Wakuu, mi nilikua nawaza sana kuhusu wagombea ubunge kupita bila kupingwa. Sasa je wakienda bungeni wanawawakilisha CCM au wananchI wote wa majibo husika. Kwa nini tume ya uchaguzi isifikirie nje ya box, ili katika majimboi ambayo wabunge wamepita bila kupingwa wananchi wawapigie kura ya ndio au hapana. Atakayepata chini ya 50% (ndio) huyo awe hafai kuwakilisha jimbo. Swala la kuacha baadhi ya wabunge wapite bila kupingwa sii democrasia hata kidogo. Huenda umetumika mchezo wa umasikini wa watu au ubabe kama ilivyokua Nyamagana ili kupita bila jasho. Tume kama mko makini bado mna nafasi ya kuweka hayo marekebisho.