Bajeti ya wizara ya kilimo, ushirika na masoko imeshindwa kupitishwa kwa sababu idadi ya wabunge wanaostahili kuwemo bungeni ili kupitisha bajeti haikufikiwa. Quorum inayotakiwa ni wabunge 175 lakini leo hata baada ya jitihada za kuwapigia kengele wabunge walioko nje waingie ndani idadi ilikuwa 110. Hapa la kujiuliza wabunge wengine walikuwa wapi? au kutohudhuria ni kutokana na wao kutokubaliana na bajeti hiyo ila wakakosa ujasiri wa kuipinga bungeni. Hii ni anasa ya gharama sana kwa mlipa kodi masikini wa kitanzania.