Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,060
- 22,755
Tuanze kwa kujikumbusha huyu msemaji wa Polisi, Mrakibu Msaidizi wa Polisi Mama Advera Senso alivyosema kuhusu kifo cha Mwandishi, Daud Mwangosi;
- Mwandishi alikuwa akikimbia kutoka upande wananchi na kuelekea walipokuwa Polisi.
- Marehemu inasemekana alipigwa na kitu ambacho mpaka sasa hakijafahamika bado mpaka uchunguzi ufanyike.
- Kuna kitu kilirushwa kikitokea upande wa Wananchi na kumfikia ambacho kilimjeruhi pia Askari akiwamo Mkuu wa kituo cha Polisi.
- Jeshi la polisi limewakamata 32 waliokuwa wakienda Mbeya kwenda kufanya vurugu, wakitokea Iringa kuhusiana na kifo cha Daudi Mwangosi.
Mpaka sasa najiuliza...hivi hali ingekuwaje kama picha zinazoonesha jinsi tukio zima lilivyotokea hazingekuwepo, lakini sipati jibu. Lililo wazi kabisa ni kwamba Chadema ingejikuta katika hali ngumu kweli kweli kwa sababu ingehusishwa moja kwa moja na kifo cha mwandishi Daud Mwangosi. DW, BBC, Aljazeera na vyombo vingine vya habari vya nje habari kuu ingekuwa Tanzania, kisiwa cha amani, yakabiliwa na hatari ya machafuko kutokana na kitendo cha chama cha vurugu...Chadema kumuua mwandishi wa habari.
Mpango ulisukwa ukasukukika na kuna watu wanalaani kwa nini haukufanikiwa kama ulivyopangwa na mbinu bado zinatafutwa za kuwajumuisha viongozi wa Chadema na kifo hiki. Lakini Mungu mkubwa...safari hii akasema imetosha, watu wangu wameteseka vya kutosha mikononi mwa hawa waovu! Watanzania tumepewa ishara na ndio sababu kubwa wasimamizi wakuu wa mpango huu hawawezi kutoa tamko lolote hadi sasa kwani giza nene limetanda mbele ya macho yao, wamepigwa butwaa na midomo imewakauka.
Sasa wameachiwa mavuvuzela kama Tendwa, Nape, Tambwe Hiza, Yusuf Halimoja, na vikaragosi vingine tunavyovishuhudia humu jamvini wakiongozwa na zomba, Ritz na wengineo. Lakini safari hii wamegonga mwamba na hawana pa kutokea, laana inawaandama kama kivuli na muda si mrefu wataanza kuumbuana kwani damu ya Daud Mwangosi haitowaacha wapate usingizi. Msemaji wa Polisi, ASP Advero Senso kaa chonjo, matamko unayoyatoa ni sawa na ya aliyekuwa msemaji wa Sadam Hussein, Tarik Aziz!