Kuwa na Uwezo wa Kufanya Maamuzi Magumu ni Kipaji au?

Mawaiba

JF-Expert Member
Dec 11, 2011
417
150
Najaribu kukumbuka jinsi Mwl. J.K. Nyerere alivyokuwa na uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi magumu. Nina imani kabisa kutokana na uwezo mkubwa wa J.K. Nyerere katika kusoma alama za nyakati na kufanya maamuzi magumu accordingly, kama leo hii angekuwa hai Nyerere angeshauri muungano wa Bara na Visiwani uvunjwe. Miongoni mwa maamuzi magumu ambayo viongozi wetu wa sasa hawana uwezo wa kuyafanya kwa hiyari ni "kung'atuka" kutoka madarakani kama alivyofanya Nyerere. Hebu tukumbushane baadhi ya maamuzi magumu ambayo Mwalimu aliyafanya wakati wa uhai wake, ili liwe somo kwa viongozi wetu wa sasa. Karibuni....
 
Najaribu kukumbuka jinsi Mwl. J.K. Nyerere alivyokuwa na uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi magumu. Nina imani kabisa kutokana na uwezo mkubwa wa J.K. Nyerere katika kusoma alama za nyakati na kufanya maamuzi magumu accordingly, kama leo hii angekuwa hai Nyerere angeshauri muungano wa Bara na Visiwani uvunjwe. Miongoni mwa maamuzi magumu ambayo viongozi wetu wa sasa hawana uwezo wa kuyafanya kwa hiyari ni "kung'atuka" kutoka madarakani kama alivyofanya Nyerere. Hebu tukumbushane baadhi ya maamuzi magumu ambayo Mwalimu aliyafanya wakati wa uhai wake, ili liwe somo kwa viongozi wetu wa sasa. Karibuni....
Mkiwabagua mkasema wao waunguja ss watanganyika...........hotuba hii inaonyesha asingeweza kupendekeza muungano kuvunjwa!
So jipange upya kisha urudi.
 
Mkiwabagua mkasema wao waunguja ss watanganyika...........hotuba hii inaonyesha asingeweza kupendekeza muungano kuvunjwa!
So jipange upya kisha urudi.
Hiyo kauli aliyoitoa wakati huo haiendani na hali tuliyo nayo hivi sasa. Hali tete ya muungano wa Bara na Visiwani inaashiria kuvunjika kwa amani. Inatakiwa mtu mwenye uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi magumu kuweza kufanya hivyo. "Uzanzi-bara" na "Uzanzi-bari" unamaslahi gani kwa jamii inayopingana na hali hiyo. Kwa kuwa huna uwezo wa kutafakari kwa undani kaa pembeni. Watu mnaokumbatia muungano mnafanya hivyo eti kwa sababu Nyerere alisema muungano ulindwe, lakini kaeni mkijua Nyerere alikuwa flexible. Ndio maana pamoja na kuitawala Tanzania chini ya chama kimoja, lakini mwisho wa siku alishauri mfumo wa vyama vingi, mfumo ambao hivi sasa unapelekea kukua kwa demokrasia Tanzania. Na hii imetokana na uwezo mkubwa wa Nyerere katika kusoma alama za Nyakati. Ndio maana nasema hata issue ya kuvunja muungano ingekuwa simple sana kwa Nyerere.
 
Back
Top Bottom