Elections 2010 Kura za maoni-jamiiforums

Karibu, ni bora ungejitambulisha, ndo mmeamua vibaraka wa mafisadi kuingia na id nyingine ili mumuongezee fisadi mwenzenu kura? Jaribu ila mtaugua vidonda vya tumbo!
Yaani hadi imekuwa kero......wanavamia tu hata kujitambulisha hawataki, wanavamia tu topiki na kuziharibu sijui wametumwa?
 
Yaani hadi imekuwa kero......wanavamia tu hata kujitambulisha hawataki, wanavamia tu topiki na kuziharibu sijui wametumwa?
Wametumwa na wanalipwa kwa hilo. Mafisadi wanahela bwana! Usipime
 
Samahani kidogo,hivi zile online opinion polls results zilizotoka katika RaiaMwema tarehe 22 September si zilitoka huku Jamii Forums?Mmeshadili uongo wake kabla administrator hajabadili utaratibu na kusema member peke yake ndiyo wapiga kura?Nacccccccccccheeeeeka.Limewafika.Mlikimbilia kutoa za mtandaoni,mngejua mngeibakiza kama last nail.

utacheka sana, bisha hodi japo ufunguliwe mlango sio unaanza na spidi ya kuchooonga, nyie mnaokuja kwa spidi mwisho wenu oct 31 hatutawasikia tena
 
Ni wazo zuri saaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaana maoni ya jamii forum kutolewa that is the fact -tunawaomba viongozi wa JF wazitoe publically -this is even more realistic compare to Redet and Snov -maji taka. Uongozi wa Jamii tunaomba mtutendee haki weka mambo hadharani-mbele ya waandishi wa habari.
 
Keep your statistics with you! everything will be revealed on 31st October! Mambo yatakuwa shega chama makini chenye wagombea makini kwenye urais, wabunge na madiwani kitaibuka kidedea.
 
Naunga mkono. Ikitolewa rasmi na waendeshaji wake basi huo utakuwa ni msimamo kamili na utaweza kuchangia katika kurekebisha hali ya hewa chafu ilivyosababishwa na tafiti bandia za Synovate na REDET. Inatakiwa itolewe katika mkutano wa waandishi wa habari mkubwa uliondaliwa vizuri.

Kwa kiwewe cha kikwete na timu yake ya kampeni, watavizuia vyombo vya habari vinavyomilikiwa na wanaojipendekeza kwa serikali visichapishe au kutangaza matokeo haya . hata kama watayatangaza watatangaza kebehi kwa jamii forum maana sisiem kwa matamshi ya maji taka hakuna anayewashinda hapa duniani!!
 
Kwa kiwewe cha kikwete na timu yake ya kampeni, watavizuia vyombo vya habari vinavyomilikiwa na wanaojipendekeza kwa serikali visichapishe au kutangaza matokeo haya . hata kama watayatangaza watatangaza kebehi kwa jamii forum maana sisiem kwa matamshi ya maji taka hakuna anayewashinda hapa duniani!!

Hili ni la kikatiba halihusiani na CCM. Soma elimu ya uraia please.
 
Hii naiunga mkono kwa nguvu zangu zote, ila napendekeza isubili a few days before 31st October.
 
Wana Jamii wote na wapenda maendeleo nina wazo moja.Naomba uongozi wa juu wa Jamii forums utoe publically utafit na kura za maoni kama walivyofanya REDET na Synovate.Nadhani hamna kikwazo chochote kukutana na waandishi wa habari na kuyatangaza ili kutoa picha kama uchaguzi ungefanyika leo nani angekua Rais.Nakaribisha maoni kutoka kwa wengine pia.

JF ina waandishi tu (wataalam), na ili kufanya tafiti kubwa kama hizo unahitajiwa uwe na wataalamu wa Takwimu. Hapo ndio tatizo!!
 
Najua mnajua na msiojua mjue, na wengi watazidi kujua na hata CCM WANAJUA Kuwa CHADEMA IKO JUU. Habari ndio hiyo.
 
Najua mnajua na msiojua mjue, na wengi watazidi kujua na hata CCM WANAJUA Kuwa CHADEMA IKO JUU. Habari ndio hiyo.

I agree with you, kuna wakati media iliipandisha chat CCJ huwezi amini only Tendwa alivyoenda on ground akukta madudu... sasa na wewe subiri October 31st!
 
Watasema JF haiko reguistered kufanya kazi za Utafiti kwa hiyo matokeo yake ni ya uongo.
Hapana, hakuna kitu kama hicho. Hata REDET haijasajiliwa mahali popote. It is just a programme of Dep. of PS and PA, of UDSM period.
 
jf inasomwa na watu wengi sana wasomi na wenye uelewa na ambao sio lazima uwaambie kuwa uchumi umekuwa ila wao wanaona kwani wanajua walipotoka na walipo na wanakoelekea...........sio lazima kumweleza mwana jf kuwa umewashughulikia mafisadi kwani atasema mbona kikwete amesema ni watu safi wakati yeye mwenyewe alisaini washitakiwew?...............utafiti wa hapa waweza kuwa makini na huru zaidi kuliko utafiti mwingine wowote because hatujanunu liwa km hao redet na synovate
 
Tena naona itakuwa more realistic kuliko ya REDET ukizingatia watu ni atleast 8000 na watu ni tofauti tofauti sio makada wa chama tuu kama akina MS.
Naona ni suala la kuamua tuu

But the same member can log in with as many user name as s/he want na kufanya uchaguzi wake! Is like kumchagua mshindi wa BSS kwa SMS ambapo mtu naweza kutuma as many messages as s/he can afford! Hivyo basi, only one person can change the direction! Therefore, kama kuna utafiti ambao sio realitsic basi ni huu wa JF ambao pamoja na mapungufu hayo niliyoainisha hapo juu bado hata wale wasio na sifa za kupiga kura, bado wanaweza kutoa maoni yao kuhusu nani anayefaa kuwa rais achlia mbali kwamba na mamia ya wa-TZ walio abroad ambao hawatashiriki kwenye general election nao wanaweza kupiga kura zao humu!!! Therefore, maoni ya JF nayo ni unrealistic!
 
I agree with you, kuna wakati media iliipandisha chat CCJ huwezi amini only Tendwa alivyoenda on ground akukta madudu... sasa na wewe subiri October 31st!
Nani asiyejua Tendwa ni another arm of this government? Na nani asiyejua kuwa CCJ pia ilikuwa na connection ya system ya nchi hii? bahati mbaya tu malengo yao yalipigwa chini na watanzania wakatafuta namna ya kuiondoa?
 
Jf imekuwa siku zote kisima cha media za nchi hii kupata habari na kuanza kuifuatilia. Basi kwa sababu hiyo achieni magazeti yafanye kazi zao. Ingewezekana kama JF ingekuwa na gazeti lake yenyewe.
Heko Raia mwema kwa kuthubutu.
 
Back
Top Bottom