Kwa Hali hii ni Hatari Tuombe Huruma ya Mungu

bemg

JF-Expert Member
Apr 25, 2010
2,799
642
Wana JF bila kujali dini zetu tuombe Mungu atuhurumie maana watawala wetu na vyombo vya kulinda usalama wetu vimekuwa adui wa uhai wetu. Maisha magumu,ukame,ajali,ufisadi,maneno matamu kwa watawala na askari wanaua raia mchana kweupe hakuna anayeajibishwa.Inauma sana nainatia huruma sana.

Mungu utukumbe mambo yaliyotupa na yanayoendelea kutupa tangu tumekuwa chini ya uhuru wetu,atuangalie aone jinsi tunavyozidi kuabishwa na utawala tulionao kwa sasa.

Maliasili na nchi yetu imekabidhiwa wageni na nyumba zetu watu wengine.Tumekuwa kama yatima bila baba wakututetea na mama zetu wanaonekana kama wajane.Wanapotokea watu wenye huruma na tunavyoteseka ili watutetee wananchi watawala wanawaita ni wahaini.Ee Mungu tuhurumie.

Maji yetu tunayapata kwa fedha kuni zetu zinazotokana na miti yetu pia twanunua.Tunalazimishwa kulipa kodi kubwa lakini mafisadi yanazitafuna mchana kweupe hakuna wakuyakamata na kuyatia haitani.Watetezi wa walala hoi ndiyo wanakamatwa kila wakiinuka kutetea haki.Ee Mungu tuhurumie.

Mabepari ndiyo wanaotutawala wala hakuna wa kutuokoa mikononi mwao ni wewe peke yako Mungu ndiyo mwenye uwezo kupitia watu wako walionahuruma ya mateso haya.Chakula chetu twapata kwa kuhatarisha maisha yetu maana wauaji wanazurura huko mashambani,ofisini, kwenye vyombo vya usafiri na mitaani.Ee Mungu tuhurumie.

Vijana wetu na nguvu kazi ya taifa wanauwawa kwa nguvu kwenye ardhi yao na katika vijiji vyao kwasababu ya kulinda maslahi ya wageni.Furaha ya mioyo yetu imetoweka kwa chama tulichokipa matumaini ya kututoa kwenye umaskini,na ngoma zetu zimegeuzwa kuwa maombolezo.

Tufariji Mungu na ututee .Mungu usituache muda mrefu hivi tuendelee kuteseka na hali hii.Ee Mungu utawala wa wafalme wa dunia hii ni wa muda tu lakini wewe watawala milele na utawala wako wadumu vizazi vyote.Tunaomba huruma yako na ushuke katika nchi yetu na utusamehe pale kama taifa tumekukosea na uturudishie umoja wetu na tufaidike na maliasili zetu.Ee Mungu tuhurumie.
 
Wana JF bila kujali dini zetu tuombe Mungu atuhurumie maana watawala wetu na vyombo vya kulinda usalama wetu vimekuwa adui wa uhai wetu. Maisha magumu,ukame,ajali,ufisadi,maneno matamu kwa watawala na askari wanaua raia mchana kweupe hakuna anayeajibishwa.Inauma sana nainatia huruma sana.

Mungu utukumbe mambo yaliyotupa na yanayoendelea kutupa tangu tumekuwa chini ya uhuru wetu,atuangalie aone jinsi tunavyozidi kuabishwa na utawala tulionao kwa sasa.
Maliasili na nchi yetu imekabidhiwa wageni na nyumba zetu watu wengine.Tumekuwa kama yatima bila baba wakututetea na mama zetu wanaonekana kama wajane.Wanapotokea watu wenye huruma na tunavyoteseka ili watutetee wananchi watawala wanawaita ni wahaini.Ee Mungu tuhurumie.

Maji yetu tunayapata kwa fedha kuni zetu zinazotokana na miti yetu pia twanunua.Tunalazimishwa kulipa kodi kubwa lakini mafisadi yanazitafuna mchana kweupe hakuna wakuyakamata na kuyatia haitani.Watetezi wa walala hoi ndiyo wanakamatwa kila wakiinuka kutetea haki.Ee Mungu tuhurumie.

Mabepari ndiyo wanaotutawala wala hakuna wa kutuokoa mikononi mwao ni wewe peke yako Mungu ndiyo mwenye uwezo kupitia watu wako walionahuruma ya mateso haya.Chakula chetu twapata kwa kuhatarisha maisha yetu maana wauaji wanazurura huko mashambani,ofisini, kwenye vyombo vya usafiri na mitaani.Ee Mungu tuhurumie.

Vijana wetu na nguvu kazi ya taifa wanauwawa kwa nguvu kwenye ardhi yao na katika vijiji vyao kwasababu ya kulinda maslahi ya wageni.Furaha ya mioyo yetu imetoweka kwa chama tulichokipa matumaini ya kututoa kwenye umaskini,na ngoma zetu zimegeuzwa kuwa maombolezo.

Tufariji Mungu na ututee .Mungu usituache muda mrefu hivi tuendelee kuteseka na hali hii.Ee Mungu utawala wa wafalme wa dunia hii ni wa muda tu lakini wewe watawala milele na utawala wako wadumu vizazi vyote.Tunaomba huruma yako na ushuke katika nchi yetu na utusamehe pale kama taifa tumekukosea na uturudishie umoja wetu na tufaidike na maliasili zetu.Ee Mungu tuhurumie.

Tumuombe MUNGU huku tukiwa katika mstari wa mbele mapambanoni
 
Kama maisha magumu fanya kazi kwa bidii ndugu yangu asiyefanya kazi na asile!!
 
"Mungu ibariki Tanzania. wabariki Viongozi wake...." Hili ni dua la kuku au Mungu bado anatupima? AU ndo viongozi aliowabariki hawa kwa ajili yetu?
 
Back
Top Bottom