Kwa Mujibu hali ya mambo inavyoendelea upande wa Zanzibar, sina shaka ila kuwataka viongozi wa serikali iliopo madarakani kuzingatia uwezekano wa kura ya maoni kabla mchakato wa katiba kuendelea. Kwa kuwa nchi hii ni ya kidemokrasia, wakuu wafanye bidii ya kuhakikisha demokrasia inadumu. Wazanziabri walio wengi nchini mwao wanaona, kutinga katiba mpya bila ya kwanza kuwataka ushauri wananchi juu ya mustakbali wa taifa lao sio sawa bali ni kuwanyanyasa kifikra na mawazo. Liliopo sasa hivi kuitishwe kura ya maoni na kuamua kama tunataka muungano au laa. Kama muungano umepita basi tuendelee na mchakato wa katiba na kama haukupita, tuangalie njia nyingine ya mashirikiano kwa mustakabali wa raia wa nchi zote mbili. venginevo ni kujaribu kuhalalisha jambo ambalo ni haramu.