Kusema Kweli Ni Sehemu Ya Uadirifu

X-PASTER

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
11,610
1,810
JF ni moja ya forum inayosomwa na watu wengi sana wenye kupenda mambo ya mtandao, kiasi ya kwamba nimesikia kuwa kuna baadhi ya waandishi wa habari wameifanya ndio chanzo chao cha habari nyingi zinazo jiri kila kukicha.

Nikatarajia kuwa Moderators ama viranja wanao simamia forum hii kuwa ni watu wapenda haki, waadilifu, wanaojali na kuheshimu uhuru wa kutoa maoni, kufuata na kutangaza misimamo ya kisiasa, kiitikadi na kiimani.


Nilidhani JF inachukizwa na vitendo vya Watanzania kuendelea kuwa kwenye mateso ya kiuchumi waliokuwanayo na wanapenda mabadiliko.

Vile vile nilitegemea kuwa JF wanavumilia katika kuto kukubaliana kimawazo, bila ya kutumia matusi, kejeli na vitisho kwa wale wanao sigana kihoja.


Nilitegemea kuwa wanachama watalindwa na kuvumiliwa mawazo yao.

Lakini ile thamani ya kuwa jukwaa huru la watu kuongea kwa uwazi haionekani humu! Jinsi ilivyo wenye kumiliki JF wanaimba kijamaa lakini wanacheza kibebari, je kwa mwenendo huu, tutafika tunako elekea?

Kujiunga kwangu kwenye hii forum ya Jamii, nilitegemea kujifunza mambo mengi na kupata mafundisho mengi yaliyo bora na yanayostahiki kuigwa na kila mwana jamii apendae maendeleo ya nchi yake au yake binafsi.

Hebu tutafakari na kujiuliza, hivi utapungukiwa kitu gani, ukijali na kutetea utaifa wako bila kujali itikadi za kisiasa na kiimani? Sasa tena mbona tunazibana midomo na kushikana mashati ili tusisogee kule tunapotarajia kwenda? Hivi hapa JF kuna wenye haki na wasio na haki kwenye kuzungumzia mustakabali wa nchi yetu? Refa anakamata jezi ya mchezaji, ili asiende kufunga, na baadhi ya watazamaji badala ya kushangaa wanashangilia...!



Ningependa tukumbushane kuwa; nchi hii ni yetu sote! Amani na utulivu havipatikani kwa kuwadhulumu, kuwakandamiza na kuwanyamazisha wengine halafu kutoa sababu zisizo za msingi! Na wala havitapatikana kuwa kuwapachika watu wanaodai haki zao kuwa wachochezi, wanatumiwa na majina mengine ya ajabu ajabu.

Haya hayatasaidia kitu! Ifahamike wazi kuwa amani na utulivu havipatikani katika nchi ambayo Katiba inakiukwa kila kukicha. Lakini mbona tunazibwa midomo pale tunapoamua kuzumngumza kwa uwazi? Kwannii lakini JF inajidharirisha kwa mambo ambayo yapo wazi kabisa?

Moderators wa JF wenyewe wanaonekana kujidhalilisha wenyewe katika hili. Nahisi na inawezekana hisia zangu zikawa za kweli, sitaki kuamini kuwa JF inafadhiriwa na serikali, na haya marumbano yote yasiyo na tija ndiyo yenye kuruhusiwa humu ndani.

JF ipo hapa kwa ajili ya hao mafisadi au wamefadhiliwa na sasa wanachukua nafasi hizo kulipa fadhila badala ya kuleta maendeleo yanayokusudiwa kwa nchi nzima bila kujali itikadi zao.

Sitaki kupandikiza hisia kuwa ile article yangu isemayo “Vipi refa anapoamua kukwatua?” inatishia usalama wa JF au kitaifa au inaingiliana na serikali, chama au dini. Kiasi ya kwamba imekuwa ni jinai ama kosa kubwa na nyeti sana kuwepo na watu wakapata wasaa wa kuchambua yaliomo, wakaamua kuinyofoa kabisa na kuweka kifungoni bila kuifikisha mahamani na bila maelezo yoyote yale. Hata pale nilipohamua kuwasiliana na Moderators kwa private message ili kujuwa kulikoni, sijajibiwa mpaka hivi sasa.

Hii ina maanisha kuwa hawana la kusema wala kujitetea maana haya na soni zimewakamata kisawa sawa kiasi ya kukosa majibu mwafaka.

Kuna msemo mmoja unasema hivi...
"LAKINI mtu anapokichukia kitu, haina maana kuwa lazima kitu hicho kiwe kibaya au hakifai. Huenda ikawa kasoro ni ya yule anayekichukia na siyo kile kinachochukiwa. Mwenye homa huweza akayachukia maji ya kunywa, yaliyo matamu na baridi, siyo kwa sababu maji hayo ni mabaya; bali ni kwa kuwa kinywa cha mgonjwa huwa ni chapwa, hakihisi ladha ya chakula hata kikiwa kitamu vipi!"

Nasikitika kusema kuwa JF imefikia hapa kiasi ya kukosa ladha! Yaani ni mchuzi uliokosa chumvi.

Ni matumaini yangu kuwa wanachama wachache sana miongoni mwetu wataendelea kusema kweli na kuchambua kwa ufasaha kila linalo jiri ili tupate kusonga mbele katika harakati za kuutetea utaifa wetu, bila kujali itikadi za kisiasa na kidini.
Japokuwa wataendelea kushikwa mashati na kukatwa ngwara (kukatwa mtama) (!?) na marefarii uchwala, lakini wasikate tamaa... ipo siku refarii atajisahau na kujifunga bao menyewe.

Niliambiwa zamani kuwa... “kusema kweli ni sehemu ya uadirifu’’.



Ila uongozi wa JF uadilifu ni msamiati uliopitwa na wakati na hauna maana yoyote kwao...!


Nimepigwa ngwara...! Na nimenyanyuka tena na nitaendelea kusimama kidete, kila nitapo dondoka tena na tena...!
 
Nadhani Mods watakuja na majibu ili tujue ni kwanini hiyo mada yako iliondolewa kabisa. Lakini kama watakuwa kimya, ni kwamba wamekusudia na kuleta dharau. Ngoja tusubiri majibu yao kwa nini wameiondoa mada yako na kutunyima haki ya kuisoma na kuijadili.
 
Tungekuwa tunatumia majina ya kweli ni rahisi kutengeneza mambo ya uhakika haswa kwa kukutana kuongea hili na lile na kuchangia mawazo halafu ingekuwa forum hii ni ya jamii yani mwendeshaji hajaingia mkataba na kampuni yoyote au sio mali ya kampuni iliyokuwa na watu zaidi ya 4 hiyo ingekuwa rahisi kufanya maamuzi ya uhakika na maamuzi mengine muhimu kwa ajili ya ustawi wa jamii nzima
 
Tungekuwa tunatumia majina ya kweli ni rahisi kutengeneza mambo ya uhakika haswa kwa kukutana kuongea hili na lile na kuchangia mawazo halafu ingekuwa forum hii ni ya jamii yani mwendeshaji hajaingia mkataba na kampuni yoyote au sio mali ya kampuni iliyokuwa na watu zaidi ya 4 hiyo ingekuwa rahisi kufanya maamuzi ya uhakika na maamuzi mengine muhimu kwa ajili ya ustawi wa jamii nzima
Shy tafadhali tufafanulie hayo niliyo yanukuu hapo juu...!

Nimepata hamu ya kujua zaidi.
 
Hapa pana Ukiristo mkubwa,utaona sehemu ya injili kwa juu mkono wa kulia mwisho ,pana UCCM wa chini kwa chini ,pana Utanzania kwa maana Tanganyika hawaitaki ,wanang'ang'ania Utanzania japo vyama vyao vinasera ya serikali tatu na halafu kuna ulimbukeni kutumia mistari wasiyoitekeleza si wanasema ..Where We Dare to Talk Openly..vipi wanakwanyua topiki kirahisi , aidha kutakuwa na moderator fisadi na si vinginevyo ,Unajua ilipoondolewa ile JAMBO FORUMS na kupachikwa jina hili nikajua tayari pameshaingiliwa bado kushika mimba tu. Lakini sasa Mimba imeanza kuchomoza.
 
"Kujiunga kwangu kwenye hii forum ya Jamii, nilitegemea kujifunza mambo mengi na kupata mafundisho mengi yaliyo bora na yanayostahiki kuigwa na kila mwana jamii apendae maendeleo ya nchi yake au yake binafsi."

Unategemea kuwa baada ya hayo juu bado una Uadirifu?

Umesema ukweli? Unataka kusema kwamba hujajifunza mengi?

Hayo mengi uliyoyaandika hukujifunza humu?

Umejuaje hayo yanatokea humu JF?

Kwa kweli hakuna mtu anaweza kunena maoni yake halafu kila mtu akbali kuwa ni ya ukweli!

Ahsante
 
Unategemea kuwa baada ya hayo juu bado una Uadirifu?
Uadirifu ninao ndio maana nikawaandikia ili kujuwa hatima na mustakabari mzima wa article yangu, baada ya kukosa majibu kwa siku mbili kama si tatu ndipo nikaandika haya niliyo yaandika.


Unataka kusema kwamba hujajifunza mengi? Hayo mengi uliyoyaandika hukujifunza humu?
Nimejifunza mengi sana na kutambua kuwa ufisadi unapiga kasi kweli kweli.
JF imefikia hapa kiasi ya kukosa ladha!
Yaani ni mchuzi uliokosa chumvi.
Umejuaje hayo yanatokea humu JF?
Yamenikuta na Nimepigwa ngwara...!

Kwa kweli hakuna mtu anaweza kunena maoni yake halafu kila mtu akbali kuwa ni ya ukweli!
Ahsante
Kwa sababu ndani ya JF uadilifu ni msamiati uliopitwa na wakati na hauna maana yoyote kwao...!
 
Ingekuwa ni jambo la busara kuweka wazi tatizo lako kwa kutuma email. Anwani zipo huru.

Binafsi kwa kuwa najua UKWELI KUHUSU JF ninajua kabisa kuwa hisia zako sio sahihi kama zile hisia za kuwa JF ni ya Chadema.

Ninajua mengi kuhusu JF kiasi kuwa nikiandika nitajianika, ila kwa wote wanijuao ki ukweli mimi ni nani kwa jina halisi na wapo humu Watakubaliana na mimi kuwa ULIYOSEMA NI MAKOSA YA KIBINADAMU KAMA YAPO na pia kuwa MODS wengi sio wamiliki wa JF. Mods wengi ni kama wewe tu ila wao wameonyesha kukubali hiyo kazi na HAWALIPWI, WANAFANYA BURE.

Kwa wanijuao kikweli wataniunga mkono. Sina haja ya kuwataja!!
 
Uadirifu ninao ndio maana nikawaandikia ili kujuwa hatima na mustakabari mzima wa article yangu, baada ya kukosa majibu kwa siku mbili kama si tatu ndipo nikaandika haya niliyo yaandika.


Nimejifunza mengi sana na kutambua kuwa ufisadi unapiga kasi kweli kweli.
JF imefikia hapa kiasi ya kukosa ladha! Yaani ni mchuzi uliokosa chumvi.
Yamenikuta na Nimepigwa ngwara...!

Kwa sababu ndani ya JF uadilifu ni msamiati uliopitwa na wakati na hauna maana yoyote kwao...!

Sio kweli uliyoandika kaka!!!
 
X - paster,

Mimi naungana nawe kabisa kwenye hili. Ile mada yako haikuwa na uchochezi wa aina yoyote ile na ilikuwa within mambo yanayojadiliwa hapa kila siku. Suala la kuifuta na kutotoa maelezo yoyote ni beyond motto ya hii forum.

Mods please, wekeni hili swala sawa. JF watu wanajadiliana kwa kutofautiana kila siku na sidhani kama ile article ya x-paster ilivuka viwango vya forum.

Rudisheni article tumkome nyani giladi mchana kweupeeeeeeeeeee.
 
Ingekuwa ni jambo la busara kuweka wazi tatizo lako kwa kutuma email. Anwani zipo huru.

Binafsi kwa kuwa najua UKWELI KUHUSU JF ninajua kabisa kuwa hisia zako sio sahihi kama zile hisia za kuwa JF ni ya Chadema.

Ninajua mengi kuhusu JF kiasi kuwa nikiandika nitajianika, ila kwa wote wanijuao ki ukweli mimi ni nani kwa jina halisi na wapo humu Watakubaliana na mimi kuwa ULIYOSEMA NI MAKOSA YA KIBINADAMU KAMA YAPO na pia kuwa MODS wengi sio wamiliki wa JF. Mods wengi ni kama wewe tu ila wao wameonyesha kukubali hiyo kazi na HAWALIPWI, WANAFANYA BURE.

Kwa wanijuao kikweli wataniunga mkono. Sina haja ya kuwataja!!
Hizi sababu ulizo zitoa hazina mashiko, Kutolipwa na kufanya kazi bure, ndio kunawapelekea kufanya vitu kinyume na taratibu?

Mbona wenyewe hawajibu, wanasubiria kitu gani?
 
Sio kweli uliyoandika kaka!!!
Tuandikie hapa tusome basi hiyo kweli ili hiyo kweli ituweke huru...!
Unajiita FairPlayer... mbona basi hatuoni huo u-FairPlayer wako ukifanya kweli...!?

Andika basi yalio kweli hili tuyasome na tukuone kweli wewe ni Fair Palyer, usiye pendelea!
 
X - paster,

Mimi naungana nawe kabisa kwenye hili. Ile mada yako haikuwa na uchochezi wa aina yoyote ile na ilikuwa within mambo yanayojadiliwa hapa kila siku. Suala la kuifuta na kutotoa maelezo yoyote ni beyond motto ya hii forum.

Mods please, wekeni hili swala sawa. JF watu wanajadiliana kwa kutofautiana kila siku na sidhani kama ile article ya x-paster ilivuka viwango vya forum.

Rudisheni article tumkome nyani giladi mchana kweupeeeeeeeeeee.
Sina uhakika kama wanayo bado, ila kwa kumbukumbu zangu sidhani hata kama wanayo na hata kama wanayo sidhani kama watairejesha, maana wao watahesabu kama wameshindwa, ilihali hapa hatupo kwenye mashindano.

Wanajisahau kuwa tupo hapa kujadiliana ili kuweka mambo sawa ili kudumisha Utaifa wetu.
 
Tayari mdudu ameshaingia humu! Hakuna uhuru nyie subirini baada ya miezi mitano ijayo ndo mtagundua kuwa mtoto anazaliwa lini!
 

Uadirifu ninao ndio maana nikawaandikia ili kujuwa hatima na mustakabari mzima wa article yangu, baada ya kukosa majibu kwa siku mbili kama si tatu ndipo nikaandika haya niliyo yaandika.


Nimejifunza mengi sana na kutambua kuwa ufisadi unapiga kasi kweli kweli.
JF imefikia hapa kiasi ya kukosa ladha!
Yaani ni mchuzi uliokosa chumvi.
Yamenikuta na Nimepigwa ngwara...!

Kwa sababu ndani ya JF uadilifu ni msamiati uliopitwa na wakati na hauna maana yoyote.. kwao.!

X,
Kwao tena? Au petu?

"Ndani ya JF" una maana 'Wenye kuhodhi'
 
WanaJF nadhani tayari kuna tatizo la kutoaminiana. Kwasababu hatuonani sura wakati wa kutoa maoni na hatuelewi ni nani huyu kajibu, ni wa jinsia gani, dini gani, ana umri gani, chama gani, kweli ni mtanzania, kweli ni mzalendo (hata kama mtanzania), ni mfanyakazi wa Ikulu/bunge/usalama wa Taifa/Polisi/mfanyabiashara, yuko nchini au nje nk. nk. Hili limesababisha ukungu na pia giza kwenye mawazo ya wana JF. Hakika ipo haja ya kufikiri upya na kwa kina namna ya kuondoa hiki kiza "that is if we truly want JF to remain the home of great thinkers, where people dare to speak openly"
 
Back
Top Bottom