Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Jamani kama mmesikiliza tokea juzi na jana na hapa tulipofikia kuna vyombo mbalimbali vimesikika vikionya kuwa matokeo yapokewe kwa amani na utulivu ?
Je mnakubaliana na mavuvuzela hao ? Nakumbuka miaka yote iliyopita matokeo yalikuwa yakitolewa na yakipokewa kwa amani ,sasa hili au haya makelele yanayozuka safari hii ,hivi kuna jambo gani lilojificha hata pakatolewa onyo na vyombo kutishia amani ya wananchi ??
Kama ni wizi wa kura watu wafanyeje ? Kama kuna kuchakachua wananchi wafanye nini ,hao wanaotoa onyo hawajawaeleza wananchi ikiwa matukio ya kura au tuseme ya uchaguzi yatapindishwa wafanye nini ? Sheria hairuhusu kuhoji matokeo yakishatangazwa haswa ya uraisi ,akishatangazwa ndio imetoka.
Je kwa mikiki na makeke haya ya kuwambia wananchi watulie chali na kuridhia kila kinachotangaza ,hapaonekani kama hapa pana mgawo unataka kufanywa na kitakachogaiwa ndio hicho hicho uridhike ???
Je mnakubaliana na mavuvuzela hao ? Nakumbuka miaka yote iliyopita matokeo yalikuwa yakitolewa na yakipokewa kwa amani ,sasa hili au haya makelele yanayozuka safari hii ,hivi kuna jambo gani lilojificha hata pakatolewa onyo na vyombo kutishia amani ya wananchi ??
Kama ni wizi wa kura watu wafanyeje ? Kama kuna kuchakachua wananchi wafanye nini ,hao wanaotoa onyo hawajawaeleza wananchi ikiwa matukio ya kura au tuseme ya uchaguzi yatapindishwa wafanye nini ? Sheria hairuhusu kuhoji matokeo yakishatangazwa haswa ya uraisi ,akishatangazwa ndio imetoka.
Je kwa mikiki na makeke haya ya kuwambia wananchi watulie chali na kuridhia kila kinachotangaza ,hapaonekani kama hapa pana mgawo unataka kufanywa na kitakachogaiwa ndio hicho hicho uridhike ???