senator
JF-Expert Member
- Aug 9, 2007
- 1,924
- 66
Mgonjwa mmoja mahututi alikuwa hawezi kuongea na kuwekewa oxgen. Akawa anaombewa na Mchungaji. Akiwa anaombewa, yule mgonjwa akachukua kalamu na karatasi, akaandika na akampa yule Mchungaji. ambaye badala ya kuisoma ile karatasi, akaitia kwenye mfuko wa joho na kuendelea na maombi hadi yule mgonjwa, AKAKATA ROHO.
Mchungaji hakuisoma ile karatasi akijua kua ni wosia wa marehemu. Akasubiri baada ya mazishi kwenye kikao cha ndugu akasema; "KUNAKITU NILIPEWA NA MAREHEMU CKU NILIYOKUA NAMUOMBEA"
Akampa mmoja wa wanandugu akisome. Haya ndiyo yaliyokuwa yameandikwa na yule mgonjwa:
"UMEKANYAGA WAYA WA OXYGEN, NAKOSA HEWA".
Mchungaji hakuisoma ile karatasi akijua kua ni wosia wa marehemu. Akasubiri baada ya mazishi kwenye kikao cha ndugu akasema; "KUNAKITU NILIPEWA NA MAREHEMU CKU NILIYOKUA NAMUOMBEA"
Akampa mmoja wa wanandugu akisome. Haya ndiyo yaliyokuwa yameandikwa na yule mgonjwa:
"UMEKANYAGA WAYA WA OXYGEN, NAKOSA HEWA".