Kuvuja mitihani ya Form four kila mwaka NECTA na waziri wa elimu wajiuzulu!

baraza la mitihani ndo responsible kwa kutunga na usambazaji wa mitihani na ndo victim no.1 kwa uvujaji wa mitihani. Hao wanao shughulika na kazi ya kutunga mitihani wana watoto na ndugu zao ambao wana takiwa kufanya mitihani husika, kwanini asimpe mwanae ama ndugu yake maswali yatakayotoka kwenye mtihani ili aweze kufaulu ukizingatia hali ya sasa watoto wako busy na fecebook na bongo flava atapata wapi muda wa kujisomea!
 
Kama kuna kitu nachukia tena sana ni ile hali ya kuwaadhibu watoto ambao hawana pesa za kuiba mitihani; hawana akili za kuiba mtihani. Huku wezi ambao ni walimu wanaachwa bila kufutwa kazi na kushitakiwa mahakamani. Unaweza ukafirki kuwa Mzazi anahusika, lakini tuangalie mlinzi wa mitihani ni nani? wenye dhamana kama tumevyozoea ni nani? Utaona ni mwalimu na Baraza, sasa iweje hawa wasifutwe kazi kwa mitihani kuibiwa ile hali wanayodhamana. Iwapo mzazi anakosa kwa hiyo mtoto anaadhibiwa kwa kosa la mzazi?

Naowaonea huruma sana mtoto wa std 7 anafutiwa matokeo??? kweli nchi hii inakili hata kama mebgu ya mchicha??? mtoto anakosa gani? apewe adhabu ya kuharibu maisha yake kwa uzembe wa watu wazima, ni aibu ni aibu.

Watoto waliofutiwa wapewe matokeo yao watinge form 1 wale wanostahili, mengine nchi iyakabili kiutu uzima sio hiki kiini macho, zaidi ya yote SERIKALI Inahusika na WIZI wa MITIHANI SERIKALI inahususika, inawezekanaje serikali iruhusu elimu kuwa biashara, nani mfanya biashara kwa maana ya biashara hataki faida, wako tiyari kufanya lolote kupata faida kubwa ikiwa ni kuhakikisha watoto wanafaulu sana na hivyo wazazi kurubunika na kupeleka watoto kwenye shule hizo kwa gharama yoyote. Mzazi anadanganywa kwa matokeo mazuri wakati mtoto hamnazo harafu anaibiwa pesa kwa ada kubwa!!! serikali ipo inaona inashangaa eti mitihani inaibiwa, ELIMU ISIWE BIASHARA KUOKOA NCHI.
 
walaumiwe wanaotunga mitihani migumu,anyway.....ilaumiwe wizara ya elimu na necta. y?
1.kuna shule nyingi za kata hazina walimu,ama wapo wa aina moja tu, mfano walimu wa sanaa tu.
2.mtihani unaotungwa ni mmoja kwa nchi nzima...
swali; je huyu mwanafunzi ambaye hana walimu wa kutosha kwa nini afanye mtihani sawa na mwanafunzi
ambaye ana walimu? mfano kuna shule zingine hazina walimu wa physics,chemistry nk lakini
necta bila aibu wanaenda kuwatahini hao viumbe.....ivi mnawatahini kwa lipi? mmepanda nini
ili mvune? kwa nini mnatumia kipimo sawa cha hukumu kwa wanafunzi wenye walimu na wasio na walimu?
 
Array,ndugu yangu sipingani na wewe kwamba anayestahili lawama zote ni nectar kwa maana ya wizara ya elimu kwa ujumla maana hao ndio wenye dhamana ya kutunga kulinda na kusimamia mitihani hao ndio waliotoa ajira kwa wezi wa mitihani hivyo wenyewe ndo wezi wa mitihni,nakubaliana na wewe pia kuwa baadhi ya shule hazina walimu ama zina walimu wa namna moja na pia inavyoonekana siyo kwamba mitihani ni migumu kiasi hicho ila inavyoonekana baraza la mitihani haliko karibu sana kuangalia syllabus gani zinazofundishwa mashuleni wazitumie kutunga mitihani kutoka humo maana mtihani ni kipimo cha namna gani Yale ambayo umeshayafundisha yameeleweka hawa wanaelekea wanatunga tu mitihani wanayoijua wao ila bora iwe migumu kiasi cha kutia hofu wanafunzi wawe tayari kununua mitihani ili wasifeli maana wameshajenga imani kuwa watakachokikuta ktk mitihani hawajawahi kufundishwa,nao wasahishaji mitihani wanasahihishaji nnao wanasahihisha kama computer hawatizami uelewa wa mjibu swali kwa mfano ameulizwa whtz the history usipojibu ni past events kama ulivyosomaa kwenye kitabu hata kama utatoa jibu kwa namna inginne inayolink na hiyo utakosa .wote hawa wanapaswa kujipanga upya kwa maana ya kuwa organised walimu, watunga mitihani na wasahihishaji.
 
Baraza la mtihani ndo wa kulaumiwa kwani kwa hali ya sasa mtihani unavuja dar na baada ya nusu saa umefika nchi nzima kwa njia mbalimbali za mawasiliano.Je hapo mwalimu msimamizi wa mtihani atafanya nini? Kama tayari wanafunzi wote wana majibu?Ingawaje kuna wakati baadhi ya walimu wanachakachua mtihani ili shule ipate sifa kutokana na kubanwa na maofisa wao
 
1: Rais Mwizi Fisadi.
2: Waziri Mkuu kapoteza Imani Bungeni.
3: Waziri wa Elimu ana Undugu na Rais.
4: Chama cha Walimu Kinaidai Serikali.
5: Polisi wanolinda Mtihani Mshahara Mdogo.

Unataka Ndalichako afanye nini na Necta yake kama si kumuonea huruma kwani hata hapo alipofika kajitahidi.

Kuvuja kwa Mtihani ni swala la kawaida sana kwa Sababu hizi 5.
 
Siku hizi shule za Ilboru,mzumbe,tabora boys na kibaha hazifanyi vizuri sana kwenye matokeo ya mitihani ya taifa kama inavyotegemewa ukizingatia wanapewa wale wanafunzi ambao wamekuwa top layers . kama kipindi nasoma Ilboru pale Pcm kila mtu alikuwa na AAA na wachache AAB kwenye hiyo Pcm. Ila sasa hzo A's nyingi zilikuwa za uongo kwani hao wanafunzi walikotoka wengi walipewa majibu ama walikuwa na mitihani kabla na ndo hao mwishoni wanakuja kutoka na 4 na 0 kibao. Form 4 ndo usiseme unakuta wanafunzi wanaopelekwa form 1 pale ni wale top 5 wa kila wilaya lakini cha ajabu mtu hata kusoma vizuri inamsumbua ila unasikia eti ndo alikuwa wa kwanza labda kwenye manispaa ya kinondoni. JAMANI NECTA KUWENI MAKINI.
 
Hivi jamani na tujiulize huku kuvuja kwa mitihani ni kosa la nani ?
Na inakuwaje wanafunzi ndio wanaobebeshwa lawama hadi kufika kufutiwa mitihani yao na kutelekezwa ?
Je mwananfunzi anapobahatika kuona mtihani ambao ataufanya siku mbili tatu zijazo ,ataupuuza au ataona
hii ni bahati ya mwaka ? Hata mwanafunzi alie na akili za kufaulu pindipo akisogezewa mtihani uliovuja basi hata wacha kuuangalia na kuufanyia kweli.

Baraza la mitihani linapokaa kwenye vyombo vya habari na kuanza kuonyesha madudu ya wanafunzi na kuuhakikishia umma kuwa wanafunzi hao waliiba mtihani ? Hivi walimuibia nani ? Walivunja ofisi za wizara ? Walitekagari inayobeba mitihani ? Naona baraza hili na utitiri mzima hadi kwa Waziri wanajificha na kufinya uzembe uliotokea ndani ya Vyombo vyao kwa kushindwa kuudhibiti mtihani huo usivuje.

Ikiwa mtihani umevuja hivi ni sawa kuwabana wanafunzi na kuwazuia kufanya tena mtihani yaani nionavyo huku ni kuwapotezea muelekeo wa maisha yao kwa kosa ambalo sio lao.

Hivi Wizara imeshindwa kuchunguza au kutuma vyombo vya uchunguzi kubaini ni nani aliehusika na uvujaji wa mitihani ? Na badala yake kuwakaba wanafunzi kwa kuwakatishia masomo yao ? Kuna nchi moja huko uarabuni imebaini kuwa mtihani umeibiwa ,tangazo la mwanzo ni kuwa result imefutwa na wanafunzi watafanya tena mtihani na uchunguzi unafanyika kujua ni nani alihusika kwa kuvuja kwa mitihani na sheria kuchukuliwa ,wanafunzi hawakuguswa wala kuadhiriwa zaidi ni kuwa watatajiwa tarehe ingine ya kufanya mitihani ,Hapa Tz sipo ni kulinda wizara na wafanyakazi wake kwa kuwatelekeza wanafunzi. Je ni haki ?
 
Hao wahusika wakuu hawataki tu, kudhibiti hiyo hali. Serikali kama ikitaka jambo lake lifanyike litafanyika tu bila mizengwe wala kupoteza muda.

Hao watayarishaji wa mitihani wanajulikana, wanaoingiza Data kwenye Computer wanajulikana, wachapishaji wanajulikana, wanao hifadhi hiyo mitihani pia wanajulikana. Sasa tatizo liko wapi?
Mbona hatujawahi kusikia kuwa PESA mpya zinazo chapishwa zimepotea?

Siku Serikali itakapo amuwa kuwaadhibu wale wote wanao husika na UFISADI huu, tena kwa adhabu ya kupigiwa mfano, watakao fuwata watatia akili.

Angalieni mfano wa nchi ya China, mafisadi wanawafanya nini. Serikali ijifunze kutoka kwao.
Si walishasema kuwa watamlinda Ndalichako kwa nguvu zote?
 
Hivi jamani na tujiulize huku kuvuja kwa mitihani ni kosa la nani ?
Na inakuwaje wanafunzi ndio wanaobebeshwa lawama hadi kufika kufutiwa mitihani yao na kutelekezwa ?
Je mwananfunzi anapobahatika kuona mtihani ambao ataufanya siku mbili tatu zijazo ,ataupuuza au ataona
hii ni bahati ya mwaka ? Hata mwanafunzi alie na akili za kufaulu pindipo akisogezewa mtihani uliovuja basi hata wacha kuuangalia na kuufanyia kweli.

Baraza la mitihani linapokaa kwenye vyombo vya habari na kuanza kuonyesha madudu ya wanafunzi na kuuhakikishia umma kuwa wanafunzi hao waliiba mtihani ? Hivi walimuibia nani ? Walivunja ofisi za wizara ? Walitekagari inayobeba mitihani ? Naona baraza hili na utitiri mzima hadi kwa Waziri wanajificha na kufinya uzembe uliotokea ndani ya Vyombo vyao kwa kushindwa kuudhibiti mtihani huo usivuje.

Ikiwa mtihani umevuja hivi ni sawa kuwabana wanafunzi na kuwazuia kufanya tena mtihani yaani nionavyo huku ni kuwapotezea muelekeo wa maisha yao kwa kosa ambalo sio lao.

Hivi Wizara imeshindwa kuchunguza au kutuma vyombo vya uchunguzi kubaini ni nani aliehusika na uvujaji wa mitihani ? Na badala yake kuwakaba wanafunzi kwa kuwakatishia masomo yao ? Kuna nchi moja huko uarabuni imebaini kuwa mtihani umeibiwa ,tangazo la mwanzo ni kuwa result imefutwa na wanafunzi watafanya tena mtihani na uchunguzi unafanyika kujua ni nani alihusika kwa kuvuja kwa mitihani na sheria kuchukuliwa ,wanafunzi hawakuguswa wala kuadhiriwa zaidi ni kuwa watatajiwa tarehe ingine ya kufanya mitihani ,Hapa Tz sipo ni kulinda wizara na wafanyakazi wake kwa kuwatelekeza wanafunzi. Je ni haki ?

Mitihani ilivuja mara ya mwisho mwaka 2008.

Matukio mengine yanayotokea miaka ya hivi karibuni ni udanganyifu kwenye vituo vya mitihani na kwenye vyumba vya mitihani. Na hii ni ngumu kwa NECTA kuidhibiti kwa kuwa NECTA haina watendaji vituoni.

Ni jukumu la jamii nzima: Wazazi, Walimu, Maafisa Elimu na Walinzi wa Usalama kwenye vituo vya mitihani kudhibiti udanganyifu huo.

Lazima tukubali kuwa Uongozi huu wa sasa wa Baraza la Mitihani umejitahidi sana kudhibiti uvujaji wa mitihani kulinganisha na ilivyokuwa kabla ya 2006. Kudhibiti huko si kwamba kunapokelewa vizuri na watu wote. Kuna watu wenye pesa ambao wangetamani kupata mitihani hiyo na wanakosa. Kuna wamiliki wa shule ambao nao wangetamani kupata mitihani hiyo kabla na wanashindwa na wanaishia kupiga vita anayedhibiti mitihani hiyo isivuje.

Kama kuna mtu ana ushahidi wa mass leakage ya mitihani naomba anipe data lini na wapi na somo gani mtihani ulivuja nje ya niliyotaja hapo juu.
 
Back
Top Bottom