea wa CHADEMA. Lakini hili la kuwaleta wawekezaji kwenye ardhi ya Mpanda kwa bei ya kutupa, limewaongezea hasira sana wananchi wa Mpanda na kwa hili, Pinda hawezi kusimama kwa amani kwenye majukwa ya Mpanda mjini na kuhutubia, anaogopa kuzomewa tena.
Naiona 2015 mbali sana. Nimewahi kuandika hapa jamvini kuwa kuing'oa CCM madarakani kupitia sanduku la kura ni kazi kubwa sana. Mimi kwa mtazamo wangu, bado naamini kuwa CCM itaondoka madarakani kwa shinikizo la wananchi wenyewe. Kama ambavyo anasema Nape kila siku kuwa CCM itatawala milele, namuunga mkono. Kama wanaharakati na wanaCHADEMA tunategemea kuing'oa CCM madarakani kwa njia ya kura, itachukua muda mrefu sana karibia na MILELE ambayo anaisema Nape.
Najiuliza kama viongozi wa CCM na serikali yao wana akili timamu. Kuuza ardhi ya wananchi kwa hekta moja TSH 200/- kwa mwaka, na Tsh 500/- kwa kila ekari itakayolimwa, ni akili za mtu anayefikiria kweli???? Hii 200 ambayo haiwezi kununua ndoo ya maji ya lita 20 ndiyo ambayo tunalipwa wananchi wa Mpanda kwa mwaka??? Inaumiza sana. Hapa Mpanda kuna eneo linaitwa KAKESE. Eneo hili ni maarufu sana kwa kilimo cha Mpunga, huku tunakodishiwa ekari moja kwa TSH. 50,000/- kwa msimu mmja wa kilimo. Najiuliza, hivi tungewaleta wawekezaji wa ndani ya nchi, wakalima kwa kutumia mbegu asilia, na kuwakodishia ekari moja kwa Tsh. 50,000/- tungelishindwa kuendesha mashamba haya na kuongeza tija ya chakula? Kwa nini ngozi nyeusi tumekuwa tukitegemea sana wazungu kutukomboa katika kila kitu?
Hivi kweli CCM inaamini kwa dhati kuwa tatizo la chakula litamalizwa na hawa wazungu ambao wanaingia kwa malengo yao? Pinda alituambia kuwa vijana wataajiriwa na kwamba wazungu wataongeza chakula. Lakini Mpanda hatuna shida ya chakula. Hadi sasa tunavuna mahindi ya mwaka huu, bado kuna magari kibao yanabeba mahindi kutoka Mpanda kwenye mikoa ya Tabora, Shinyanga hadi Mwanza. Tunahitaji wazungu kwa lipi? Kweli 200/- kwa mwaka....Pinda akili zake zina akili kweli? Tena bila aibu anajiita mtoto wa mkulima???? Shame on you Mizengo. Pinda hakulelewa na wazaze wake awe na akili za ajabu namna hii.
2015 ni mblai sana. Kama kweli tunampango wa kuikomboa nchi hii, tuchukue hatua. Nimewahi kumwandikia Dr. Slaa kupitia jamvi hili kuwa Kuiondoa CCM madarakani ni ndoto kubwa sana ambayo haiwezi kutokea katika miaka ya hivi karibuni bila kuamua kutumia nguvu ya umma. Viongozi wa CCM watatutukana sana, Tutatawaliwa na Baba, mtoto hadi mjukuu wa ukoo mmoja na hatutakuwa na lolote la kufanya. japo wengi tunauona mwisho kuwa uko karibu, lakini karibu ambayo tunaiona sisi, ni miaka mingi sana.
Mmarekani amewekeza sana hapa Nchini. Kuiondoa CCM madarakani ni kuhatarishi maslahi ya Marekani hapa nchini. Nafikiri mnakumbuka jinsi hoja ya DOWANS ilivyoisha baada ya Symbion kununua mitambo ile tena alikuja Hilaly Clinton na kuisifia sana. Hadi leo, hata wale ambao walikuwa wanapiga kelele kuhusu Dowans wametulia kabisa. Hata hawa AGRISOL ni wamarekani, migodi mingi imewekezwa na wamarekani. Kwa hiyo Mmarekani atatumia kila namna anayoweza kuhakikisha kuwa Vibaraka wake wanaendelea kubaki Madarakani ili aendelee kuchuma.
Bajeti yetu bado ni tegemezi kwa kiasi kikubwa. serikali haina uwezo wa kukataa kusaini mikataba ya miaka 99 kwa shilingi 200 kwa hekari kama huu wa AGRISOL wa mpanda, kwa sababu watanyimwa nyongeza kwenye bajeti. Tunafanaya nini?
Tumelalamika sana. Tumeongea mengi sana. Tumesema mengi pia. Nini tunafanya kuhakikisha kuwa hali hii haiendelei? Kama tutaendelea kusema U-CCM na U-CHADEMA wetu kwenye mambo ya msingi kama ARDHI, tutalipoteza Taifa hili na siyo Mwna CCM walla Mwana CHADEMA ambaye atabaki salama. Wengi wanaoshabikia CCM huko Arumeru mashariki, hawa wanaoshabikia CHADEMA ni MASIKINI wa kutupwa. Hawana mbele wala nyuma. Hakuna mwenye matumaini hata mmoja. Usione watu wamevaa Kofia za CCM na matshirt ya kijani na njano ukadhani wanapenda, hawana ALTERNATIVE. Hata ambao tunavaa kofia za CHADEMA, hatuna namna nyingine. Tukiendelea kusema CCM, na mimi CHADEMA, ardhi inayochukuliwa na maliasili zinazoporwa siyo za CCM wala siyo za CHADEMA, wala hata siyo za CUF, ni za WATANZANIA. Kuna siku CCM itapita, CHADEMA, CUF, NCCR na vyama vingine vyote vitapita, lakini TAIFA la TANZANIA lisimama milele. Hata kama maliasili zote zitachukuliwa na wazungu, milima ikianguka na nyumba zote na sisi wote kupita, bado TANZANIA itabaki MILELE NA MILELE.
Tuna kufa masikini, kuishi kwa shida, hatuna matumaini ya kesho na ugumu wa maisha, siyo kwa wana CCM wala siyo kwa wana CHADEMA, wote tumepigika, wote tunanunua kwenye maduka yale yale, wote tunatibiwa kwenye hospitali zilizochoka na madaktari waliokata tamaa. Hata polisi wengi, ukiwatoa akina SAID MWEMA na wenzake wachache, hata wanajeshi, ukiwatoa akina DAVID MWAMUNYANGE na wenzake wachache, wote wanaishi maisha mgumu kama rais wengine. Angalia nyumba za askari polisi, niliwahi kuhisi pengine wanajeshi wanamakazi mazuri, nikiwa Morogoro mwaka mmoja, nikafika Mzinga, kwenye kambi za jeshi na kwenye kiwanda cha KUTENGENEZA SILAHA. Hali ni ile ile, nyumba mbovu, tena niliyefika kwake, alikuwa na cheo cha SAJENTI. Ana nyumba ya chumba kimoja na sebule, tena imechoka mno. Nashindwa kuelewa wanajeshi wamelishwa nini hata wavumillie maisha magumu namna hii?
MWISHOOO....CCM kuondoka madarakani kupitia sanduku la kura, ni NDOTO, tena TUNAOTA MCHANA tukiwa hatuna hata LEPE LA USINGIZI. Tukiendelea kuimba U - CCM, U - CHADEMA, U - CUF na U - NCCR mageuzi, tutabaki kuwa mtaji wa matajiri wa ulaya na Marekani. Hadi siku ambayo tutaamua kuweza tofauti za dini zetu, kabila zetu, itikadi za SIASA na mengine mengi kando na kulipigania TAIFA letu na maliasili zake. Sina haja ya kusema Mungu ibariki Tz, MUNGU katubariki kila kitu, ni kitu gani ambacho hatuna hapa Tz? Tukisema Mungu tubariki, na wasomali, Sudani kusini, watasemaje? Tunashndwa na Rwanda ambayo imetoka vitani na sasa tunaiona kwa mbali....AIBU SANA.
Tumeshabarikiwa, tuchukue hatua kuiondoa CCM madarakni na viongozi wake wabinafsi, tusipofanya hivyo, ataingia, LOWASA au HUSSEIN MWINYI 2015, kama ilivyo kwa SIOI SUMMARI huko ARUMERU.
NAOMBA KUWAKILISHA......