KWA AKINAMAMA TU, na WABABA WAZOEFU

ntamaholo

JF-Expert Member
Aug 30, 2011
12,906
6,909
Wakuu salamuni.

Naombeni mwongozo wenu. Mke wangu amejifungua hvi karibuni, alijifungua salama na hali yake baada ya wiki moja na nusu alikuwa safi, na taratibu akaanza kunisogelea.

Kwa sasa ni wiki ya tatu tangu ajifungue, na tayari tumeanza kujamiana na kuondoa ugwadu. Mimi naogopa kwani nahisi anaweza kunasa mimba nyingine wakati bado tunahitaji kumtunza kijana wetu mpaka akomae vya kutosha.

Tumepanga akienda clinic ya kwanza, atumie moja ya njia za kudhibiti mimba ili kuepuka yeye kupata mimba soon.

Swali langu ni kuwa, Mwanamke kawaida anarudi kwenye mzunguko wake baada ya mda gani akisha jifungua?

Ni njia gani nzuri ya uzazi wa mpango ambayo haitaathiri afya ya wife wangu?

Nawashukuruni wakubwa

UPDATES.

Baada ya kusoma michango ya wadau mabalimbali katika uzi huu, baada ya kutafuta na vyanzo vingine vya suala husika nje ya JF, ushauri msimamo na ushauri wangui ni huu hapa.

(I) Nawashukuru wote waliochangia, lakini pia niwashukuru zaidi walioshauri tusubiri mpaka atleast 2 months ndo tuanze kufahamiana na wife. Nawashukuru sana kwa ushauri huo.

(ii) Ni nyongeza ya kiimani juu ya suala husika.

Kwa mjibu wa BIBLIA, mwanamke aliyejifungua lazima akae hali ametenngwa kwa mda wa siku saba. Siku ya nane, kama amezaa mtoto mme, anatakiwa ampeleke kwa utakaso, atahiriwe nyama ya govi lake, baada ya hapo akae kwa mda wa siku 33 bila kufanya lolote wala kukutana na mwanamme.

Na kama ni mtoto wa kike, mwanamke anatakiwa akae hali ya kutengwa kwa wiki mbili, baada ya hapo ampeleke kutakaswa kisha akae bila kufanya chochote hasa kujamiana kwa mda wa siku 66. Haya yote yanapatikana WALAWI 12:1-10.

UZAZI WA MPANGO.

Kwa mjibu wa Biblia, njia za uzazi wa mpango tunazozitumia hivi leo, ni kukosoa njia aliyoianzisha MUNGU, kama unaamini. Hivyo, kwa muamini, ni mwiko kutumia uzazi wa mpango nje ya utaratibu wa MUNGU.

Iwapo mtu atakaa kwa mda wa siku zilizoamriwa kujitenga na mke/mme wake kwa mda ulioamriwa na MUNGU, mwanamke akawa ananyonyesha full time, basi homoni zinazowajibika kutengeneza mayai kwa ajili ya urutubishaji, zitaacha kazi hiyo na kujikita kutengeneza maziwa ya mtoto. Hivyo baada ya hapo, hakuna haja ya kutumia kondomu wala njia yoyote ile kwani MUNGU kesaha maliza hesabu zake tayari mpaka mtoto afikishe miaka miwili hadi mitatu.

Utata ulioopo ni kwa kizazi cha leo ambapo mama naye anawajibika kufanya kazi ili kuongeza lishe ya nyumbani, lakini kwa serikalini ndio maana hupewa likizo ya uzazi takribani siku 90 ili kuwezesha suala hilo kufanikiwa.

Mie nimeaacha kabisa, na najuta kwa nini sikufahamu suala hili mapema, hata hivyo najilaumu kwani yawezekana mazingira ya ndoa yangu ndiyo yaliyosababisha yote haya, kama ningehudhuria mafunzo ya ndoa kanisani yawezekana yasingenikuta haya.

Nawashukuruni sana.
 
Kila mwanamke ana mzunguko tofauti.

Wapo wanaokaa miezi sita, wapo wengine mzunguko unaanza soon baada ya kujifungua.
So be very careful, hapa huwa pagumu maana naona kama unacheza bahati nasibu.

Upande wa njia nzuri ya uzazi ni mtizamo wa 'naweza beba hili kwa gharama ya hili'

kila njia ina faida na hasara zake.
Ni wewe na mkeo kupima ni faida zipi mtazibeba kwa hasara kiasi gani.

Lakini kwa mtazamo wangu njia ambazo hasara ni chache hasa za kiafya ni
1. Siku salama
2. Condom
3. Pull out method????? Inahitaji precautions nyingi.

Kwa ufafanuzi kuhusu njia za uzazi rejea mada hapo 'better be safe than sorry'
 
Mkuu wiki tatu noma,vuta vuta at least miezi miwili hivi.....

DU, ngoja nijipange. haya mambo yanatisha. Kuna nesi mmoja alikuwa akitufundisha elimu rika DSM, alisema, wanaume wengi hutoka nje ya ndoa kwa kisingizio kuwa wake zao wamejifungua na watalazimika kukaa pendingi kwa mda mrefu zaidi bila kugusana.

Yeye alikataa mawazo hayo, alisema kama damu za mama zimekatika, shughuli inaweza kuanza nyumbani. Na alisema kuna akina mama inawachukua just a week, baada ya hapo wako fiti kwa tendo la ndoa.

Utata uliopo ni na sikumbuki kama alisema lazima kutumia kondom
 
Kila mwanamke ana mzunguko tofauti.

Wapo wanaokaa miezi sita, wapo wengine mzunguko unaanza soon baada ya kujifungua.
So be very careful, hapa huwa pagumu maana naona kama unacheza bahati nasibu.

Upande wa njia nzuri ya uzazi ni mtizamo wa 'naweza beba hili kwa gharama ya hili'

kila njia ina faida na hasara zake.
Ni wewe na mkeo kupima ni faida zipi mtazibeba kwa hasara kiasi gani.

Lakini kwa mtazamo wangu njia ambazo hasara ni chache hasa za kiafya ni
1. Siku salama
2. Condom
3. Pull out method????? Inahitaji precautions nyingi.

Kwa ufafanuzi kuhusu njia za uzazi rejea mada hapo 'bettert be safe than sorry'

nakushukuru mkuu, zamani niliweza pull out, lakini kwa sasa, nafanya ili nimwage, hivyo nashindwa. mi naona nisafiri niende mali kabisa. Njia hii huitumia wachaga sana
 
bado hajapona huyo, wazee walioweka siku 40 si wajinga, ujue kuna kusikia maumivu na kuwa na mwili wa kawaida.
wazee wetu walimuweka ndani mzazi si chini ya siku arobaini, hospitali tunaambiwa si chini ya siku arobaini, unless huyo ni kati ya wale wachache ambao viungo vyao ni kama rababendi leo leo amerudia hali yake ya awali.
Nadhani unaweza kuimagine huo mzigo wa miezi tisa unahitaji wiki ngapi kujirudi kwa ajili ya kazi ya uzazi ujao.
Mimba sio rahisi kama ananyonyesha fulltime.
Ila kubwa naloliona hapo, mkeo anawasiwasi utaenda nje, cha muhimu hapo mpe faraja kuwa karibu nae mtoe wasiwasi apone vizuri, alee huyo mtoto mlieshajaliwa, maisha na starehe zipo tu.
 
umewahi sana kusema za ukweli ila kama mwenydwe haumii haya. Kuhusu njia salama ya uzazi wa mpango kuna uzi aliuleta Afrodenzi hapa una kila unachotaka kujua ufuatilie. Umegusia kuhusu kusafiri,kwa iyo hutaki kuona katoto kako kakismile kwa mara ya kwanza?
 
Wala haina tatizo,kama ananyonyesha possibility ya kupata mimba ni ndogo ila ni vizuri akaenda kwa daktari haraka kupata njia muafaka ya kuzuia mimba.Hilo wazo la kwenda mbali wala siliafiki hao uliowataja Bw.Ntamaholo kwa nyumba ndogo hao weeeeeeeeeeeee!!!!!acha kabisa.

KWA HERI!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
jamani huyo mkeo haumii? Wiki 3 hata kizazi hakijapona vizuri!

Kiafya zinatosha sana! Jamani hivi kwani wanawake huwa hasikii hamu? Na kama yeye anataka? Nmh ndio maana baadhi ya watu wanasema tumezidi kujifanya victim!
 
bado hajapona huyo, wazee walioweka siku 40 si wajinga, ujue kuna kusikia maumivu na kuwa na mwili wa kawaida.
wazee wetu walimuweka ndani mzazi si chini ya siku arobaini, hospitali tunaambiwa si chini ya siku arobaini, unless huyo ni kati ya wale wachache ambao viungo vyao ni kama rababendi leo leo amerudia hali yake ya awali.
Nadhani unaweza kuimagine huo mzigo wa miezi tisa unahitaji wiki ngapi kujirudi kwa ajili ya kazi ya uzazi ujao.
Mimba sio rahisi kama ananyonyesha fulltime.
Ila kubwa naloliona hapo, mkeo anawasiwasi utaenda nje, cha muhimu hapo mpe faraja kuwa karibu nae mtoe wasiwasi apone vizuri, alee huyo mtoto mlieshajaliwa, maisha na starehe zipo tu.

naona kipururu kina msumbua sana..
 
Mpaka week ya pili celvix inakuwa imejifunga, ndani ya week moja tu michubuko na kidonda kama ulichanika kinapona!

So kuanza sex after 2 weeks is okay mradi wote mwahitaji na sitegemei hard core stuff kwa marrried couple! Kwa case ya mimba, mkeo si ananyonyesha full time? You should be okay for at least six moons, huku mkifikiria ni njia gani mwaweza tumia, personal napendelea natural na condom during danger times!
 
Mpaka week ya pili celvix inakuwa imejifunga, ndani ya week moja tu michubuko na kidonda kama ulichanika kinapona!

So kuanza sex after 2 weeks is okay mradi wote mwahitaji na sitegemei hard core stuff kwa marrried couple! Kwa case ya mimba, mkeo si ananyonyesha full time? You should be okay for at least six moons, huku mkifikiria ni njia gani mwaweza tumia, personal napendelea natural na condom during danger times!

hakupata matatizo yoyote wakati wa kujifungua, ilimchukua mda kidogo kumaliza shughuli hiyo, namshukuru Mungu kwa hilo. Na mtoto, ilimchukua siku nne kitovu kodondoka, yaani wote wako safi tu.
 
Wala haina tatizo,kama ananyonyesha possibility ya kupata mimba ni ndogo ila ni vizuri akaenda kwa daktari haraka kupata njia muafaka ya kuzuia mimba.Hilo wazo la kwenda mbali wala siliafiki hao uliowataja Bw.Ntamaholo kwa nyumba ndogo hao weeeeeeeeeeeee!!!!!acha kabisa.

KWA HERI!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

kwa habari ya kunyonya, mtoto ananyonya nadha above normal. maana mama anweza kualamika maziwa yamejaa na yanamuuma, huku dogo kalala, akishtuka tu, hakubali mpaka apate mabhele, anavuta kwa nguvu utadhani hajanyonya wiki, au utadhani ni pre paid service mpaka mama yake anaumia kwa jinsi ananvyonyonya

 
Kwa utafiti nilio ufanya kwa kushirikiana na mke wangu, Njia bora ya uzazi wa mpango ni kuweka kipandikizi. Ni bora kuliko sindano au vidonge. Pia kabla ya kuchukua uamuzi wa njia gani ya kutumia Nenda na mkeo kwenye kituo cha afya kwa ufafanuzi zaidi wa njia za uzazi wa mpango.
 
Kiafya zinatosha sana! Jamani hivi kwani wanawake huwa hasikii hamu? Na kama yeye anataka? Nmh ndio maana baadhi ya watu wanasema tumezidi kujifanya victim!
MWANAMKE ALIYEJIFUNGUA KWA NJIA YA KAWAIDA ANAPASWA AKAE SI CHINI YA SIKU 40 NA ALIYEJIFUNGUA KWA KUPASULIWA ANAPASWA KUKAA ZAID YA MIEZI 3, hii ni kwa mujibu wa madaktari bingwa na wakunga wa jadi, swala la kushika mimba baada ya kujifungua hili linategemea na mzunguko wa mwanamama husika.
 
Back
Top Bottom