Papa Mopao
JF-Expert Member
- Oct 7, 2009
- 4,105
- 2,499
Kuna siku nilipanda daladala toka Tegeta mpaka Ubungo na bahati mbaya sikupata bahati ya kupata siti,nikatafuta daladala ya kwenda mbagala nako nilisimama hadi Buguruni, asubuhi hiyo! Baada ya mishemishe pale Buguruni,nikachukua gari hadi Mbagala nilisimama,baadae nikachukua daladala kuelekea Mnazi mmoja nako nilisimama vilevile aloo miguu iliniuma vibaya mno yaani, baada ya mishemishe hapo mjini,nikachukua daladala ya Mwenge toka pale Mnazi mmoja nilisimama hadi Mwenge na nikaunganisha na za Tegeta kwa kusimama tena, hahhahaha! Balaa hakuna kitu kibaya kama kusimama kwenye daladala bila hata ya kupata siti njia nzima na nilipata siti tu toka pale Tegeta mpaka pale Tegeta Kibaoni kwa siku hiyo. Noomaaa!! Sitasahauu!!!