Kwa CCM na Serikali yake Kuweka Sheria Pembeni Kwa Mambo ya Kitaifa- MAAFA Kwa Taifa?

Mtu wa Mungu

JF-Expert Member
Nov 9, 2010
444
19
Tunaoishi tumeshuhudia Uchaguzi Mkuu ukivurugwa wazi wazi na hatimaye Kikwete kutwaa madaraka kwa kura 27% dhidi ya mshindi halali 64%;Wabunge wengi wa upinzani waliochaguliwa kihalali katika uchaguzi mkuu wakinyang'anywa kiharamia na vyombo vya usalama ushindi wao waliopata kwa mujibu wa sheria; Wabunge 19 wa CCM wakiingizwa kibabe bungeni bila kuchaguliwa na wapiga kura; wabunge wa CCM kwa utemi wakimpeleka mbunge sophia simba Bunge la SADC bila kuchaguliwa kwa mujibu wa sheria; na sasa mitafaruku ya kugombea viti vya umeya ambapo tunashuhudia sheria kuwekwa pembeni kiharamia; Tunajiuliza CCM na serikali yake wanatupeleka wapi????????????? Taifa lianze kujadili jambo hili kama janga la kitaifa kwa mstakabali wa amani na usalama wa taifa la Tanzania!!!!!!!! Vyama vya upinzani havina dola ya kutumia kuzua tafrani tunazoona kila leo!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom