sio vizuri kuruka dozi au kukatisha kutumia dawa hasa kwa hizi dawa zinazotibu malaria,antibiotcs,antiprotozoals etc.unaposahau kutumia dawa hizo unasababisha wadudu ambao tayari wanakuwa wameshaanza kudhoofishwa na dawa wafufuke upya na mara nyingi hurudi kwa nguvu zaidi ya mwanzo na wengine huwa sugu.
Lkn kwa vile imeshatokea bahati mbaya basi wewe endelea na dawa kama kawaida ila uwe makini zaidi na usirudie kosa.at least wewe umeonyesha kujali wakati kuna wengine huwa wanakatisha dozi wakifikiri tayari wamepona.hao wako kwenye hatari kubwa ya kutotibika kirahisi hapo baadaye.
Tizo, pole na kuumwa.
Dozi ya dawa inapangwa baada ya utafiti wa kina kuangalia minimum concentration ya dawa kwenye mwili inayoweza kuendeleza mapambano na ugonjwa na maximum ambayo itapambana bila kuleta madhara makubwa zaidi kwa mwili. Kama umeruka dozi unashauriwa kutumia dawa mara unapokumbuka na kuangalia muda uliobaki kwa ajili ya dozi inayofuatia. Kama upo karibu sana ni bora kuruka. Otherwise,ni muhimu kuchukua namba ya simu ya daktari ili uweze kuwasiliana juu ya maswali ya papo kwa hapo.