Kuunga kwetu Zimbabwe hakuna mjadala - Kikwete,

Kwa hiyo mnataka kusema nchi kama Namibia na Afrika Kusini nao wanyakue ardhi kutoka kwa wazungu? Hilo ndilo mnalotetea hapa? Nadhani watu wamesahau hapa kwamba ardhi sio ishu kwa Zimbabwe sasa. Ni Mugabe ametumia kisingizio hicho ili kubaki madarakani na kutafuta ushawishi wa nchi za kiafrika kumuunga mkono.

Hivi kaka Mkandara una habari kwamba sasa hivi kuna makampuni makubwa ya kichina, Saudi Arabia na canada yananunua mashamba makubwa dunia kote a na kuwekeza kwenye kilimo cha mazao ya chakula? Mfano mmoja ni Madagascar ambao hekari zaidi ya milioni 1 zimeshanunuliwa. Wakati watu wanafikiria kuwekeza katika kilimo sisi wengine na viongozi wetu (akina Mugabe) tunaongelea kuirudisha thamani ya ardhi katika enzi za ujima. Kwamba heri ibaki bure kuliko mzungu aitumie kuzalisha!

Sioni busara ya kumnyang'anya raia ardhi kutokana na rangi ya ngozi yake na kumpa raia mwingine asiye na rasilimali wala mtaji wa kuiendeleza, eti kwa sababu tu ni mweusi. Suala la ardhi kwa sasa ni la kiuchumi zaidi kuliko hapo awali tulipokuwa tunapigania uhuru ambapo lilikuwa ni la kisiasa. Huko tumeshatoka jamani. Watu wanataka ajira, nyumba bora, elimu bora na hospitali bora. Ardhi isiyo na tija sio lengo kwa sasa. It is just another white elephant!

Angalia Zimbabwe sasa, baada ya kupewa ardhi eti ndio wanakufa njaa! What a shame!
 
Wakuu, matatizo ya Zimbabwe yalipamba moto rasmi mwaka 2002. Kipindi kifupi kabla ya uchaguzi mkuu, Mugabe alianza kutofautiana na wafanya biashara wakubwa wa nchi hiyo (Wazungu) ambao walilaumu sana sera zake za uchumi. Kipindi hicho pia, Mugabe alihitaji sana support ya watu hao wenye pesa zaidi. Kwa kuwa hilo lilishindikana, akaona njia mbadala ni kurudi nyuma na kuangalia loopholes anazoweza kuzitumia kupata ushindi (ikumbukwe kuwa Mugabe mwaka ule alikuwa anaelekea kushindwa kabisa uchaguzi mkuu). Ndipo alipogeukia suala la ardhi, ikiwa ni njia ya kuwakomoa wazungu aliokuwa wakimpinga na pia kujenga hoja zinazokubalika na wananchi wa Zimbabwe na hivyo kumpa ushindi. Ukweli ni kwamba, alishinda uchaguzi ule kwa mbinu yake hiyo. Na aliungwa mkono na asilimia kubwa ya Wazimbabwe katika hatua ya kunyang'anya ardhi kwa lengo la kuigawa kwa wananchi wake.

Tatizo kubwa likajitokeza kwa namna ardhi ile ilivyogawiwa. Iligawiwa kwa wananchi kwa upendeleo mkubwa. Hasa kwa kuzingatia milengo ya kisiasa na support katika ushindi wake. Wale walioonekana kutompa support, waliwekwa pembeni na kubaguliwa. Na hata rasilimiali nyingine pia ziligawiwa kwa misingi hiyo. Ni ukweli wa dhahiri pia kuwa ardhi ile haikuzalisha kama ilivyotarajiwa. Kwani Wazimbabwe wengi hawakuwa na uwezo wa kuiendeleza, na wala hawakuwa tayari (hawakuandaliwa) kufanya hivyo. Hivyo, ikabaki kuwa mapori makubwa hadi sasa.

Uingiliaji wa mataifa ya ulaya (hasa UK) na marekani katika kuweka shinikizo kupinga unyang'anywaji wa ardhi ulichangia sana kuporomosha uchumi, ustaarabu na utulivu uliokuwepo Zimbabwe. Uingereza ilianza kuchukua hatua baada ya wazungu walionyang'anywa ardhi kukimbilia Uingereza kulalamika (kumbuka wazungu wale walikuwa na uraia wa UK pia).
 
Wazungu hawataki Waafrika tujue kinachoendela duniani. Wameimaliza Zimbabwe kwasababu Mugabe hawaheshimu wazungu(UK). Wazungu walipoitawala Afrika hawakujenga shule, barabara na hospitali. Wazungu ndiyo waliosababisha Afrika kuwa maskini sana. Wamechukua mali zote za serikali gold, diamond na wafanyakazi wote bora (watumwa). Wanafanya mbinu zote ili Mugabe ashindwe kutawala. Je wanamtesa Mugabe au wananchi wa Zimbabwe na Afrika nzima? Wanairudisha nyuma Afrika nzima kimaendeleo. Afrika na nchi zote za south zitaendelea kuteseka mpaka pale nchi za Afrika zitakapuwa na umoja wa kibiashara.
 
Nurujamii,

Tafadhali rejea posts za hawa wafuatao ili uweze kulielewa tatizo la Zimbabwe vizuri: Bulesi, Augustine Moshi and Field Marshall ES.

N.B. Sidhani kama wazungu walifanya madudu kule Asia kama walivyofanya Zimbabwe. Kwa mfano, hawakuivamia China, Malyasia, Singapore, South Korea e.t.c na kupora ardhi yote yenye rutuba huku wakiwaacha wazawa bila ardhi. I think, there partnership has more to do with trade than otherwise.

Tumeshuhudia hapa JF watu kukwaruzana kwasababu ya dini...Waafrika tujifunze...Nadhani Mchina alijifunza...Kwasababu mpaka sasa wana mgogoro na Vatican kwasababu wao wanasema Askofu atateuliwa ama kuchaguliwa na wachina na si Vatican...UNAONA?
Hapo kuna la kujifunza.
 
Nurujamii,

... Ukisikiliza kampeni nzima ya Mugabe wakati ule ilikuwa kuhusu Uingereza tu, utafikiri alikuwa anagombea Urais against Prime Minister Blair! na wananchi wakamsikia kwani kila Blair akibwabwaja Mugabe anaitoa ktk Luninga..Matokeo yake Mugabe alishinda kwa asilimia 120 of 150 seats wakati mwaka 2000 Mugabe alishinda viti 63 tu kati ya viti 120...kila mtu alijua Mugabe anaondoka uchaguzi unaofuata..

...hivi huyu Mugabe si alishindwa uchaguzi akakataa kutoa matokeo?wewe Mkandara acha propaganda Mugabe alishindwa na waliopiga kura ni Zimbabweans sio waingereza kwa hiyo swala la Blair hapo halipo,Mugabe ndio tatizo la ile nchi na siasa zake za kibaguzi na sio Blair wala wazungu,hiyo ardhi itarudi kwa utaratibu sio huyo ndugu yako aliyetimua wazungu(wazimbabwe) then akagawa kwa militants wake
 
Back
Top Bottom