kuwa na nyumba ndogo kuna maana gani kitaalamu?

bysange

JF-Expert Member
Jan 11, 2011
4,456
1,563
WanaJF naomba mnijibu je kuna maana yoyote kuwa na nyumba ndogo(mke au mume wa pili)maana najiuliza maswali ya kina majibu haba.
 
hakuna maana yoyote zaidi ya kuongeza shida na matatizo, huwa wanadhani watatatua matatizo lakiini mwisho wake huwa ni kuongeza zaidi ya zamani
 
msaidie tu kumjibu kwani kwake ni swali ,
nimona pete yako..it means ur not committed...oohh

Mmh just I had it on the wrong finger!Haya ngoja niwe muungwana...Nyumba ndogo haina lolote..utalazimika kuishi a double life that is nowhere close to being as exciting and as fun as a agent 007 movie!
 
At least mwenzako akijua kama una nyumba ndogo inaweza kusaidia kujenga heshima na ubunifu ndani ya nyumba
 
Nyumba ndogo hujitokeza baada ya 1. Uaminifu ktk tendo la ndoa kupungua au kutofanywa kwa ustadi unaotakiwa. 2. Unatokana na uchu wa ngono unaosukumwa na pepo la ngono. 3. Watu wa jinsi hii wanatakiwa waombewe. Si bure.
 
Upungufu wa maadili ya dini pia unachangia, kama mtu anahofu ya Mungu hawezi kukiuka taratibu za ndoa!
 
WanaJF naomba mnijibu je kuna maana yoyote kuwa na nyumba ndogo(mke au mume wa pili)maana najiuliza maswali ya kina majibu haba.

muuliza swali kaoa? kama bado hataweza kuelewa maana.asubiri akishaoa na kuonja shubiri za hawa kina dada ndo atajua ubaya na utamu wa nyumba ndogo. Long live nyumba ndogo zinaokoa sana watu kupata heart attack,unabembelezwa, unalishwa,unabebwa kama mdoli na kuogeshwa,unapikiwa ukitakacho,maneno matamu,unapewa style utakayo nk nk,thubutu yake nyumba kubwa kama unapata haya yote,utasikia nimechoka,kesho nina kazi nyingi,mara kama hutaki kula kale bar au mwombe housegirl akupikie,kukunjiwa uso kila mara,nknknkn...kazi kwako.kama ndo unaanza chuo mwaka wa kwanza siku ya kwanza unaulizia UE ya nini?
 
Natamani nipate mume ambaye hataendekeza haya mambo ya nyumba ndogo, ambaye ni mvumilivu katika udhaifu wangu, mwenye kiasi, anaidhibiti nafsi yake, na kujikana kabisa pale inapobidi.


Ambaye anaona yote ya duniani yanapita tu, kuliko kupoteza muda kumsaidia shetani kazi, awe anatumia muda wake kusali, kuomban kufunga na hata kuwafundisha wengine njia ya Mungu. Sio lazima awe mchungaji.

Kwa sababu nyumba ndogo sio nzuri kabisa.
 
wala tusidanganyane wandugu,nyumba ndogo ni pressure tupu na kuzidisha matatizo maana mtu hukosa starehe na kufanya mambo kimfichomficho tu kutokana na wasiwasi. jaribu kuichukua hiyo nyumba ndogo moja kwa moja utaona inafanya yale yale uliyoyakataa nyumba kubwa. huu ni ujinga wa kufikiri, tujue kuwa hata hizo nyumba kubwa mwanzoni zilifanya hivyohivyo kama nyumba ndogo, sasa kipi kinakuthibitishia kuwa hiyo nyumba ndogo siku zinavyozidi kusonga mbele haitabadilika?
 
nyumba ndogo ni presha ,cha msingi we mshauri mamsap/nyumba kubwa muwe mnajikumbusha the good ol days wakati mko ktk uchumba etc.
watoto mnawapeleka kwa bibi ndugu,every weekend wao kwa bibi,uncle,anti ,family freinds etc,ili muwe free for u and her only,muwe na vitu vya kufanya kwa pamoja,e.g swimming,jogging,cycling etc, vunja routine kwa mwanaume mtongoze upya and kama bado mmna nguvu nendeni disco,msikae pamoja alafu anza kupractice kutongoza vitoto vya CBE or chuo hii inasaidia ku-rejuvenet ujana,then mamsap anakuja as if amekubamba na kadem ka chuo kanaanza kupanic,ITs just a role playing ,ndo maana ndoa zinadumu kwa watu wanaofanya vitu pamoja.
Nyumba ndogo huwa inakuridhisha tu ukondoka anakuja kamjamaa anatoa Dozi ya ukweli ,sometime huwa ni mlinzi wa jirani,muuza duka,muuza maji etc.matokeo yake unapata kale kaugonjwa.
lakini ukiwe close na Nyumba kubwa with lots of activities in the weekend utashangaa mwenyewe .Thats why unaona wazungu wanenda holidays husband and wife only.
 
WanaJF naomba mnijibu je kuna maana yoyote kuwa na nyumba ndogo(mke au mume wa pili)maana najiuliza maswali ya kina majibu haba.

Bwana mdogo, mimi ni Ngariba aka mkata magovi wa kienyeji na pia ni kungwi. Watu wengi sana hawajui starehe za nyumba ndogo.
Nyumba ndogo inakuondolea pressure na tension ambayo unaipata nyumba kubwa, nyumba ndogo inakupa yale unayoyakosa nyumba kubwa.
Maisha ni mashindano. Mji mzima ukiwa na duka moja basi mwenye duka atauza kwa bei anayotaka, atafunga na kufungua duka kwa muda anaotaka. Lakini kama maduka ni mengi kutakuwa na ushindani ili kuvutia wateja.
Nyumba kubwa zinajisahau sana kutimiza wajibu wao hivyo ukiwa na nyumba ndogo unaifanya nyumba kubwa kukaa sawasawa.
Ukitaka kujua zaidi ni PM nikupe somo zaidi.
 
Back
Top Bottom