Kwa muda wa siku mbili sasa nimekua nikikutana na maji yanayokaribia kwisha muda wake ama muda wake wa kutumika kuwa umekwisha kabisa.Leo nimenunua maji ambayo muda wake wa kutumika uliisha tangu tarehe 11/10/2012, tena tumenuua KATONI MBILI toka kwa muuzaji wa jumla hapa MUSOMA. Halafu nawapigia TBS SIRARI wanasema hawawezi kushughulikia ishu hiyo hadi nipeleke risiti kwao halafu twende dukani kuthibitisha madai hayo, hivi huoni kwamba huo ni uchochezi na Mfanyabiashara huyo? Habari nimeshawapa lakini kufuatilia inakuwa ni kesi yangu tena.
Hivi TBS wanafanyaje kazi, mimi nadhani wanapopata taarifa ni jukumu lao sasa kupita MADUKANI na kukagua bidhaa ili kujua ubora wake na si kuniingiza mimi kuwa sehemu ya kesi. Naomba wakazi wa MUSOMA tuwe makini na maji haya toka Kampuni ya RWENZORI kwani ni hatari kwa afya zetu
Hivi TBS wanafanyaje kazi, mimi nadhani wanapopata taarifa ni jukumu lao sasa kupita MADUKANI na kukagua bidhaa ili kujua ubora wake na si kuniingiza mimi kuwa sehemu ya kesi. Naomba wakazi wa MUSOMA tuwe makini na maji haya toka Kampuni ya RWENZORI kwani ni hatari kwa afya zetu