Elections 2010 Kura zetu kwa Slaa

Jibaba Bonge

JF-Expert Member
May 6, 2008
1,246
401
Tumempata mwanana, mpambanaji hodari
Mzalendo pia mwana , mafisadi kukabiri
Utani kwake hakuna, kweli yeye dakitari
Siku ile ikifika, Kura zetu kwa Slaa

Tumpe kura kwa wingi, uchumi kuukomboa
Tumpeni nyingi kingi, nchi kuisimamia,
Avuke vyote vigingi, mtandao kuubomoa
Siku ile ikifika, Kura zetu kwa Slaa

Siku ile ikifika , kura tumpe Slaa
Yeye ndiye msifika , mafisadi kwao balaa
Wezi watetemeka, walisikiapo ‘Slaa'
Siku ile ikifika, Kura zetu kwa Slaa

Anahaha makamba , kama anakata kamba
Mafuriko yamkumba, anenayo yote pumba
Chama chake kinayumba, sasa kutumia ndumba
Siku ile ikifika, Kura zetu kwa Slaa

Pipozi pawa ni sasa, kona zote yasikika
Ukombozi ndiyo sasa, ccm kuizika
Nchi yetu kutakasa, wakati ndo umefika
Siku ile ikifika, Kura zetu kwa Slaa
 
Hii Imetulia Jibaba. Nashauri wale wenye kuweza wazidi kuusambaza huu ushauri ni ujumbe mkubwa kwa watz wapenda mabadiliko.
 
si tumtafute andanenga (RTD) akaimbe kabla ya mikutano ya slaaaa
 
Back
Top Bottom