Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 20,690
- 20,450
Wakati kipindi cha maswali na majibu kikiendelea sasa hivi, Spika wa bunge Bw. SS alisitisha maswali kwa muda na kutoa kauli kwamba amekua akipokea malalamiko kupitia ujumbe kutoka kwa wabunge kwamba wanasumbuliwa na TAKUKURU huko majimboni. Bwana SS akauliza, "sasa mbunge wa sasa anatekeleza ahadi zake alizotoa 2005, anagawa vyerehani, halafu TAKUKURU wanamsumbua, tunaomba baada ya maswali na majibu mwanasheria mkuu atoe ufafanuzi", alisema SS huku wabunge wakishangilia kwa nguvu.
Katika tukio lingine, spika amemzuia Naibu waziri wa Fedha, Omary Yusuf Mzee kumuita yeye (SS) kuwa ni Naibu Spika badala ya Spika. "Naona hii ni mara ya pili unaniita naibu spika" alisema SS na kumfanya Yusuf Mzee kuomba msamaha huku wabunge wakifa mbavu.
Tukio lingine pia lilimhusu SS, pale alipomtaka waziri mmoja kukaa vizuri kwenye kiti, kwani waziri huyo alikuwa amekizungusha kabisa kiti chake kiasi cha kumpa mgongo spika na akawa anapiga stori na mtu wa nyuma yake huku bunge likiendelea na maswali na majibu. "Naona umezungusha kabisa kiti chako kiasi cha kunipa mgongo, ni vyema watu wote wakawa wananitaza spika. Tena umekalia kiti cha waziri wa maendeleo ya jamii" alisema SS na kusababisha kicheko kutoka kwa wabunge.
Katika tukio lingine, spika amemzuia Naibu waziri wa Fedha, Omary Yusuf Mzee kumuita yeye (SS) kuwa ni Naibu Spika badala ya Spika. "Naona hii ni mara ya pili unaniita naibu spika" alisema SS na kumfanya Yusuf Mzee kuomba msamaha huku wabunge wakifa mbavu.
Tukio lingine pia lilimhusu SS, pale alipomtaka waziri mmoja kukaa vizuri kwenye kiti, kwani waziri huyo alikuwa amekizungusha kabisa kiti chake kiasi cha kumpa mgongo spika na akawa anapiga stori na mtu wa nyuma yake huku bunge likiendelea na maswali na majibu. "Naona umezungusha kabisa kiti chako kiasi cha kunipa mgongo, ni vyema watu wote wakawa wananitaza spika. Tena umekalia kiti cha waziri wa maendeleo ya jamii" alisema SS na kusababisha kicheko kutoka kwa wabunge.