Congo
JF-Expert Member
- Mar 13, 2008
- 2,063
- 2,292
Mkapa alisema uongo kuhusu Vicent. Sio kweli kuwa alikuwa anaujua ukoo wote wa Nyerere. Yawezekana alikuwa anajua familia ya Julius Nyerere tu. Vicent ni mtoto wa Josephat Kiboko Nyerere ambaye ni mdogo wake tumbo moja na Julius Nyerere. Bahati mbaya huyu Josephat Kiboko alikuwa mtundu mtundu mpaka wakati fulani huko nyuma aliwahi kuwekwa ndani rumande Butimba na kaka yake. Mdogo wa Julius Nyerere mwingine alikuwa Joseph Kizurira Nyerere ambaye aliwahi kuwa kiongozi wa Umoja wa Vijana wa TANU. Uongozi sio lazima uende shule, shule inasaidia kuwa mwelewa zaidi. Kama suala ni elimu mbona hao wenye elimu ndio wezi, waporaji wa ardhi za wanachi, wanaosaini mikataba mibovu, wasiojua kupima dhahabu mpaka wanaumbuliwa na waporaji wasiosoma, wanaopanga kujenga uwanja wa ndege kubwa Mpanda (utakaowesha boeing 737 kutua) bila kijihakikishia abiria watakoutumia, wanaobalidi barabara zipite vijijini kwao, wanaohamisha wananchi wa Kipawa kwa malipo kidogo bila kuwa na uekezaji wowote, wanaoruhusu maji yenye sumu yatiririkie mitoni, hao ndio wasomi unaowataka?Ndio maana Mkapa alikuwa na mashaka kama vicent ni wa ukoo wa Nyerere elimu yake imejaa viraka anahitaji kwenda shule kama alivyofanya Mbowe. Elimu haina mwisho lakini inategemea kama anapenda shule