Siku hizi baadhi ya wanasiasa wanapotaka kujenga hoja fulani ili kuhalalisha vitendo vinavyofanywa na baadhi ya vyombo vya dola pale ambapo kuna malalamiko ya uvunjaji wa haki za binadamu, tunawasikia baadhi yao wakidai Mamlaka zote zimewekwa na Mungu tunapaswa kuzitii. Hii phrase inatumiwa vibaya! Ni kweli mamlaka zote za nchi zimewekwa na Mungu na kweli pia inatupasa kuzitii. Lakini tunasahau kwamba hatupaswi kutii mamlaka dhalimu kwa vile ni mamlaka. Ni kama kusema inabidi tuwatii wazazi kwa vile imeandikwa kwenye Biblia - Amri ya Nne ya Mungu. Lakini hatupaswi kuwatii wazazi kama wanatushawishi kutenda dhambi au kuvunja sheria halali za nchi kwa vile ni wazazi. Tunapaswa tu kuwatii wazazi katika mambo yote mema/mazuri. Na tuna uhuru na tunapaswa kutowatii katika mambo mabay yote. Hali kadhalika kwa mamlaka za nchi. Tunapaswa kuzitii mamalaka za nchi kwa vile zimewekwa na Mungu lakini hatupaswi (kama ilivyo kwa wazazi) kutii mamlaka zinazokosa haki au zinazovunja sheria za nchi. Kama mamlaka hizo zikishindwa kuwalinda wananchi wake na mali zao na badala yake kuwa chanzo cha vurugu na machafuko (uvunjaji wa haki za binadamu na kuwafanya wananchi kukosa haki au kunyanyasika kwa sababu hiyo) basi hatupaswi kuzitii mamlaka za aina hiyo. Hivyo, tusipende kupotosha umma, kuwa kutii mamlaka tunatii blindly, hapana! Ni katika mambo mema tu na si mabaya!