CHASHA FARMING
JF-Expert Member
- Jun 4, 2011
- 7,789
- 8,912
KURITHISHA BIASHARA/FAMILIY BUSINESS
Famiily business imetapakaa sehemu nyingi sana dunianikuanzia Marekani, Ulaya, Asia na Africa, na kampuni nyingi sana kubwa dunani nyingi ni za familia zinamilikiwa na familia pamoja na kwamba zinakuwa na watuwengine nje ya familia
Hapa chini ni moja ya kampuni 250 duniani zinazo milikiwa nafamilia, ingawa zinashre holder wengine out of family
Company | Rank |
Wal-Mart Stores | 1 |
Ford Motor Co. | 2 |
Samsung | 3 |
LG Group | 4 |
Carrefour Group | 5 |
Fiat Group | 6 |
Ifi Istituto Finanziario Industriale S.p.A. | 7 |
PSA Peugeot Citroën S.A | 8 |
Cargill Inc. | 9 |
BMW (Bayerische Motoren Werke AG) | 10 |
Hyundai Motor | 11 |
Koch Industries | 12 |
Robert Bosch GmbH | 13 |
SCH (Banco Santander Central Hispano S.A.) | 14 |
ALDI Group | 15 |
Auchan Group | 16 |
Pinault-Printemps Redoute | 17 |
Ito-Yokado | 18 |
Tengelmann Group | 19 |
J Sainsbury | 20 |
Motorola | 21 |
Viacom | 22 |
Novartis Group | 23 |
Tyson Foods | 24 |
Bouygues | 25 |
Roche Group | 26 |
Bertelsmann | 27 |
Weyerhaeuser | 28 |
Loews | 29 |
News Corp. | 30 |
NIMEOROZESHA CHACHE KATI YA NYINGI SANA ZINAZO MILIKIWAKIFAMILIA HAPA DUNIANI
SASA BASI KWA NINI FAMILY BUSINESS NYINGI SANA KWA TANZANIAHUFA MARA TU, MMILIKI ANAPO UGUA, KUFARIKI AU KUZEKA?
1. UENDESHAJI WA BIASHARA KIUCHAWI/KWA KUTUMIAWAGANGA
Ni ukweli kabisa kwamba baadhi ya matajiriwa tanzania ukifuatilia historia za biashara zao na jinsi wanavyo ziendeshautagundua kwamba, zinaendeshwa kwa nguvu za giza, unakuta kuna mashariti kibao,likiwemo ra tajiri kutoa kafara, tajiri kutoruhusiwa kutumia vitu vya anasa nakazlika
Kwa staili hii biashara nyingisana za ainahii, hufa mara tu mmiliki wake anapo kuwa ametoweka duniani
2. KUKOSEKANA KWA MAANDALIZI
Wanyabiashara wengi huwa hawana utamaduniwa kuwaandaa watoto wao kwa ajiri ya kurithi biashara na matokeo yake ni waowenyewe kuendelea kuendesha biashara, kukosekana kwa maandalizi hupelekea kufakwa biashara za familia, na biashara hufa kwa sa babu mtu anaye chaguliwakurithi biashara au kusimamia anakuwa hana elimu wala uelewa kuhusu biashara zababa yake na matokeo yake ni kuongoza anavyo jua yeye na mwisho kufa kwabiashara yenyewe
Maandalizi kufanyika kwa haraka na kwa zima moto
3. UGONVI WA KIFAMILIA
Hii ni moja ya sababu kuu ya familybusiness nyingi sana kufa, Mara tu baada ya Baba/Mama anapo fariki, huanzaugonvi mkubwa sana wa kugawana mari za baba/mama, Na huu ugonvi ni matokeo yaKutokuwepo maandalizi mapema ya Nani ataongoza biashara za Fmailia,
4. UKUBWA WA FAMILIA
Ukubwa wa Familia nao ni sababu kuu yaBiashara nyingi za familia kufa, Mara baada ya Mwanzilishi kuchoka au kuugua,Watoto wa mmiliki na wake zake huanza michakato ya kugawana mari na kwa kuwafamilia ni kubwa sana hujikuta wana ua kampuni
5. FAMILIA/WATOTO/MKE/MME KUWA MBALI SANA NABIASHARA
Hili nalo ni Tatizo kubwa sana, Mara nyingiutakuta BABA/MAMA anapambana kivyake na wafanya kazi huku Watoto na Mama wakiwabise na mambo yao wenyewe,
6. WATOTO/MKE/MME KUTOKUWA NA HOBY NA BIASHARA
Utakuta baba ana biashara kubwa sana lakiniwatoto wana hoby na vitu vingine kabisa na hata sisi ni mashahidi, utakutababa ana kampuni kubwa ila watoto wake either wanasomea fani tofauti auwanafanya kazi za kuajiriwa, hushangai kukuta mtoto ni mwalimu huku baba yakeni mfanya biashara mkubwa sana.
7. BIASHARA NYINGI KUENDESHWA KIMAGENDO/ RUSHWA,UKWEPAJI WA KODI
Wafanya biashara wengi sana, ukifuatiliabishara zao utaambiwa wanakwepa kodi, au wanafanya biashara za magendo auwahonga sana watendaji wa serikali ili kufanisha biashara zao, kwa staili hii,ni razima biashara ife kwa sababu watoto wanakuwa hawana huo uwezo wa kufanyabiashara za hivyo au hwapendi kufanya biashara za namna hiyo hivyo kupelekeabiashara kufa
Je, ni zipi njia sahihi au njia nzuri zakurithisha biashara?
1. ANZA KUANDAA FAMILIA YAKO MAPEMA
Anza kwa kustracture familia yako katika mkao wa kuindaa kuja kurithibiashara zako mara tu utakapo kuwa huna nguvu, umefariki na kazalika, hii ninzuri ili kuwepo na muda wa kutosha wa familia ku-adress personal conflict zitakazojitokeza au zilizopo,
Unaweza hata kutumia watu wan je kuishawishi familia au kuipa elimufamilia yako
Familia ni lazima waafikiane na mrithi wa kuongoza biashara yao, haihitaji siri yoyote hapa
2. ANZA KUMUANDAA MURITHI KISAIKOLOJIA
Warithi wa biashara huandaliwa mapema sana na sio ishu ya zima moto, namara nyingi kwa watanzania warithi wa biashara hupatikana kupitia kikao chafamilia mara tu baada ya msiba, na hapa ujuzi huwa hauzingatiwi
Mpe mazoezi kwa vitendo, ikiwa ni pamoja na kumwachia afanye baadhi yashughuli
MRITHI ANATAKIWA AANDALIWE
- KIELIMU- apewe elimu inayo husika na biashara zaBaba, na Mtoto asiruhusiwe kusoma POLITICAL SCIENCE wakati anatakiwa kurithiBiashara
- KISAIKOLOJIA- Ni lazima aadaliwe kisaikolojiaili ajue jinsi ya kuhendo hiyo kazi,
Hapa hakikisha hufanyi KOSA wakati wa kuchagua na Hii huchua si CHINI YAMIAKA 15 KUMUANDAA
3. ANZA KUANDAA DOKOMENTI ZA KURISISHA MAPEMA
Ni vizuri dokoment za kurisisha zikaanza kuandaliwa mapema sana ikiwemonkuwatumia wanasheria kuziandaa na kuanza kubadili majina ya umiliki wabiashara kutoka wewe kwenda kwa uliye muandaa au familia yako
Tumia wanasheria kufanya hii kazi
4. PANGA KABISA NA LINI UTAMUACHIA MRITHI MAJUKUMU
Hapa watu huzani ni Mpaka Mmilikia Afe/augue/azeeke ndo arisishe, Nounatakiwa kabisa kupanda Tarehe na wakati wa kukabidhi majukumu na wewekupumzika Nyumbani na kula matunda ya kazi yako
5. MTAMBULISHE MRITHI WAKO KWA MARAFIKI WAKO WABIASHARA/WAFANYAKAZI
Ni vizuri marafiki wako wa biashara wakajua mrithi wako mapema
NB: Kwa Tanzania wafanyabiashara wenye asiri ya asia au wahindi ni moja kati ya watu wenye mafanikio kwenye familiy business kurisisha, ndo maana ni vigumu kukuta mtoto wa kihindi akitafuta kazi, wengi wao wanasoma kusaidia biashara za baba zao, na wengi wao wanasoma kozi ambazo zinaendana na biashara za wazazi wao
Ndo maana huwezi kuta watato wakihindi vyuoni wakiwa wanasoma education au socilogy na lazalika