Anyisile Obheli
JF-Expert Member
- Dec 13, 2009
- 3,398
- 319
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
.... kuisaidia kiMaendeleo na kujenga utu wa Mtanzania wenye heshima
dah mkuu umemaliza kabisa,Utu ni taasisi pana! Taasisi ambayo ndio uti wa mgongo wa maendeleo ya mtu na jamii yake.
Alikuwa JK Nyerere peke yake alikuwa anasubutu Kuusemea Utu na kuuweka kama kigezo cha ustawi wa Taifa!
Bila Utu, ambao ndiyo asili ya Mtu, maedeleo yote hayana maana yoyote! Yanakuwa ni maendeleo ya vitu! Ni utu kwanza...
Utu ni Uungu ndani mtu, hatuwezi kuusaliti... lazima utu kutangulia kila nyanja ya jamii bila hivyo hicho kinachoitwa ustawi na maendeleo haina maana.
Maendeleo ya Utu ndio yatawale maendeleo na ustawi wa jamii na taifa, na si maendeleo ya vitu bila kuujali na kuujenga na kuendeleza utu wake kwanza..
Utu unanyaushwa, kuharibiwa na kuangamizwa na UFISADI!
Utu unarutubishwa na haki, upendo, maadili ya uongozi, kuheshimiana na usawa wa pato la taifa, matumaini na upendo!
Ni hakika CCM na Kikwete wameutupilia mabali Utu ulioasili ya Mtu! Mengine yote yanafuatia hapo ni Mgawanyiko na Mtabaka kwa Taifa. Mgawanyiko na mtabaka hayo vinazaa Udini, ukabila, kuimarisha, ujinga, dhuluma, maradhi nk. Kisa Utu umewekwa kando, tumeisaliti asili yetu. Na kama utu haupo ...ina maana tuna kinyume cha utu...ambacho ni unyama ndani ya Mtu... Na usiombe kuishi ndani ya jamii au Taifa kama hilo!