Kushikwa Ugoni: Ukimfumania mtu na mpenzi wako utamfanyia unyama huu?

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Inasikitisha, lakini ndiyo tena yametokea, baada ya kufumaniwa na mke wa mtu, jamaa katobolewa jicho na kukatwa masikio; tafadhali soma zaidi hapa chini:

Akatwa masikio, atobolewa macho baada ya kufumaniwa

2007-11-10 09:29:07
Na Nathan Mtega, PST, Songea


Joshua Ndunguru, 28, wengi wanamjua kama kijana mtanashati, aliyezaliwa akiwa hana kilema chochote.

Lakini sasa, kama Mungu atamnusuru na kifo na kutoka hospitalini salama, wengi watamsahau kwani atakuwa si yule Joshua wanayemjua.

Huyu wa sasa atakuwa na chongo huku akiwa hana masikio.

Hii imekuja baada ya kuadhibiwa kwa kukatwa masikio na kutobolewa jicho lake moja baada ya kufumaniwa akifanya ngono na mke wa ndugu yake.

Habari zinasema kwamba Ndunguru, mkazi wa kijiji cha Lakeshore, ufukweni mwa Ziwa Nyasa, wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma alikutwa kitandani na mke wa ndugu yake aitwaye Tele Mapanje.

Akisimulia tukio hilo, ndugu wa majeruhi huyo Bw. Andrew Ndunguru alisema mke wa Mapanje alishukiwa mapema kuwa na uhusiano usiofaa na shemejiye huyo.

Alidai kuwa mumewe alisikia madai hayo na kufuatilia nyendo za mkewe kwa muda mrefu na akafanikiwa kuwakamata Oktoba 7 mwaka huu, saa 7:30 usiku na ndipo akaamua kumwadhibu mgoni wake kwa hasira.

Aliongeza kuwa baada ya fumanizi hilo, mkewe alitoroka na kukimbia lakini mtuhumiwa alikamatwa na Mapanje pamoja na wapambe aliokuwa ameongozana nao na kumkata masikio na kisha kumtoboa jicho la kulia.

Baada ya tukio hilo, Andrew Ndunguru anasimulia kwamba majeruhi aliyekuwa akivuja damu kwa wingi alikimbizwa katika hospitali ya serikali ya Wilaya ya Mbinga na hali yake inaelezwa kuwa ni mbaya.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Bw. Falhum Mshana alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa polisi inawashikilia watu watatu ambao ni mume wa mwanamke huyo Mapanje, Barnaba Kagoma na Lika Boy ambao alisema watafikishwa mahakamani mara tu baada ya uchunguzi kukamilika.
Source link: IppMedia.

Hoja:
--Je, wewe ukimfumania mpenzi wako, mke,mume au hawala akifanya mapenzi na mtu, unaweza kufanya yaliyotendeka kama hapo juu?!

--Kama sivyo, ni hatua zipi utachukua?
--Je, kama wewe ni mfumaniwa, ni bora kuuawa au kuachiwa kilema kama hicho?

Naomba mawazo yenu WanaJF. Ahsante.


SteveD.
 
Mshkaji apo amefanya vema tena adhabu aliyompatia ni ndogo saaana!

..kama mkeo malaya,malaya tu!haisaidii kwa kujipatia kesi ya jinai!na kuwaacha watoto wenu na njaa au wakihemea kwa ndugu na majirani!

..steve,wewe mbona hujajibu hayo maswali kwanza!au chakula hukaribishwa mgeni kwanza,bila mwenyeji kuonja?

..la kufanya,
..1.kumuonya huyo mama aache tabia ya kutembea na shemejiye!
..2.asiposikia ni kumkamata ugoni na kumpa talaka!
..3.kumpa kilema kama hicho haisaidii kwasababu utafungwa!bora umvunje mguu ataenda wekwa ogo na itafaamika alipigwa kutokana na hasira za kufumania!
..4.huyo jamaa kijijini angepigwa faini ya ngombe kadhaa!baraza la wazee linakaa na kutoa uamuzi,ama sivyo ahame kijiji!
..5.kimsingi,kama mkeo anatoatoa ni kumuacha na kuomba mwenyezi mungu gonjwa lipitie mbali,kumtia mtu kilema haisaidii!
 
Hii kali wana JF
Kama ni mimi nitamuacha nitamdivorce that day ndio jambo kubwa kwanini nipate kesi ya bure kwani haisaidii kama umetendo kosa u cant denied it kosa limeshatendeka huwezi kumkomoa mtu then unaenda kuozea jela.
 
--Je, wewe ukimfumania mpenzimke,akifanya mapenzi na mtu, unaweza kufanya yaliyotendeka kama hapo juu?!

...inategemeana hali hiyo itakukumba kwenye mazingira gani. Imagine ushamtafuta mkeo siku nzima, njaa inakuuma, jasho linakutoka, majirani wanakuchungulia madirishani, na washkaji kijiweni wanakunyoshea vidole, wakati huo huo kina mama ntilie wa jirani wanajichekesha na vile vicheko vya ngebe... halafu shabaash... jamaa mmoja wapo anakufuata kukutonya "kawachungulie pale...!"

--Kama sivyo, ni hatua zipi utachukua?

...eeh Mw'Mungu ndiyo mjuaji, mnh apishilie mbali!!!

--Je, kama wewe ni mfumaniwa, ni bora kuuawa au kuachiwa kilema kama hicho?

...hakuna lenye unafuu mjomba, kufumaniwa ni kufumaniwa tu, ushajiharibia Cv! maana kuna wanaoweza kukuachia 'kilema' cha akili, wakiamua kukuvisha utungo kisha wakuingilie kinyume na maumbile, na picha wakazitoe kwenye 'UWAZI'!!!

Naomba mawazo yenu WanaJF. Ahsante.

SteveD.

...sidhani kama kuna mtu atayeweza kusema ukweli tendo atalolifanya akifikwa na 'kaadhia' hiyo, kwani huwezi jua 'wehu' wa mtu mpaka akumbane na mtihani kama huo.
 
Inasikitisha, lakini ndiyo tena yametokea, baada ya kufumaniwa na mke wa mtu, jamaa katobolewa jicho na kukatwa masikio; tafadhali soma zaidi hapa chini:

Source link: IppMedia.

Hoja:
--Je, wewe ukimfumania mpenzi wako, mke,mume au hawala akifanya mapenzi na mtu, unaweza kufanya yaliyotendeka kama hapo juu?!

--Kama sivyo, ni hatua zipi utachukua?

Whoa whoa...think I'd just get hit by a bus...Wow, this is hard one!!!!

To be honest, I'd probably just walk away from the scene as fast as I could. The idea is to run away to find a rage corner, and stay there until I'm ready to face the reality rationally.


--Je, kama wewe ni mfumaniwa, ni bora kuuawa au kuachiwa kilema kama hicho?

Wala sina uhakika ni adhabu gani nichukuliwe nikiwa kama mfumaniwa. Kwa uhakika, hakuna cha afadhali katika adhabu zote hizo mbili. Lakini kama nikibambwa na mwenye mali ambaye ataoneka ana ghadhabu ya mkizi, basi nitafanya kile nilichofundishwa na babu yangu kwamba 'ukimchokoza cobra, basi hakikisha una mwahi kutema mate'
 
Hoja:
--Je, wewe ukimfumania mpenzi wako, mke,mume au hawala akifanya mapenzi na mtu, unaweza kufanya yaliyotendeka kama hapo juu?!

--Kama sivyo, ni hatua zipi utachukua?
--Je, kama wewe ni mfumaniwa, ni bora kuuawa au kuachiwa kilema kama hicho?

Naomba mawazo yenu WanaJF. Ahsante.


SteveD.

Kwanza kabisa Kuicontrol Hasira nitakayokuwa nimeipata ili niweze kufanya sound judgement.

Maamuzi nitakayofanya ni pamoja na kuita ndugu zake ili waje either waone au waambiwe na mashuhuda ikiwa ni pamoja na mimi mwenyewe kama shuhuda.

Siku hiyohiyo aondoke either aende kwao au kwa huyo bwana aliyekuwa nae.Hili haliitaji mjadala na mtu yeyote awe padri, askofu au shekh.

Vitu ambavyo sitafanya

Kumpiga either mke/mme aliyekuwa nae sitofanya maana kama wote walikubaliana kwenda kufanya ngono so wote kama ni adhabu wote wanastahili. Na adhabu ni kwa mke wangu tu ambayo ni soma hapo juu

Adhabu kama waliotoa hao mabwana kwa huyo mwanaume, itamfanya huyo mheshimiwa kuwekwa ndani huku jamaa akipona ataendelea ku... mkewe wakati yeye yupo lupango

Sitakubali kumrudia huyo mwanamke maana hiyo ndio tabia yake.
 
..kama mkeo malaya,malaya tu!haisaidii kwa kujipatia kesi ya jinai!na kuwaacha watoto wenu na njaa au wakihemea kwa ndugu na majirani!

..steve,wewe mbona hujajibu hayo maswali kwanza!au chakula hukaribishwa mgeni kwanza,bila mwenyeji kuonja?
..la kufanya,
..1.kumuonya huyo mama aache tabia ya kutembea na shemejiye!
..2.asiposikia ni kumkamata ugoni na kumpa talaka!
..3.kumpa kilema kama hicho haisaidii kwasababu utafungwa!bora umvunje mguu ataenda wekwa ogo na itafaamika alipigwa kutokana na hasira za kufumania!
..4.huyo jamaa kijijini angepigwa faini ya ngombe kadhaa!baraza la wazee linakaa na kutoa uamuzi,ama sivyo ahame kijiji!
..5.kimsingi,kama mkeo anatoatoa ni kumuacha na kuomba mwenyezi mungu gonjwa lipitie mbali,kumtia mtu kilema haisaidii!

--- si unajua tena mimi nilivyokuwa bonge la mtu, 13stones at least, bouncers sawasawa... huyo kijana kama ningemkuta na mke wangu, ningempiga bonge la ki-luksi na kumtembeza mtaa mzima kwa kucha, kisha nikimaliza nampeleka kwa wakwe zangu ili kupata ushahidi wa yeye kumwoa mke wangu maana atakuwa ameshapata talaka automatically!!
--- kutokana na umbo langu kuwa kubwa, naogopa hata kusogelea watu wanaonichokoza, hivyo ningemfumania huyo kijana, najua tu lazima akili ingekuja kuwa niondoke kwenye hilo eneo maana naweza kuua kwa konde moja tu la shingo!!:)

SteveD.
 
..kama mkeo malaya,malaya tu!haisaidii kwa kujipatia kesi ya jinai!na kuwaacha watoto wenu na njaa au wakihemea kwa ndugu na majirani!

..steve,wewe mbona hujajibu hayo maswali kwanza!au chakula hukaribishwa mgeni kwanza,bila mwenyeji kuonja?

..la kufanya,
..1.kumuonya huyo mama aache tabia ya kutembea na shemejiye!
..2.asiposikia ni kumkamata ugoni na kumpa talaka!
..3.kumpa kilema kama hicho haisaidii kwasababu utafungwa!bora umvunje mguu ataenda wekwa ogo na itafaamika alipigwa kutokana na hasira za kufumania!
..4.huyo jamaa kijijini angepigwa faini ya ngombe kadhaa!baraza la wazee linakaa na kutoa uamuzi,ama sivyo ahame kijiji!
..5.kimsingi,kama mkeo anatoatoa ni kumuacha na kuomba mwenyezi mungu gonjwa lipitie mbali,kumtia mtu kilema haisaidii!

Hii kali wana JF
Kama ni mimi nitamuacha nitamdivorce that day ndio jambo kubwa kwanini nipate kesi ya bure kwani haisaidii kama umetendo kosa u cant denied it kosa limeshatendeka huwezi kumkomoa mtu then unaenda kuozea jela.


Hakika bora kuachana naye maana huyu Bwana kwa kitendo alichokifanya ni kama vile alikuwa anafanya booking ya magereza. Lakini hiyo pia inasababishwa na short temperedness a.k.a ku-provoke. Ila kwa kuwa alikuwa akijua tangu mwanzo hatua aliyochukua ni booking kabisa ya kukaa gerezani.
Nampa pole lakini ndiyo hivyo tena imeshatokea.
 
...inategemeana hali hiyo itakukumba kwenye mazingira gani. Imagine ushamtafuta mkeo siku nzima, njaa inakuuma, jasho linakutoka, majirani wanakuchungulia madirishani, na washkaji kijiweni wanakunyoshea vidole, wakati huo huo kina mama ntilie wa jirani wanajichekesha na vile vicheko vya ngebe... halafu shabaash... jamaa mmoja wapo anakufuata kukutonya "kawachungulie pale...!"



...eeh Mw'Mungu ndiyo mjuaji, mnh apishilie mbali!!!



...hakuna lenye unafuu mjomba, kufumaniwa ni kufumaniwa tu, ushajiharibia Cv! maana kuna wanaoweza kukuachia 'kilema' cha akili, wakiamua kukuvisha utungo kisha wakuingilie kinyume na maumbile, na picha wakazitoe kwenye 'UWAZI'!!!



...sidhani kama kuna mtu atayeweza kusema ukweli tendo atalolifanya akifikwa na 'kaadhia' hiyo, kwani huwezi jua 'wehu' wa mtu mpaka akumbane na mtihani kama huo.


Mchongoma na wengine,
Faida mojawapo ya kuwa Mwana JF ni pia kupata kujifunza mambo kadha wa kadha. Hili alilolileta Steve D unaweza kuona kama ni jambo la mzaha kwetu kuchangia, lakini ndiyo mambo ambayo yanaigusa jamii ya kawaida ya watanzania. Wengi hupendelea kuongelea uchumi ama siasa, lakini masuala ya mengine ya kijamii kama haya yana nafasi kubwa sana katika kuelimisha umma.
Kabla sijakwenda kutoa maoni au jibu langu juu ya swali au maswali yaliyoulizwa, kwanza ni vema sote tumuangalie binadamu ni nani.
Kwa tafsiri yangu, binadamu ni mnyama kama walivyo wanyama wengine isipokuwa yeye siyo hayawani (irrational). Binadamu ni rational animal.
Kwahiyo basi matendo yoye yafanywayo na wanyama kama vile kupigana, kuwa na wivu (kama jogoo) nk, hivyo vyote binadamu anavimiliki. Tofauti iliypo kati ya binadamu na wanyama wengine, ni namna gani anaweza kumiliki matendo ya yafanywayo na wanyama.
Binadamu amaepewa uwezo wa kujifunza, kuiga na kutawala mazingira yake. Kwa maana mbali ya vitu alivyotunukiwa kama usingizi, hasira, kulia, kucheka nk vilevile huweza kuwa daktari, mfamasia, mkulima, dereva nk.
Kwa kifupi, usisubiri hadi hapo upate matatizo ndiyo utake kujijua kwamba wewe ni nani, ni vema ujijue kuanzia sasa kwamba wewe ni binadamu (mnyama) na sifa zako kama binadamu unazifahamu. Hii itakurahisishia sana kuwa na mahusiano mazuri/kuridhisha na watu au viumbe vingine.
Nikirudi kwenye swali ni kwamba kama nimeoa au nimeolewa ni lazima nijue kwamba ninajihusisha au ninaihusisha nafsi yangu na binadamu mwingine ambaye ana sifa kama zangu.

Kwa upande wangu, linapotokea jambo lolote lile kwanza ni kujipa muda wa kutafakari kabla ya kuchukua hatua zaidi. Hii elimu kama unayo inakusaidia kumiliki hasira na zaidi hukuongezea uwezo wa kufikiri unapokuwa na tatizo. Kama huna elimu ya kujitambua basi wewe ni hayawani.

Suala la kuachana au kusuluhisha litategemea mazungumzo baina yenu. hata siku moja usijaribu kuchukua maamuzi juu ya mkeo au mume bila ya kuwa na mazungumzo ya kina juu ya mustakabali wenu. Wengi hasa wanaume, huwa na maamuzi ya papo kwa hapo juu ya mustakabali wa ndoa zao pasi na kuangalia au kuzungumza kwa kina juu ya matatizo yao. Wakati mwingine makosa ya mke huwa ni matokeo ya makosa ya mume.
 
wazee mimi nataka nishare na ninyi experience yangu. Wakati niko chuo nafanya Masters tulitokea tukapendana sana na binti Mmoja wa Kikenya. Kweli sikujua uhusiano ulianzaje bali tulijikuta tumependa sana. Uhusiano wetu ulikuwa mzuri yaani tulikuwa couple wazuri sana. Sasa ile imebaki miezi kama sita hivi tugraduate demu akawa ananiambia sasa vipi? unampango gani? nataka nipate mimba tukirudi Africa tuzae etc. Kweli nilimpenda sana huyo demu. Navyosema nilimpenda sio mchezo jamani achaneni na mapenzi kabisa. Tulifikia mahali demu akawa ndio tunakaa nae geto kama mke na mme. Sasa ilifika mahali demu akabadilika ghafla siku hiyo nimeenda kwake nikakuta picha za jamaa wa Kenya lakini yeye hakuwa shule. Wazee acheni ilikuwa soo ukisikia mtu anafanya kitu mbaya ni noma. Iliniuma sana na huyo ni demu tuu na wala sio mke. Nilishindwa kulala kama week tatu hivi sio mchezo. Wakuu naamini ikitoke kwa mkeo ambaye kweli unampenda inauma mnoooo!

Labda uwe humpendi ila sasa inahitaji uwe na roho ngumu na ujitahidi kujicontrol mwenyewe tuu otherwise ni very dangerous wakuu.
 
Mimi nitanyamaza,
Sitachukua hatua zozote- wala sitamuuliza mke wangu wala ndugu yangu chochote- nitahakikisha tu kuwa mwe wangu ameshuhudia na ndugu ameshuhudia kuwa nimewafumania.
 
kumpatia adhabu mgoni wako siyo dawa ila ni ufinyu kiona mbali kiakili, kwani siku zote majuto ni mjukuu huja kinyume. alisahau kwmaba dawa ya moto ni moto na wala siyo maji , alichotakiwa kufanya ni kwamba angetafuta mdogo wa mkewe moja mzuri sana kisha akamtia mimba hapo angekuwa amempa adhabu nzuri sana huyo mwanamke mwenye kilanga kuliko kumtia kilema nduguye na yy kusota lupango huku akiwaacha watoto na wazazi wake katika hali ya mateso
 
Kama ingekuwa zamani wakati ukimwi hakuna angeweza kupewa adhabu ndogo lakini kwa wakati kama huu, adhabu aliyopata ni ndogo sana.kwa hakika wakati huu ukigundua kuwa kuna mtu ana mahusiano na rafiki yako wa kike au mke wako no way ni kuachana na huyo mwanamke saa hiyo hiyo wakati wa kuonyana umepitwa hali halisi kwa sasa ni mbaya yaani kwa tanzania nina imani watu karibu wote walishagonga ila tu hawajaanza kuumwa. sasa nani anataka kulea ukimwi
 
Mimi ninamshangaa huyu mzalendo halisi ambaye anasubiri mpaka apate ushahidi,ila ninachotaka kumfahamisha ni kwamba, mpaka ilipofika mahali ukapata taarifa kuwa kuna jamaa anakula ina maana ilishachakazwa sasa huo ushahidi unaousubiri utakupeleka kaburini maana kazi yako itakuwa ni kubwia virus kila siku. take care
 
ila mimi kwa sasa simuamini mwanamke yeyote wa tanzania yaani wote wameoza kwanza hawajui kukata ule msemo wa zamani tuliokuwaga tunasema maharage ya mbeya kwa sasa hivi wenzetu wa nchi nyingine za afrika huwa wanaita dada zetu maharage ya Tanzania yaani hakuna mwanamke rahisi kufanya ngono zembe kama mwanamke wa tanzania hata angekuwa mke wa nani yaani ukiomba hakatai na hata angekuwa na elimu gani mimi sijui walilogwa na nani
 
Kama hamuamini na haswa nyie mnaowakatia wake zenu tiket ya emmiret eti wakafanye biashara jaribuni na nyie siku moja kusafiri muwafuatilie muone balaa linalofanyika kuanzia hapo hong kong kwa dotto muuza ugali hapo chung king mansion ghorofa ya saba block A yaani hapo wake za watu wanaliwa tigo kwa ugali tu na wakati mwingine siyo kwamba hawana pesa la, basi laana tu. Mkitoka hapo muwafuatilie hadi guang zhou hapo ndipo hitimisho la balaa lao maana wakikutana na wapop huwa wanapagawa sijui wanafikiri wanigeria wote ni akina kanu? hapo guang zhou utakuta wenyewe wakitamba eti sisi hatutembei na wabongo wachovu bwana wasiojua kuhonga, michongo yetu ni wapop bwanaa, akina babayaro kuna sehemu hapo guang zhou wenyewe wameipa jina la Rose Garden ukifika hapo kuanzia siku hiyo utamkataza mkeo kusafiri maana ni kama sodoma na gomora
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom