kichenchele
JF-Expert Member
- Jun 28, 2010
- 539
- 176
Napenda kutumia nafasi hii kuwafahamisha wana Simba wenzangu juu ya ukweli uliopo kwa Emmanuel Okwi kujiunga na Yanga, Emmanuel Okwi anatarajiwa kurejea nyumbani hivi karibuni na mara tu atakapo fika anatarajiwa kujiunga na Yanga, makamu mwenyekiti wa club ya Simba ndugu Kaburu ndo amekuwa akiratibu zoezi zima la kumuuza Okwi kwa yanga na ameahidiwa kupewa cha juu kama alivyofanya kwa Kelvin Yondani na Juma Kaseja Mwaka juzi, huyu jamaa yuko kibiashara sana na ni kweli Emmanuel Okwi alitakiwa kusaini yanga mapema sana lakini baada ya wapenda simba kumbana na kumlazimu apige simu na kuweka loud speaker kidogo alifanikiwa kuwatuliza watu waliokuwa na jazba kubwa lakini ukweli ndo huo Okwi anaenda Yanga na ndo maana wanahaha kuwasajiri akina mrisho Ngasa na Twite ili mashabiki wa Simba wasije wakapanic lakini hii ni soccer mchezaji aruhusiwe kwenda kokote mara tu baada ya taratibu kufuatwa,