Jodoki Kalimilo
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 12,013
- 10,169
Nimekuwa nikifuatilia muda mrefu kuhusu hili jambo ambalo serikali imekuwa ikisisitiza kuhusu watumishi wa serikali kutojishughulisha na siasa hasa wanajeshi wetu na viongozi wakuu wa mawizara, lakini hivi majuzi ameteuliwa mnadhimu wa Jeshi ndugu Samwel Ndomba ambae alishashika post za ukuu wa wilaya na ukuu wa mkoa, though theoretically hizi nafasi zinaonekana kuwa ni za kiserikali kutokana na muundo wa serikali kuu lakini ukiziangalia kwa jicho la pili utagundua kwamba sifa ya kuteuliwa katika hizi nafasi lazima uwe mfuasi wa chama kilichopo madarakani. Hapa kitu nachotaka kufahamu kwa huyu jamaa kurudi tena jeshini huku tayari ameshika nafasi mbalimbali za kisiasa (ukuu wa wilaya na mkoa) inakuaje hapa maana mie huwa nadhani mtu akishaingia huku kwenye ukuu wa wilaya au mkoa huwa harudi tena unless kama atakuwa waziri etc ambazo lazima uwe mbunge kupitia chama cha siasa.