Kuwa waziri kabla ya kuapishwa kuwa mbunge

68. Kila Mbunge atatakiwa kuapishwa katika Bunge kiapo cha
uaminifu kabla hajaanza kushiriki katika shughuli za Bunge; lakini
Mbunge aweza kushiriki katika uchaguzi wa Spika hata kabla
hajaapishwa.


UFAFANUZI


1. Kwanza elewa kuwa amesha itwa Mbunge si Mteule hata kabla ya kuapa na sifa ya kuitwa Mbunge ndio inatakiwa ili mtu awe Waziri

2. Inasema kabla ya kushiriki shughuli za Bunge si shughuli za Serikali (Waziri ni sehemu ya Utendaji wa Serikali (Executive).

Hitimisho: Hao ni Mawaziri na wanawajibika kwa aliyewateuwa (Rais) kwa kusimamiwa na Waziri Mkuu.

Vipi wakiapishwa kuwa mawaziri hiyo tarehe 7 halafu wakitinga wizarani wanakuta barua kutoka Kamati ya Bunge ikimtaka Waziri aijibu yeye mwenyewe kabla ya kikao kijacho cha bunge? Au vipi kamati ya bunge ikimzukia wizarani tarehe 8 kutaka maelezo/ufafanuzi wa kitu fulani? Atajibu hiyo barua/kukutana na hiyo kamati au atasepa na kusema bado hajaapishwa kuwa mbunge ili aweze kushikiri katika shughuli za bunge?
 
Hivi kweli Kikwete anavunja
maudhui ya katiba akiwa na
macho makavu!! Mawaziri kwa
mujibu wa katiba, I stand 2 b
corrected, lazima watokane na
wabunge. Na ili utambuliwe kama
Mbunge lazima uwe umeapishwa
na Speaker. Kikwete yupo juu ya
Katiba. Anateuwa mbunge na
papo hapo anamteuwa kuwa
waziri, maana ni kwamba kampa
mtu uwaziri kabla hajawa
mbunge! Tujadili



Chini ya ibara 55 (4 ) kuhusu
Uteuzi wa Mawaziri inasema
Mawaziri na Naibu Mawaziri
wote watateuliwa kutoka
miongoni mwa Wabunge,
ibara 68 inasema 68. Kila
Mbunge atatakiwa kuapishwa
katika Bunge kiapo cha uaminifu
kabla hajaanza kushiriki katika
shughuli za Bunge; lakini
Mbunge aweza kushiriki katika
uchaguzi wa Spika hata kabla
hajaapishwa.
 
Vipi wakiapishwa kuwa mawaziri hiyo tarehe 7 halafu wakitinga wizarani wanakuta barua kutoka Kamati ya Bunge ikimtaka Waziri aijibu yeye mwenyewe kabla ya kikao kijacho cha bunge? Au vipi kamati ya bunge ikimzukia wizarani tarehe 8 kutaka maelezo/ufafanuzi wa kitu fulani? Atajibu hiyo barua/kukutana na hiyo kamati au atasepa na kusema bado hajaapishwa kuwa mbunge ili aweze kushikiri katika shughuli za bunge?

Anaweza kuijibu barua kama Waziri, au kuingia Bungeni/ kukutana na kamati ya bunge kama waziri, akaiwakilisha serikali lakini asifanye kazi za mbunge.

A conundrum!

Hapa inahitajika katiba mpya iliyo comprehensive zaidi.
 
Nimeikuta hii kule kwa Wanabidii:

"Utaratibu wa Mbunge kuapishwa hauna maana yoyote! Mbunge huchaguliwa na watu na kuthibitishwa na returning officer wa wilaya/jimbo na kumtangaza na kumpa cheti cha kuteuliwa ubunge. Vivyo hivyo wanaoteuliwa na tume kutokana na mapendekezo ya vyama kuwa wabunge viti maalum nao hutangazwa kuwa wabunge na tume. Wale wa kuteuliwa na Rais nao hupewa cheti na uteuzi na Rais.

Kwahiyo kuapishwa bungeni ni superfluous na ni kwa mbunge kuweza kukanyaga the red carpet ya bunge kama kanuni zinavyosema. Ni utaratibu ulianzishwa na Spika Msekwa alipokuwa naibu spika 1990-1995. Ni formality ya kimjengoni tu. Mbuge anakuwa mbunge anapoteuliwa na mamlaka ya uteuzi."
 
Vipi wakiapishwa kuwa mawaziri hiyo tarehe 7 halafu wakitinga wizarani wanakuta barua kutoka Kamati ya Bunge ikimtaka Waziri aijibu yeye mwenyewe kabla ya kikao kijacho cha bunge? Au vipi kamati ya bunge ikimzukia wizarani tarehe 8 kutaka maelezo/ufafanuzi wa kitu fulani? Atajibu hiyo barua/kukutana na hiyo kamati au atasepa na kusema bado hajaapishwa kuwa mbunge ili aweze kushikiri katika shughuli za bunge?

Very good Question:
Kwanza wametinga Wizarani au barua imeletwa wizarani: Yeye atakuwa anafanya kazi za Wizara si za Bunge isipokuwa Kamati ya Bunge itakuwa inafanya kazi ya Bunge. Kumbuka kuwa hapa suala ni la uajibikaji (accountability). Hiyo tume inakuwa inawajibika kwa Bunge na hiyo ni shguli ya Bunge lakini Waziri anawajibika kwa aliyemteua (Rais) kupitia Waziri Mkuu, hiyo ni shughuli ya Serikali.

Mfano mbaya ni pale ingekuwa, Spika anamteua kujumuika katika kamati ya Bunge au kufanya ziara kama Mbunge kabla ya kuapishwa? Hapo jibu ni hawezi. Mbunge anakuwa mbunge anapotangazwa na anakuwa halali kufanya shughuli za Bunge akiapishwa. Ni suala la kisheria zaidi kuliko tunavyofikiri. Naweza kufikiri kuwa mfano wake ni huu.

Mtu anamaliza BSC Medicine na Interniship anakuwa Daktari na apapaswa kuitwa hivyo; Lakini huyu Daktari ili aruhusiwe kufanya kazi ya udaktari kisheria anapaswa kuandikishwa katika rejesta ya Mdaktari na kupewa leseni (cheti) cha kupractice Medicine na Msajiri!!
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Very good Question:
Kwanza wametinga Wizarani au barua imeletwa wizarani: Yeye atakuwa anafanya kazi za Wizara si za Bunge isipokuwa Kamati ya Bunge itakuwa inafanya kazi ya Bunge. Kumbuka kuwa hapa suala ni la uajibikaji (accountability). Hiyo tume inakuwa inawajibika kwa Bunge na hiyo ni shguli ya Bunge lakini Waziri anawajibika kwa aliyemteua (Rais) kupitia Waziri Mkuu, hiyo ni shughuli ya Serikali.

Mfano mbaya ni pale ingekuwa, Spika anamteua kujumuika katika kamati ya Bunge au kufanya ziara kama Mbunge kabla ya kuapishwa? Hapo jibu ni hawezi. Mbunge anakuwa mbunge anapotangazwa na anakuwa halali kufanya shughuli za Bunge akiapishwa. Ni suala la kisheria zaidi kuliko tunavyofikiri. Naweza kufikiri kuwa mfano wake ni huu.

Mtu anamaliza BSC Medicine na Interniship anakuwa Daktari na apapaswa kuitwa hivyo; Lakini huyu Daktari ili aruhusiwe kufanya kazi ya udaktari kisheria anapaswa kuandikishwa katika rejesta ya Mdaktari na kupewa leseni (cheti) cha kupractice Medicine na Msajiri!!

Majibu ya Naibu Spika, Job Ndugai alipoulizwa:

Hata hivyo taarifa ya Ikulu haikusema wabunge hao wateule wataapishwa lini na wapi, lakini Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alipoulizwa jana alisema alisema kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge, mtu yeyote anayeteuliwa kuwa mbunge, ataapishwa katika mkutano wa Bunge unaofuata baada ya uteuzi wake, bila kujali ni mbunge wa kuteuliwa au wa jimbo.

Ndugai alisema kwa msingi huo, wabunge hao wateule wataapishwa wakati wa Mkutano wa Nane wa Bunge la Bajeti unaotarajiwa kuanza mjini Dodoma, Juni 12.

Alipoulizwa itakuwaje ikitokea wateule hao wa Rais wakateuliwa pia kuwa mawaziri na kuendelea na kazi kabla ya kuapishwa kuwa wabunge, Naibu Spika alisema kwa hali ya kawaida, hilo haliwezekani.

"Kwa mujibu wa Katiba, mawaziri watateuliwa kutoka miongoni mwa wabunge, na anakuwa mbunge mteule hadi pale anapoapishwa, na ndiyo maana baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu, kazi ya kwanza ya Bunge ni kuchagua Spika na Naibu Spika, ambao baadaye watafanya kazi ya kuwaapisha wabunge, na ndipo atateuliwa Waziri Mkuu na kisha mawaziri," alifafanua Naibu Spika

Source: HabariLeo | Rais Kikwete ateua wabunge wapya
 
"Katika Bunge" na "katika kikao cha Bunge" kuna tofauti. Kunaweza kuja tafsiri ya Spika kuwakilisha Bunge, na kiapo kinachoendeshwa na Spika kiofisi kimeendeshwa "katika Bunge" by virtue of the authority of the Speaker, lakini hakikuendeshwa "katika kikao cha Bunge"

Naibu Spika wa Bunge amesema kwamba kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge, mtu yeyote anayeteuliwa kuwa mbunge, ataapishwa katika mkutano wa Bunge unaofuata baada ya uteuzi wake, bila kujali ni mbunge wa kuteuliwa au wa jimbo. Nimeongezea habari husuka kwenye post yangu ya mwanzo kabisa.

Kuna umhimu wa kusoma kanuni za Bunge pia.
 
Maswali ya kizushi:
1.Kama hawa ni wabunge na si 'wabunge teule' kulikuwa na sababu gani za rais kuwateua kwanza kabla hajawatangaza kama mawaziri

2. Endapo waziri anaweza kufanya baadhi ya shughuli akiwa si mbunge kamili, kulikuwa na sababu gani ya Rais kuwateua wabunge kwanza. Kwanini asiwateue katika uwaziri na kisha kuwateu ubunge hapo june kwasababu kusingekuwa na athari yoyote?

3. Kwa kutumia katiba hii tuliyo nayo ni wakati gani kwa awamu zote kiongozi aliteulliwa kuwa waziri kabla ya kuwa mbunge kamili?

4. Ikitokea uwepo wa dharura sana wa bunge kukutana, je hawa walioteuliwa wataingia bungeni kama waalikwa wa bunge au wataapishwa kwanza ili washiriki shughuli za bunge?
 
Na mimi naomba ufafanuzi kuhusu katiba kifungu cha 56 cha Masharti ya kazi ya Mawaziri;

56. Waziri au Naibu Waziri hatashika madaraka yake ila mpaka
awe ameapa kwanza mbele ya Rais kiapo cha uaminifu na pia
kiapo kingine chochote kinachohusika na utendaji wa kazi yake
kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.

Je Raisi hakuvunja katiba?




 
naomba wanasheria tusaidiane hapa kama ni kuzuia uwajibikaji wa hao mawazir wasiokuwa wabunge au tumshtaki rais kwa kuvunja katiba.
 
Wadau wa katiba wanadai hata ofisini kwa spika anweza kuapishwa sio lazima ndani ya ukumbi wa bunge

sawa kwa kuwa katiba iko silent kwa ilo,ila kuteua watu yan common citizen kuwa waziri au naibu kabla ya kuapa kuwa mbunge ni kinyume cha katiba ya jamhuri tanzania...ibara ya 54(4)
 
Na mimi naomba ufafanuzi kuhusu katiba kifungu cha 56 cha Masharti ya kazi ya Mawaziri;

56. Waziri au Naibu Waziri hatashika madaraka yake ila mpaka
awe ameapa kwanza mbele ya Rais kiapo cha uaminifu na pia
kiapo kingine chochote kinachohusika na utendaji wa kazi yake
kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.

Hiki kiapo jingine nafikiri ni kile cha bunge kwa mujibu wa kanuni za bunge. Naibu Spika mwenyewe anasema kuwa haiwezekani kwa wateule hao wa Rais wakateuliwa pia kuwa mawaziri na kuendelea na kazi kabla ya kuapishwa kuwa wabunge.

Naibu spika anasema "Kwa mujibu wa Katiba, mawaziri watateuliwa kutoka miongoni mwa wabunge, na anakuwa mbunge mteule hadi pale anapoapishwa, na ndiyo maana baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu, kazi ya kwanza ya Bunge ni kuchagua Spika na Naibu Spika, ambao baadaye watafanya kazi ya kuwaapisha wabunge, na ndipo atateuliwa Waziri Mkuu na kisha mawaziri.

Wasiwasi wangu tuu ni Spika asije na hoja inayopingana na ya Naibu Spika.
 
Je, mbunge akitangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi kuwa mbunge na kabla hajaapishwa Bungeni anaweza kuteuliwa kuwa waziri? Je, kuwa waziri si ni sehemu ya mojawapo ya shughuli za Mbunge?
Mzee Mwanakijiji

Hivi kuandaa bajeti ni shughuli za bunge?, kwani bajeti inaandaliwa na waziri peke yake? Kama bajeti ni shughuli za bunge na inaandaliwa na watu wasio wabunge kama makatibu nk, kwa msingi huo mbunge mteule anaweza kuwa waziri ingawa atapingana na ibara 55.4. Labda basi neno kushiriki shughuli za bunge lina maana ya kuingia bungeni na kushiriki mijadala na siyo kuiandaa nje ya bunge.
 
Majibu ya Naibu Spika, Job Ndugai alipoulizwa:

Hata hivyo taarifa ya Ikulu haikusema wabunge hao wateule wataapishwa lini na wapi, lakini Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alipoulizwa jana alisema alisema kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge, mtu yeyote anayeteuliwa kuwa mbunge, ataapishwa katika mkutano wa Bunge unaofuata baada ya uteuzi wake, bila kujali ni mbunge wa kuteuliwa au wa jimbo.

Ndugai alisema kwa msingi huo, wabunge hao wateule wataapishwa wakati wa Mkutano wa Nane wa Bunge la Bajeti unaotarajiwa kuanza mjini Dodoma, Juni 12.

Alipoulizwa itakuwaje ikitokea wateule hao wa Rais wakateuliwa pia kuwa mawaziri na kuendelea na kazi kabla ya kuapishwa kuwa wabunge, Naibu Spika alisema kwa hali ya kawaida, hilo haliwezekani.

“Kwa mujibu wa Katiba, mawaziri watateuliwa kutoka miongoni mwa wabunge, na anakuwa mbunge mteule hadi pale anapoapishwa, na ndiyo maana baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu, kazi ya kwanza ya Bunge ni kuchagua Spika na Naibu Spika, ambao baadaye watafanya kazi ya kuwaapisha wabunge, na ndipo atateuliwa Waziri Mkuu na kisha mawaziri,” alifafanua Naibu Spika

Source: HabariLeo | Rais Kikwete ateua wabunge wapya

Duh! Aisee hakika katiba yetu ni mbovu kweli kweli.

Kwa mkanganyiko huu,katiba ndiyo ingekuwa kimbilio katika kutoa jibu. Lakini sasa,katibu ndiyo chanzo cha mkanganyiko.

Mimi pia nilifikiri "mbunge" anakuwa mbunge anapopewa cheti cha ubunge na aliyemuidhinisha,awe DED,NEC au rais. Sasa bwana Ndugai (Naibu wa Spika) anakuja na tafsiri nyingine.

Asante mkuu EMT kwa kuona hili. Shukrani zaidi kwa rais kwa kuonyesha mkanganyiko huo. Kwani nimepata hoja nyingine katika mjadala wa katiba mpya.
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mwanakijiji

Hivi kuandaa bajeti ni shughuli za bunge?, kwani bajeti inaandaliwa na waziri peke yake? Kama bajeti ni shughuli za bunge na inaandaliwa na watu wasio wabunge kama makatibu nk, kwa msingi huo mbunge mteule anaweza kuwa waziri ingawa atapingana na ibara 55.4. Labda basi neno kushiriki shughuli za bunge lina maana ya kuingia bungeni na kushiriki mijadala na siyo kuiandaa nje ya bunge.

Mkuu Feedback, Kimbunga na Mzee Mwanakijiji mmesoma maelezo ya Naibu spika niliyoongezea kwenye post yangu ya mwanzo kabisa? What do you think? Yuko sahihi?
 
Last edited by a moderator:
Kuna umhimu wa kusoma kanuni za Bunge pia. [/COLOR]

Kweli. Lakini ni hatari kama kanuni za bunge zinakuwa zinakinzana na katiba,sheria mama.

Au pengine Naibu wa Spika hafahamu miongozo kutoka kwenye katiba.

Kama kweli utaratibu wa kuapishwa bungeni sio legally binding procedure,yaani iliwekwa kama ceremonial procedure wakati wa Msekwa,basi hapo naingia katika total confusion.
 
Ibara ya 68 inasema "Kila Mbunge atatakiwa kuapishwa katika Bunge kiapo cha uaminifu kabla hajaanza kushiriki katika shughuli za Bunge" Kwa tafsiri ya haraka haraka sidhani kama mbunge anaweza kuapishwa kwenye ofisi ya spika bali katika bunge unless ofisi ya spika iko "katika Bunge".
EMT

Mimi bado nakazia mbunge anaweza kuapishwa sehemu yeyote, labda niambiwe neno 'katika bunge' ni ndani ya ukumbi wa bunge na si ofisini.
Labda niulize hivi mbunge akiwa kwenye maeneo ya bunge na si ukumbini atahesabika amehudhuria bunge?
 
Back
Top Bottom