Kuuawa kwa mwanae Ennis – Ulikuwa ni mwaka wa mikosi wa mwigizaji Bill Cosby

Kifo cha Ennis ndiyo kimetokea na hakuna awezaye kumrejesha duniani. Lakini yapo maswali ya kujiuliza. Inakuwaje mtu anapata pancha njiani, kisha anaamua kubadilisha tairi la gari lake, halafu anatokea mtu mwingine ambaye anaamua kumpiga risasi na kumuua……! Kwa sababu gani hasa….? Yaani fedha kidogo ambazo hata hivyo hakuweza kuzichukuwa ndiyo zitoe uhai wa mtu…..?
1. Kwa mujibu wa taarifa za kiuchunguzi, Bwana Mikail alikuwa akifanya kazi katika mgahawa uliokuwa karibu na maeneo ambayo mauaji yalifanyika. Katika dhana pana ya udhibiti wa kiuhalifu, ili tukio lolote la kihalifu litokee mambo matatu lazima yatokee:

1. Mazingira yanayoweza kusababisha uhalifu kutokea
2. Mhalifu pia lazima awepo kwa ajili ya kutekeleza uhalifu
3. Mtendewa uhalifu (victim)
2. Vilevile suala la namaa uhalifu unavyoweza kutokea liko ndani ya maamuzi ya mhalifu mwenyewe ingawa kuna wakati kuna baadhi ya matukio yanatokea bila ya ridhaa ya mhalifu mwenyewe. Kwa mfano mhalifu anaweza kuingia ndani ya nyumba kwa lengo la kupora mali/fedha lakini wakati wa purukushani, na hasa ukitokea upinzani wakati wa uhalifu anaweza kuua.

3. Suala la pesa kidoogo haliondoi nia ya mhalifu kutekeleza uhalifu wake. Mfano mdogo ni mtu na mkewe waliokwenda kilabuni na pesa kidogo kwa ajili ya kunywa pombe za kienyeji na nauli ya kurejea nyumbani kwao. Ulipofika usiku wa manane wakati wanarejea wakagundua hata pesa ya nauli wametumia. Walianza kutembea kwa miguu kurejea nyumbani ndipo kundi la wahalifu liliwavamia kwa nia ya kuwapora na hawakufanikiwa kupata chochote ndipo kwa hasira wakawajaza michanga vinywani mwao hadi wakazimia na asubuhi yake wakajikuta hospitalini. Mfano mwingine ni aina ya uhalifu wa kubahatisha unaofanywa na wahalifu wa Manispaa ya Mtwara - Mikindani. Wahalifu hawa maarufu kama tukale wapi mara nyingine huwavizia watu wanaorejea majumbani mwao kutoka katika starehe zao. Mara lango linapofunguliwa wao huingia pamoja na gari lakini si kuwa mara zote wanafanikiwa. Cha kujifunza hapa ni kuwa mara zote ni muhimu kuwa makini na mazingira ya aina zote ambayo kwa namna moja au nyingine waweza kufikiri uhalifu unaweza kutokea.

Tabia za kihalifu kwa Bwana Mikail ilijengeka toka utoto wake. Mazingira ya shule pia yalipalilia sana tabia zake za kiuhalifu. Hadi anaanza kufanya kazi alikwishakuwa mhalifu mzoefu. Wazazi wanapaswa kuwa makini sana na tabia za watoto wao ili kuepukana au kupunguza kundi la wahalifu ndani ya jamii yetu.

utaalamu wa kutambua watendaji wa uhalifu kwa kutumia vinasaba DNA ni njia rahisi sana ya kuwatambua wahalifu halisi badala ya kuwavictimise hata wasiokuwa wahalifu (wahalifu wa kusingiziwa ni tatizo kubwa katika nchi yetu). Bwana Mikail alichunguzwa pia kwa njia hii na iligundulika katika kofia/matambara aliyozungushia katika bastola aliyoitumia kufanyia mauaji ya ENNIS.

HATA UKIWA JAMBAZI SUGU KIASI GANI HALI YA UTU BADO IKO KATIKA KILA MOYO (WITH NO REGARD NI NDOGO KIASI GANI). BWANA MIKAIL ALIKIRI KWA MAKOSA ALOFANYA NA KWA KUTAMBUA KUWA ALIKUWA AMELIFANYA KOSA ALIAMUA KUONDOA NA RUFAA YAKE

Nashukuru sana Mtambuzi kwani nakumbuka sana visa na mikasa ya kiuhalifu niliyowahi kuisikia miaka ya nyuma. Twasubiri mikasa mingine mingi zaidi

The Listener - Ex - detective
Ahsante mkuu The Listener kwa ufafanuzi wako mahiri.
Nafurahishwa sana na maoni yako uyatoayo katika makala hizi za kila Ijumaa.....................
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom