Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Maeneo mengi ya mipakani na hasa ambako kulikuwa na vita vya ukombozi wa nchi jirani na Tanzania minara ya jinsi hii imejengwa kama kumbukumbu ya wapiganaji wetu. Kama inavyoonyesha mnara huu uliopo uwanja wa mashujaa Mtwara.
Baba huyu amepozi na Samaki wake akitoka kuvua. Angalia na wakina mama wale mbele yake nao wanatoka kutafuta samaki hasa kwa ajili ya biashara. Samaki Mtwara ni wengi na biashara hii inafanyika kwa wingi na hasa wakina mama wanaouza samaki wa kukaanga. Mkoa una utajiri mkubwa wa samaki.
Mibuyu ni miti inayoupendezesha mji huu wa Mtwara kwani imetapakaa kila mahali.
Uvuvi ni sehemu ya maisha ya watu wa Mtwara. Lakini hapana viwanda vya Samaki kama vile vilivyojazana Kanda ya ziwa. Kwa nini?
Kama kawaida usafiri wa Bajaj ndio usafiri wa kutumainiwa na wakazi wa mji wa Mtwara. Hakuna daladala kama za Daresalaam.
Baba huyu amepozi na Samaki wake akitoka kuvua. Angalia na wakina mama wale mbele yake nao wanatoka kutafuta samaki hasa kwa ajili ya biashara. Samaki Mtwara ni wengi na biashara hii inafanyika kwa wingi na hasa wakina mama wanaouza samaki wa kukaanga. Mkoa una utajiri mkubwa wa samaki.
Mibuyu ni miti inayoupendezesha mji huu wa Mtwara kwani imetapakaa kila mahali.
Uvuvi ni sehemu ya maisha ya watu wa Mtwara. Lakini hapana viwanda vya Samaki kama vile vilivyojazana Kanda ya ziwa. Kwa nini?
Kama kawaida usafiri wa Bajaj ndio usafiri wa kutumainiwa na wakazi wa mji wa Mtwara. Hakuna daladala kama za Daresalaam.