Negotiator
JF-Expert Member
- Aug 9, 2010
- 303
- 44
"Mwisho, Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikali iwaeleze Watanzania juu ya hatua, kama zipo, ilizozichukua kuzuia ukiukwaji huu wa Makubaliano ya Muungano, Sheria ya Muungano na Katiba. Na mwisho, Serikali itoe kauli mbele ya Bunge hili tukufu kama - kwa ukiukwaji huu wa Makubaliano ya Muungano, Sheria ya Muungano na Katiba ya Muungano – Bunge hili tukufu litakuwa ndani ya mamlaka yake kuchukua hatua za kumshtaki Rais kwa mujibu wa ibara ya 46A ya Katiba kwa kushindwa kuihifadhi, kuilinda na kuitetea Katiba ya Muungano kama kiapo cha kazi yake kinavyomtaka."
Hii ni nukuu ya aya ya tatu kutoka mwisho ya maoni ya kambi rasmi ya upinzani ofisi ya rais Muungano kama ilivyowasilishwa na Tindu Lissu leo bungeni.
Hii ni nukuu ya aya ya tatu kutoka mwisho ya maoni ya kambi rasmi ya upinzani ofisi ya rais Muungano kama ilivyowasilishwa na Tindu Lissu leo bungeni.