WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 956
Kuuaga umaskini Tanzania, ni kazi kweli kweli.Fikiria haya yafuatayo:
kwa mwendo huu, umaskini unapungua?
- Asilimia 50% ya idadi ya watu Tanzania ni wale wenye umri chini ya miaka 18.Hii inaashiria fertility rate kubwa sana. Asilimia 49% wakiwa kati ya miaka 15-64 ambao ni umri wa kuzalisha. Hii ina maana kuwa nusu ya watanzania bado hawako katika nafasi ya kuchangia ukuaji wa pato la taifa na hatimaye kuuondosha umaskini.Cha kusikitisha zaidi ni kuwa, katika kila watu 100 walio katika kundi la kuweza kuzalisha, ujue kuna watu 104 ambao ni tegemezi.Just think about the age dependency ratio here in relation to growth and poverty reduction.
- Robo ya households, zinaongozwa na wanawake ambao inasemekana ni maskini zaidi ukilinganisha na wanaume.
- Asilimia, 3% ya watoto chini ya miaka 18 wamepoteza mzazi mmoja, ambapo asilimia moja ya wale chini ya miaka 18 wamepoteza wazazi wote.Hii inaonyesha kiwango cha uyatima na mzigo wa kulea watoto yatima.
- Ni asilimia 11% tu ya household Tanzania zenye umeme, Mijini ni aslimia 38 tu ndio wana umeme
- Asilimia 80 ya household bado wanatumia vyoo vya shimo ( pit latrines).Ni asilimia 3 tu ndio wanatumia vyoo vya kisasa (modern flush toilets) !!
- Asilimia 30 wanaishi kwenye nyumba ya chumba kimoja cha kulala wakati asilimia 37 wanaishi nyumba ya vyumba viwili vya kulala.
- 4/10 households za mijini Tanzania bara wanaishi nyumba yenye chumba kimoja tu cha kulala.
kwa mwendo huu, umaskini unapungua?