Kwa hali hii ni bora tubinafsishe kila kitu

menny terry

JF-Expert Member
Mar 18, 2011
509
667
Kama wiki mbili zimepita Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya SIMON GROUP LMT bwana Robert Simon Kasena alidai kuwa UDA ilifikia ktk hali mbaya mno ilikuwa ikiweka rehani mali zake alafu inapopewa pesa na kununulia mabasi ya biashara baada ya muda yote hutokomea kusiko eleweka.Akaongeza kuwa UDA iliweka rehani mali zake ambazo ni Ubungo basi temino pamoja na eneo lilipo machinga complex.Lakini ilipo shindwa kulipa ilibidi iuze viwanja vyote kwa halmashauri.Japo wengi wanabisha mi naona heri UDA imeuzwa ijapokuwa sijapenda uuzwaji wake. Kama nilivyodokeza hapo juu kuwa kwanini tusibinafsishe maeneo yote na sekta zote zilizojaa uzembe? Kwa mfano bunge la makinda ambalo lipo kwa ajili ya kupitisha uozo wa jk,pili jeshi ambalo linalipua hovyo mabomu na kuacha watu wakitaabika hovyo,tatu Usalama wa taifa ambao wanyama wanaibiwa tena ndani ya nchi yetu bila wao kuwa na habari,Nne halmashauri za jiji ambazo hatakuzibua mifereji zimeshindwa,tano ofisi ya dpp na Takukuru ambazo hata kumnyooshea kidole chenge,lowasa,Rostam ambao ushaidi upo wazi,sita mahakama na jela ambazo zikotayari kumwona zombe,chenge hawana makosa lakini mwizi wa kuku ana hatia, kama shule na hospitali za binafsi zinafanya vizuri wakati za serekali zinaboronga nazo tubinafsishe.Kwa kweli kama kweli ubinafsishaji ni suluhisho mi naona bora tubinafsishe kila kitu.nawasilisha.
 
Naunga mkono hoja kwamba ni bora na Ikulu ikabinafsishwa alafu baadae tumalizie na barabara zote za lami
 
Nia yako ni njema, lakini sidhani kama unaelewa undani wa ubinafsishaji.Kwa ufupi ubinafsishaji ni unyanyang'ani of a countries resources and transfering the resources to a few rich.It's in fact a way of putting the political elite in the pockets of those who control the economy of a country.They say give me the economy of a country and I don't care who is in power.To me ubinafsishaji sio njia ya ku-improve the economy of a country,but rather ni njia ya ufukarishaji.
 
Nia yako ni njema, lakini sidhani kama unaelewa undani wa ubinafsishaji.Kwa ufupi ubinafsishaji ni unyanyang'ani of a countries resources and transfering the resources to a few rich.It's in fact a way of putting the political elite in the pockets of those who control the economy of a country.They say give me the economy of a country and I don't care who is in power.To me ubinafsishaji sio njia ya ku-improve the economy of a country,but rather ni njia ya ufukarishaji.
Acha kukurupuka soma vizuri hiyo thread ndio ujibu
 
Back
Top Bottom