Kupita bila kupingwa - is this democracy too?

Hivi karibuni nimesikia kuwa baadhi ya wabunge wa CCM waliopita bila kupingwa walitumia mbinu ya kuwanunua wagombea wa upinzani ili wajiengue katika hatua ya mwisho kwa lengo la wao kubakia kama wabunge waliopita bila kupingwa. Vile vile nimesikia kuwa hata baadhi ya wabunge wengine walioshindwa ubunge walikuwa awali wameshinda, lakini wakarubuniwa wakauza ushindi wao kwa wabunge wa CCM. Nachelea kutoa mifano nisije nikawapa baadhi ya watu ugonjwa wa mshtuko wa moyo.

Kama hili ni kweli, basi Tz, tumeingia mahali pa hatari kubwa. Kuuza demokrasia au kujaribu kuinunua ni kosa kuu kuliko uhaini kwa mtazamo wangu.

WanaJF, naomba niambieni, kwanza hili ninyi mmelisikia? Ni kweli? Kama ni kweli, mnadhani nini kifanyike kuzuia hali hii? Kumbukeni kama ni kweli, basi nafasi za uongozi katika chaguzi zijazo, na hata Uspika wa bunge zitanunuliwa na hawa mafisadi ambao kwao mamilioni ni vijisenti tu.
 
hizo habari ni za kweli kabisa mfano jimbo la ismani mheshimiwa lukuvi alimhonga kapwani pesa na gari ili asimpinge
 
hizo habari ni za kweli kabisa mfano jimbo la ismani mheshimiwa lukuvi alimhonga kapwani pesa na gari ili asimpinge
Du..huyo mgombea bado yuko mtaani?...Lakini hii kweli iko verified?, maana kama ni kupewa gari, huyo jamaa ataanza kulitumia angalau miezi mi2 baadaye ili ionekana kalitafuta mwenyewe!
 
Huo ni ubakaji wa demokrasia. Mi nadhani ikithibitika mwanasiasa amefanya kitendo hicho, chama kimshughulikie ikiwa ni pamoja na kumfungulia mashitaka ya jinai.
 
Huo ni ukweli kabisa kwani hata mgombea wa chadema jimbo la mbeya vijijini ameuza ushindi kwa ccm
 
Wana JF kwa ufahamu wangu katiba inazungumzia wabunge wa aina nne ambao wataapishwa kufuatia uchaguzi uliomalizika wa 31.11.2010:

a: Wa kuchaguliwa kwa kura za wananchi kwenye majimbo.
b: Viti Maalum kwa mujibu wa katiba.
c:Viti 10 wa kuteuliwa na Rais
d: Mwnasheria Mkuu kwa wadhifa wake anaingia kwa mujibu wa katiba ya Tanzania.

Sasa kundi hili la wabunge lukuki ambao walijipitisha kwa hila za namna mbalimbali na kujipachika sifa ya kupita bila kupingwa wataapishwa kwa mamlaka ipi?
 
mbona wengine tulishachukua msimamo... hakuna kitu kama "wabunge waliopita bila kupingwa" - wangepingwaje kama hawakuwa kwenye karatasi za kura?
 
waliopitishwa bila kuchaguliwa!

Zamani wakati wa chama kimoja kulikuwa na chaguzi nyingi tu ila kwa mtu aliyesimama mmoja ilikuwa kuna kura za NDIYO na HAPANA. Na ilikuwa kama hapana ni nyingi basi mtu kashindwa wananchi hawamkubali. Ili kukuza demokrasia inatakiwa mfumo huu uwepo ambao unawapa haki wananchi wa kumchagua wamtakaye hata kama akiwa mmoja. Mfani mzuri tumeuona NYAMAGANA watu walikuwa hawamtaki Masha laiti asingepata mpinzani ingekuwa ngumu kwake ku-mobilize wananchi kwa kuwa hawamtaki. Mambo kama haya yanarudisha nyuma maendeleo, uongozi si kukalia kiti tu bali hata kuwaunganisha wananchi katika kujiletea maenedeleo pia ni jambo muhimu sana.
 
Jambo hili ni serious sio la kufanyia mchezo; inaanza kidogo kidogo kutozingatia katiba hatimaye jamii itaikuwa inaishi kwa ile sheria ya law of the jungle. Wenye jibu watwambie kabla hawa watu hawajaapishwa; au kama ndiyo tayari na hapa kuna kuchakachua katiba. Wanaharakati mko wapi?????
 
Ndg Zangu Nadhani Mnakumbuka vyema siasa chafu na zenye hila zilivyokuwa zikiendeshwa kabla, siku ya uchaguzi na baada ya uchaguzi haswa na wagombea wa CCM.

Sote tutakuwa bado tunakumbuka vyema kisa cha Lawrence Masha Jimbo la Nyamagana pale alipotangazwa kwamba kapita bila kupingwa, na nini kilichotokea baada ya matokeo yale kutenguliwa.

Mimi sikubaliani na hili suala na hivo naomba sheria nyingine iundwe kubadili huu mfumo.

nawakilisha
 
Ndg Zangu Nadhani Mnakumbuka vyema siasa chafu na zenye hila zilivyokuwa zikiendeshwa kabla, siku ya uchaguzi na baada ya uchaguzi haswa na wagombea wa CCM.

Sote tutakuwa bado tunakumbuka vyema kisa cha Lawrence Masha Jimbo la Nyamagana pale alipotangazwa kwamba kapita bila kupingwa, na nini kilichotokea baada ya matokeo yale kutenguliwa.

Mimi sikubaliani na hili suala na hivo naomba sheria nyingine iundwe kubadili huu mfumo.

nawakilisha

ngoja kwanza tuvuke mtihani wa kumpata Spika tuone kama kuna uwezekano wa kutungwa hiyo sheria unayoitaka.

maana haka ka-mama kakipita, basi ujue wazo lako halina nafasi.
 
MwanaJF niko pamoja nawewe. Kwani sheria unayoisema ni ipi na inasemaje? Nijuavyo mimi ni kwamba Katiba ya JYT haitaji wabunge hawa. Lakini sheria za nchi hii zinamruhusu mwnanchi mpiga kura kufungua kesi mahakamani kwa jibu la hakika!!!!!!!!!! Hebu tuelimishe wa kwetu!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mimi sina tatizo kubwa na dhana ya mbunge kupita bila kuwa na mpinzani. Mimi naona miongoni mwa hoja za msingi hapa kuwa hizi hapa:-
1) mbinu chafu walizotumia kubaki wagombea pekee- wengi wa waliotajwa tunajua njia chaf u walizotumia
2) si jambo geni katika nchi yetu kwa mgombea mmoja kupigiwa kura ya NDIYO/HAPANA ili wapiga kura kataka jimbo husika wawe wamepewa nafasi ya kumkubali/kumkataa mgombea husika. Kitu gani kilizuia hawa kupigiwa kura za NDIYO/HAPANA au JINAauPICHA/KIVULI??????????
3) Katiba ya sasa haitaji hawa kuwa wabunge halali. Ni kwa mamlaka ipi basi wamehalalishwa kuwa wabunge?
4) Kitendo cho chote nje ya katiba ni uvunjaji makusudi wa sheria, jambo ambalo likiendekezwa ni mwanzo wa kujenga jamii inayoishi kwa sheria ya jungle law-very dangerious!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
5) Pamoja na concern za watanzania wengi zilizotolewa mapema sana-Mwanakijiji (JF) akiwa mmojawapo-Tume ya Uchaguzi imeshikilia kuziba masikio na kuendelea kibabe!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
6)Wahusika wote ni kutokana na preferential voters za vyama- siyo voters choice katika jimbo husika. It is undemocratic kwa wabunge hawa kujiita ni wawakilishi halali wa wapiga kura wa vyama vingine katika jimbo.
 
Back
Top Bottom