Kashaijabutege
JF-Expert Member
- Oct 20, 2010
- 2,696
- 740
Ndugu wana JF ambao mnatafuta wachumba wa kuoa, nawashauri muoe wanawake wenye taaluma ya ualimu. Kina mama walimu, wengi wao, ni watulivu na ni walezi wazuri wa familia. Wanavaa mavazi ya heshima na ni wavumilivu sana katika ndoa.
Hata hivyo, sisemi kuwa wanawake wa taaluma nyingine hawafai kuoa; la hasha. Vivyo hivyo, si kila mwalimu wa kike anakuwa mwanandoa mzuri, ila nasema wengi wao taaluma yao huwapa maadili yanayowafanya wawe wake wazuri.
Kama kuna mwanamke mwalimu asiye na sifa nilizozitoa naomba atoe ushuhuda wake. Mliooa walimu kama mimi mnasemaje? I love my wife (Teacher).
Kina mama mliolewa na walimu, je nao ni baba wazuri?
Hata hivyo, sisemi kuwa wanawake wa taaluma nyingine hawafai kuoa; la hasha. Vivyo hivyo, si kila mwalimu wa kike anakuwa mwanandoa mzuri, ila nasema wengi wao taaluma yao huwapa maadili yanayowafanya wawe wake wazuri.
Kama kuna mwanamke mwalimu asiye na sifa nilizozitoa naomba atoe ushuhuda wake. Mliooa walimu kama mimi mnasemaje? I love my wife (Teacher).
Kina mama mliolewa na walimu, je nao ni baba wazuri?