ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,906
- 6,909
Wakuu salamuni.
Naombeni mwongozo wenu. Mke wangu amejifungua hvi karibuni, alijifungua salama na hali yake baada ya wiki moja na nusu alikuwa safi, na taratibu akaanza kunisogelea.
Kwa sasa ni wiki ya tatu tangu ajifungue, na tayari tumeanza kujamiana na kuondoa ugwadu. Mimi naogopa kwani nahisi anaweza kunasa mimba nyingine wakati bado tunahitaji kumtunza kijana wetu mpaka akomae vya kutosha.
Tumepanga akienda clinic ya kwanza, atumie moja ya njia za kudhibiti mimba ili kuepuka yeye kupata mimba soon.
Swali langu ni kuwa, Mwanamke kawaida anarudi kwenye mzunguko wake baada ya mda gani akisha jifungua?
Ni njia gani nzuri ya uzazi wa mpango ambayo haitaathiri afya ya wife wangu?
Nawashukuruni wakubwa
UPDATES.
Baada ya kusoma michango ya wadau mabalimbali katika uzi huu, baada ya kutafuta na vyanzo vingine vya suala husika nje ya JF, ushauri msimamo na ushauri wangui ni huu hapa.
(I) Nawashukuru wote waliochangia, lakini pia niwashukuru zaidi walioshauri tusubiri mpaka atleast 2 months ndo tuanze kufahamiana na wife. Nawashukuru sana kwa ushauri huo.
(ii) Ni nyongeza ya kiimani juu ya suala husika.
Kwa mjibu wa BIBLIA, mwanamke aliyejifungua lazima akae hali ametenngwa kwa mda wa siku saba. Siku ya nane, kama amezaa mtoto mme, anatakiwa ampeleke kwa utakaso, atahiriwe nyama ya govi lake, baada ya hapo akae kwa mda wa siku 33 bila kufanya lolote wala kukutana na mwanamme.
Na kama ni mtoto wa kike, mwanamke anatakiwa akae hali ya kutengwa kwa wiki mbili, baada ya hapo ampeleke kutakaswa kisha akae bila kufanya chochote hasa kujamiana kwa mda wa siku 66. Haya yote yanapatikana WALAWI 12:1-10.
UZAZI WA MPANGO.
Kwa mjibu wa Biblia, njia za uzazi wa mpango tunazozitumia hivi leo, ni kukosoa njia aliyoianzisha MUNGU, kama unaamini. Hivyo, kwa muamini, ni mwiko kutumia uzazi wa mpango nje ya utaratibu wa MUNGU.
Iwapo mtu atakaa kwa mda wa siku zilizoamriwa kujitenga na mke/mme wake kwa mda ulioamriwa na MUNGU, mwanamke akawa ananyonyesha full time, basi homoni zinazowajibika kutengeneza mayai kwa ajili ya urutubishaji, zitaacha kazi hiyo na kujikita kutengeneza maziwa ya mtoto. Hivyo baada ya hapo, hakuna haja ya kutumia kondomu wala njia yoyote ile kwani MUNGU kesaha maliza hesabu zake tayari mpaka mtoto afikishe miaka miwili hadi mitatu.
Utata ulioopo ni kwa kizazi cha leo ambapo mama naye anawajibika kufanya kazi ili kuongeza lishe ya nyumbani, lakini kwa serikalini ndio maana hupewa likizo ya uzazi takribani siku 90 ili kuwezesha suala hilo kufanikiwa.
Mie nimeaacha kabisa, na najuta kwa nini sikufahamu suala hili mapema, hata hivyo najilaumu kwani yawezekana mazingira ya ndoa yangu ndiyo yaliyosababisha yote haya, kama ningehudhuria mafunzo ya ndoa kanisani yawezekana yasingenikuta haya.
Nawashukuruni sana.
Naombeni mwongozo wenu. Mke wangu amejifungua hvi karibuni, alijifungua salama na hali yake baada ya wiki moja na nusu alikuwa safi, na taratibu akaanza kunisogelea.
Kwa sasa ni wiki ya tatu tangu ajifungue, na tayari tumeanza kujamiana na kuondoa ugwadu. Mimi naogopa kwani nahisi anaweza kunasa mimba nyingine wakati bado tunahitaji kumtunza kijana wetu mpaka akomae vya kutosha.
Tumepanga akienda clinic ya kwanza, atumie moja ya njia za kudhibiti mimba ili kuepuka yeye kupata mimba soon.
Swali langu ni kuwa, Mwanamke kawaida anarudi kwenye mzunguko wake baada ya mda gani akisha jifungua?
Ni njia gani nzuri ya uzazi wa mpango ambayo haitaathiri afya ya wife wangu?
Nawashukuruni wakubwa
UPDATES.
Baada ya kusoma michango ya wadau mabalimbali katika uzi huu, baada ya kutafuta na vyanzo vingine vya suala husika nje ya JF, ushauri msimamo na ushauri wangui ni huu hapa.
(I) Nawashukuru wote waliochangia, lakini pia niwashukuru zaidi walioshauri tusubiri mpaka atleast 2 months ndo tuanze kufahamiana na wife. Nawashukuru sana kwa ushauri huo.
(ii) Ni nyongeza ya kiimani juu ya suala husika.
Kwa mjibu wa BIBLIA, mwanamke aliyejifungua lazima akae hali ametenngwa kwa mda wa siku saba. Siku ya nane, kama amezaa mtoto mme, anatakiwa ampeleke kwa utakaso, atahiriwe nyama ya govi lake, baada ya hapo akae kwa mda wa siku 33 bila kufanya lolote wala kukutana na mwanamme.
Na kama ni mtoto wa kike, mwanamke anatakiwa akae hali ya kutengwa kwa wiki mbili, baada ya hapo ampeleke kutakaswa kisha akae bila kufanya chochote hasa kujamiana kwa mda wa siku 66. Haya yote yanapatikana WALAWI 12:1-10.
UZAZI WA MPANGO.
Kwa mjibu wa Biblia, njia za uzazi wa mpango tunazozitumia hivi leo, ni kukosoa njia aliyoianzisha MUNGU, kama unaamini. Hivyo, kwa muamini, ni mwiko kutumia uzazi wa mpango nje ya utaratibu wa MUNGU.
Iwapo mtu atakaa kwa mda wa siku zilizoamriwa kujitenga na mke/mme wake kwa mda ulioamriwa na MUNGU, mwanamke akawa ananyonyesha full time, basi homoni zinazowajibika kutengeneza mayai kwa ajili ya urutubishaji, zitaacha kazi hiyo na kujikita kutengeneza maziwa ya mtoto. Hivyo baada ya hapo, hakuna haja ya kutumia kondomu wala njia yoyote ile kwani MUNGU kesaha maliza hesabu zake tayari mpaka mtoto afikishe miaka miwili hadi mitatu.
Utata ulioopo ni kwa kizazi cha leo ambapo mama naye anawajibika kufanya kazi ili kuongeza lishe ya nyumbani, lakini kwa serikalini ndio maana hupewa likizo ya uzazi takribani siku 90 ili kuwezesha suala hilo kufanikiwa.
Mie nimeaacha kabisa, na najuta kwa nini sikufahamu suala hili mapema, hata hivyo najilaumu kwani yawezekana mazingira ya ndoa yangu ndiyo yaliyosababisha yote haya, kama ningehudhuria mafunzo ya ndoa kanisani yawezekana yasingenikuta haya.
Nawashukuruni sana.