Kutoka CUF Makao Makuu...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Ripoti ya Awali Kuhusu Matukio Yasiyo ya Kawaida Katika Zoezi la Upigaji Kura kwa Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Magogoni, tarehe 23 Mei, 2009


Wapendwa Wanahabari,

Wakati upigaji kura kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa jimbo la Magogoni, lililo kwenye Wilaya ya Magharibi, Unguja, ukiendelea hivi sasa, tunatoa tarifa ya mwanzo inayohusu matukio yasiyo ya kawaida yanayohusiana na uchaguzi huu.

I. KITUO CHA WELEZO SKULI


  • Aliyekuwa OCD wa wilaya ya Mjini, Bwana Nurdin, amewapeleka watu ambao si wakaazi halali wa jimbo la Magogoni kwa sheha wa shehia ya Welezo, Bi Mgeni, kwa ajili ya kupatiwa shahada za kupigia kura.
  • Sheha, Bi Mgeni, anapeleka watu wasiokuwa na shahada za kupiga kura na anasimamia kuwapigisha kura. Angalau watu watatu (miongoni mwa hao waliopelekwa) wamesharipoti katika ofisi zetu kuthibitisha hili.
  • Katika Chumba Na. 4, wapiga kura wanapewa shahada mbili za kupigia kura. Kwa uchache, watu wanne wamesharipoti kwetu kwamba wamepewa shahada mbili mbili.
  • Katika Chumba Na. 5, wapiga kura wamegundua kwamba karatasi zao za kupigia kura haziandikiki. Ni baada ya kujaribu mara zaidi ya tatu, ndipo kwa mbali alama waliyoweka imejitokeza
  • Saumu Kitwana Mussa mwenye shahada halali Na. 630003322 iliyoandikishwa kupigiwa kwenye kituo cha Welezo Skuli, Chumba Na. 6 amekataliwa kwa madai kwamba jina lake halimo kwenye Orodha ya Wapiga Kura

II. KITUO CHA KINUNI


  • Kundi la Janjaweed likiongozwa na viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) limezunguka maeneo ya kituo kwa ajili ya kushinikiza kupiga kura

III. KITUO CHA VIWANDA VIDOGO VIDOGO


  • Gari Namba ZNZ 45948 inatumika kupakia vijana kutoka ofisi ya CCM Mkoa na ambao si wakaazi wa jimbo la Magogoni, iliyopo Amani, kupeleka kituo cha Viwanda Vidogo Vidogo kwa ajili ya kupiga kura

IV. KITUO CHA WELEZO HOSPITALI


  • Kijana mwenye kipande kilichoandikwa jina la Omar Hashim Mohammed, chenye namba ya usajili 620 001 358, amekutwa na shahada ya kupiga kura ambayo ni feki. Wenzake wenye shahada kama hiyo wameweza kupiga kura katika kituo hicho cha Welezo Hospitali.

Wapendwa Wanahabari,

Hii ni taarifa ya awali juu ya matukio yanayoendelea sasa na ambayo hadi sasa yameripotiwa kwenye ofisi yetu kwa ushahidi kamili. Tutawatumia taarifa nyengine kadiri zitakavyokuwa zinatufikia.

Pamoja na salamu za Chama,

Dawati la Habari na Mahusiano,
Civic United Front
(CUF – Chama cha Wananchi)
 
Waanzisha muafaka mwingine lakini uwe wa kajimbo hako tu. Allowance ziwe zile zile!
 
CUF Sasa ni wazi kuwa ni chama cha wapemba tu.

Kuna chaguzi kubwa mbili nchini hivi sasa lakini kwa CUF kelele zao zote ni za yale yanayotokea Magogoni tu, kwanini?

Kwa CUF kuendelea, kuna haja ya kubadili mikakati yao, kwani kama watabakia kuwa chama cha wapemba tu, sio muda mrefu kitajimaliza.
 
CUF Sasa ni wazi kuwa ni chama cha wapemba tu.

Kuna chaguzi kubwa mbili nchini hivi sasa lakini kwa CUF kelele zao zote ni za yale yanayotokea Magogoni tu, kwanini?

Kwa CUF kuendelea, kuna haja ya kubadili mikakati yao, kwani kama watabakia kuwa chama cha wapemba tu, sio muda mrefu kitajimaliza.

HUNA HOJA,ni bora kuwa msomaji wa hii thread...kwani lazima CUF walalamikie ya busanda?..busanda ni CCM na CHADEMA ndio vinara kule na zanzibar ni CUF na CCM......acha unazi usiokuwa na kichwa wala miguu
 
Chama Cha mafisadi bidii ya ufisadi imeelekezwa kwenye kufisadi kura na haki za wananchi baada ya kufisadi mabilioni yetu kupitia EPA

Shame on you chama cha mafisadi!
 
CUF Sasa ni wazi kuwa ni chama cha wapemba tu.

Kuna chaguzi kubwa mbili nchini hivi sasa lakini kwa CUF kelele zao zote ni za yale yanayotokea Magogoni tu, kwanini?

Kwa CUF kuendelea, kuna haja ya kubadili mikakati yao, kwani kama watabakia kuwa chama cha wapemba tu, sio muda mrefu kitajimaliza.
.
Hata Chadema hawajaongelea ya magogoni je nacho ni chama cha WATANGANYIKA TU???
 
Sasa hizi ndio huwa naita akili za mende -Cockroach..... mtu unalalamikia tatizo lile lile kila mwaka na huji na uvumbuzi. CUF mbona mnalalamika kila mwaka halafu hamtafuti ufumbuzi??
 
Sasa hizi ndio huwa naita akili za mende -Cockroach..... mtu unalalamikia tatizo lile lile kila mwaka na huji na uvumbuzi. CUF mbona mnalalamika kila mwaka halafu hamtafuti ufumbuzi??


Unaongea kama vile mtu mzima aliyepakwata (kama unaelewa nina maana gani ?)unataka kusema wananchi wa TANZANIA wao pigia kelele maisha na hali inavyofanywa kuwa ngumu na viongozi kwa kujilimbikizia mali ya nchi ni wao wakulaumia ?wakati serekali ndio yenye nguvu za dola inafanya mamuzi wayatakayo na wakati wautakao .
 
Unaongea kama vile mtu mzima aliyepakwata (kama unaelewa nina maana gani ?)unataka kusema wananchi wa TANZANIA wao pigia kelele maisha na hali inavyofanywa kuwa ngumu na viongozi kwa kujilimbikizia mali ya nchi ni wao wakulaumia ?wakati serekali ndio yenye nguvu za dola inafanya mamuzi wayatakayo na wakati wautakao .

Acha kutukana... CUF haitashinda kwa wewe kutukana. Swali liko palepale ... Kwa nini uingie kwenye uchaguzi ambao unajua utashindwa?
 
Sasa hizi ndio huwa naita akili za mende -Cockroach..... mtu unalalamikia tatizo lile lile kila mwaka na huji na uvumbuzi. CUF mbona mnalalamika kila mwaka halafu hamtafuti ufumbuzi??
hwataki kujifunza, labda wamegeuza siasa kama mchezo
 
Acha kutukana... CUF haitashinda kwa wewe kutukana. Swali liko palepale ... Kwa nini uingie kwenye uchaguzi ambao unajua utashindwa?

Nini maana ya uchanguzi?katika akili yako?uchaguzi unafanana na ligi za mpira sasa ukisema sitocheza mechi hii kwakuwa sitoshinda kwanini utauda timu( in a first place)?
 
Nini maana ya uchanguzi?katika akili yako?uchaguzi unafanana na ligi za mpira sasa ukisema sitocheza mechi hii kwakuwa sitoshinda kwanini utauda timu( in a first place)?

mkuu.. hapo sasa umenena... je kama una uhakika refarii hatakubali goli hata moja mtakalofunga... bado utapeleka timu uwanjani? au utatafuta ufumbuzi wa tatizo la refarii kwanza?
 
HUNA HOJA,ni bora kuwa msomaji wa hii thread...kwani lazima CUF walalamikie ya busanda?..busanda ni CCM na CHADEMA ndio vinara kule na zanzibar ni CUF na CCM......acha unazi usiokuwa na kichwa wala miguu

Kama Busanda ni Chadema na CCM, Cuf kwanini wamemsimamisha mgombea! Nia yao ni kuona ccm inashinda mbona Chadema kwakujua hawana nguvu Magogoni kama ilivyo Cuf Busanda; Chadema hawakusimamisha mgombea Magogoni! Cuf inalogwa na ruzuku ya CCm wanayopata kila mwezi na Sharrff Hamad kulipwa pension wameridhika, ndio maana wako radhi kuwa CCM B!
 
Both CUF na Chadema wapaswa kulaumiwa kwani hadi sasa hawajatupa ripoti za Busanda...Niliisema hii kule ktk Ripoti ya CCM ya Busanda

...CUF na Chadema wanachoshindwa kujua Adui yao Halisi wa Maendeleo ya Siasa ni Nani....CUF cannot rule the country if they maintain Only Isles, the same Chadema cannot rule the country if the maintain Mainland....if they know they cannot win all places they have to sit and foresee what they need to do....

Kwakuwa tumekubaliana kutokubaliana, kila chama kisurvive kivyake!!! watakapofika ktk Deadlock ndio watajua nini maana ya kukusanya nguvu pamoja.!!!...kwasasa acha kila mmoja apoteze resource chache walizonazo!!!

CCM ndio wananufaika na hii sintoelewana ya Upinzani. CCM knows wapi pa kuipiga CUF,na wanajua wapi pa Kuipiga Chadema...at the End normal citizen ndio watakao suffer....wataachishwa kazi...wataletwa wahindi na wachina kufanya kazi ambazo kijana wa std 7 ndio anastahili kufanya kazi...Wizi, Ujambazi, Uongo, Utapeli, Ukahaba na ELIMU duni ndio yatakuwa marafiki wa watanzania.
 
CUF Sasa ni wazi kuwa ni chama cha wapemba tu.

Kuna chaguzi kubwa mbili nchini hivi sasa lakini kwa CUF kelele zao zote ni za yale yanayotokea Magogoni tu, kwanini?

Kwa CUF kuendelea, kuna haja ya kubadili mikakati yao, kwani kama watabakia kuwa chama cha wapemba tu, sio muda mrefu kitajimaliza.
stop being fool.
tunazungumza habari za wapemba hapa?
Hapa tunaongelea demokarasia inavyochinjwa na dhulma wanayofanyiwa wananchi.
 
Sasa hizi ndio huwa naita akili za mende -Cockroach..... mtu unalalamikia tatizo lile lile kila mwaka na huji na uvumbuzi. CUF mbona mnalalamika kila mwaka halafu hamtafuti ufumbuzi??


Nakwambia ndugu yangu ni shida tu, utasikia watu wa upinzani ...oh tunaibiwa ..oh...CCM wanaleta mamluki...kila mwaka kila uchaguzi ni yale yale. Je, kwa nini msitafute ufumbuzi?? Walau hata kutengeneza manati ya kuwapiga mamluki!!
 
Wana JF tusilaum CUF kuweka nguvu Pemba na Ungunja. Ni vyema hata Chadema wakachanganua vyema maeneo gani waweke nguvu zaidi kwani hawataweza kushindana na CCM kutawanya limited resources zao all over this big country. Ndivyo ilivyo duniani kote: Belgium, USA, S.A. Kenya, Malawi, Zimbabwe, Zanzibar (CCM vs. CUF: Ungunja vs. Pemba). Tuachwe kupumbazwa na propaganda za CCM kuwa chama fulani siyo cha kitaifa. Bali ukweli ni kwamba matumizi mazuri ya resources ndogo uliyo nayo ndiyo jambo la msingi. Maoni yangu: CUF wa focus zaidi Zanzibar na coast line; Chadema waweke kipaumbele Dar, Kilimanjaro, Arusha, Manayara, Mara, Kagera na baadhi ya miji ambako wanaamni mitaji yao itapata resoanable return, Mwanza; UDP waelekeze nguvu zao Shinyanga na Mwanza.

Vinginevyo ni kuendelea kucheza muziki kwa tune ya mafisadi CCM!!!

Haya ni maoni yangu tu.
 
Back
Top Bottom