menny terry
JF-Expert Member
- Mar 18, 2011
- 509
- 667
Kama wiki mbili zimepita Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya SIMON GROUP LMT bwana Robert Simon Kasena alidai kuwa UDA ilifikia ktk hali mbaya mno ilikuwa ikiweka rehani mali zake alafu inapopewa pesa na kununulia mabasi ya biashara baada ya muda yote hutokomea kusiko eleweka.Akaongeza kuwa UDA iliweka rehani mali zake ambazo ni Ubungo basi temino pamoja na eneo lilipo machinga complex.Lakini ilipo shindwa kulipa ilibidi iuze viwanja vyote kwa halmashauri.Japo wengi wanabisha mi naona heri UDA imeuzwa ijapokuwa sijapenda uuzwaji wake. Kama nilivyodokeza hapo juu kuwa kwanini tusibinafsishe maeneo yote na sekta zote zilizojaa uzembe? Kwa mfano bunge la makinda ambalo lipo kwa ajili ya kupitisha uozo wa jk,pili jeshi ambalo linalipua hovyo mabomu na kuacha watu wakitaabika hovyo,tatu Usalama wa taifa ambao wanyama wanaibiwa tena ndani ya nchi yetu bila wao kuwa na habari,Nne halmashauri za jiji ambazo hatakuzibua mifereji zimeshindwa,tano ofisi ya dpp na Takukuru ambazo hata kumnyooshea kidole chenge,lowasa,Rostam ambao ushaidi upo wazi,sita mahakama na jela ambazo zikotayari kumwona zombe,chenge hawana makosa lakini mwizi wa kuku ana hatia, kama shule na hospitali za binafsi zinafanya vizuri wakati za serekali zinaboronga nazo tubinafsishe.Kwa kweli kama kweli ubinafsishaji ni suluhisho mi naona bora tubinafsishe kila kitu.nawasilisha.