Kutoka Mtwara

Status
Not open for further replies.

Kaa la Moto

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
7,903
1,053
Wakuu kwa wiki mbili zilizopita nimekuwa sipo jf kwani nilikuwa safarini Mtwara kwa shughuli maalum na bahati mbaya sikupata hata nafasi ya kuingia internet cafe. Kila nilipojaribu kutafuta zilipo sikupata na muda wa shughuli yangu haukuniruhusu kupata wasaa huo.

Nilijisikia kweli kumiss corner hii ya jf niliyoizoea.

Niliwamiss members wengi wa jf kama akina NN na yoyo, mkandala, omutwale, lunyungu. invisible, junius, ngekewa, na siwezi kumaliza orodha yote hapa............

Ninayo mengi ya kusema kuhusu Mtwara na picha kiasi za kuvutia za Mtwara.

Mji ulio pembezoni mwa bahari ulio na beaches nyingi sana tena nzuri hata kupita hizi chafu zilizojaa harufu za Dar lakini zikiwa na wananchi maskini kweli kweli.

Kwa kuwa sijapata muda mzuri nitakuja siku ingine kuelezea zaidi na kuweka picha.

Sasa hivi niko safarini so stay tuned.
MF
 
Wakuu kwa wiki mbili zilizopita nimekuwa sipo jf kwani nilikuwa safarini Mtwara kwa shughuli maalum na bahati mbaya sikupata hata nafasi ya kuingia internet cafe. Kila nilipojaribu kutafuta zilipo sikupata na muda wa shughuli yangu haukuniruhusu kupata wasaa huo.

Nilijisikia kweli kumiss corner hii ya jf niliyoizoea.

Niliwamiss members wengi wa jf kama akina NN na yoyo, mkandala, omutwale, lunyungu. invisible, junius, ngekewa, na siwezi kumaliza orodha yote hapa............

Ninayo mengi ya kusema kuhusu Mtwara na picha kiasi za kuvutia za Mtwara.

Mji ulio pembezoni mwa bahari ulio na beaches nyingi sana tena nzuri hata kupita hizi chafu zilizojaa harufu za Dar lakini zikiwa na wananchi maskini kweli kweli.

Kwa kuwa sijapata muda mzuri nitakuja siku ingine kuelezea zaidi na kuweka picha.

Sasa hivi niko safarini so stay tuned.
MF
ok ok thanx mkuu afadhali na hizo picha tutakumbuka mbali sana,nilifika pale mwaka 1998 kipindi mkuu wa mkoa aliitwa musa kaisi,ni kweli beach safi sana na hotel kubwa iliitwa tingatinga sijui bado ipo au?na kuna baa ya vigogo wa huko inaitwa mk bado ipo?na pale mikindani beach wale wenyeji wameacha tabia ya kukimbilia bichi kupata haja kubwa badala ya kujenga vyoo?usisahau picha ya ule mlango wa barabarani wakati unaingia lindi,pia daraja la mkapa
 
Huyo mkuu wa mkoa sio Musa Kaisi ni Nsa Kaisi.Majina ya Kyela hayo mdau matamshi yake ndo yanapelekea mtu afikiri ni MUSA!Huyo jamaa ni komandoo kamili alisoma Cuba na kufuzu with flying colors akaja na personal letter toka kwa Rais Castro akimueleza Nyerere jinsi Nsa alivyo extraodinary!
 
Huyo mkuu wa mkoa sio Musa Kaisi ni Nsa Kaisi.Majina ya Kyela hayo mdau matamshi yake ndo yanapelekea mtu afikiri ni MUSA!Huyo jamaa ni komandoo kamili alisoma Cuba na kufuzu with flying colors akaja na personal letter toka kwa Rais Castro akimueleza Nyerere jinsi Nsa alivyo extraodinary!
yaah asante kwa masahihisho mkuu na yule jamaa hata maamuzi yake yalikua ya kikomando tu maana nakumbuka tulienda kwaajili ya mkapa na muluzi walikua wanakabidhiana bandari ile muluzi atumie,jamaa akapiga mkwara kwamba hakuna kupika pale ikulu ndogo wakati lunch inahitajika sasaba kamili kwa waheshimiwa,ilibidi aje mbabe mwingine kutoka ikulu kutwambia lunch iwe tayari mda huo huyo kaisi ataongea nae yeye ndo kazi ikafanyika,namkumbuka sana huyo komandoo
 
Huyo mkuu wa mkoa sio Musa Kaisi ni Nsa Kaisi.Majina ya Kyela hayo mdau matamshi yake ndo yanapelekea mtu afikiri ni MUSA!Huyo jamaa ni komandoo kamili alisoma Cuba na kufuzu with flying colors akaja na personal letter toka kwa Rais Castro akimueleza Nyerere jinsi Nsa alivyo extraodinary!

Unachosema una uhakika nacho?. Mimi nimefanya kazi na NSA Kaisi Singida wakati huo akiwa LT col.

Ninavyoojua Nsa Kaisi sio Graduate na hata maamuzi yake ni ya moja kwa moja (Amri) kama walivyokuwa wanajeshi wengine. Sifa ninayompa na nilimpenda ni mtu anayejali sana muda hana mchezo katika time.

Kama kuna mtu yoyote atamuona basi mpe jina Hamza Yousuf ( alizoea kuniita Mwarabu wa Zanzibar) mimi nilikuwa namwita Malafyale
 
Wakuu niliahidi hapa kuwaletea habari na picha toka Mtwara na nimeanza kuziweka kule kwenye jukwaa la Jamii pichaz. Bado nakumbuka ahadi yangu.
 
Huyo mkuu wa mkoa sio Musa Kaisi ni Nsa Kaisi.Majina ya Kyela hayo mdau matamshi yake ndo yanapelekea mtu afikiri ni MUSA!Huyo jamaa ni komandoo kamili alisoma Cuba na kufuzu with flying colors akaja na personal letter toka kwa Rais Castro akimueleza Nyerere jinsi Nsa alivyo extraodinary!


Jina kamili la huyo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa ni Nsajigwa Mwakaisi,naye akalifupisha kwa kujiita Nsa Kaisi. Amekwishastaafu Utumishi serikalini.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom