Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
- Thread starter
- #61
Kwaminchi,
Mkuu kwanza kumbuka kuwa hapa tunahoji sheria zetu iwe for or against.. ni mawazo ya kila mtu kutokana na utaratibu uliopo au utakao kuja. Kwa hiyo sheria tunaiweka nje kwanza na kutazama kile kinachotokea/kitatokea kwa kujenga hoja zetu..
Hata hivyo naomba kifungu hicho cha sheria (Katiba) kinachosema hivyo..
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67
ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya
kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki
katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya
Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa
nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi
waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia
utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
_________________________________________________________________
21
(2) Kila raia anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu
katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomhusu yeye, maisha
yake au yanayolihusu Taifa.
Mzee Mkandara Ibara hiyo ndiyo kiini cha kesi ya Mtikila. Ndiyo maana mabadiliko ya baadaye ya sheria yalipoongezwa Mahakama iliyapiga chini mara zote. Tafadhali soma hukumu ya kina Jaji Manento ambayo imepangua hoja hizi kwa kina kwanini sheria ya mabadiliko ya Katiba ya 1994 ilikuwa ni kinyume na Katiiba.
Katiba haiwezi kutambua haki fulani halafu kuifuta ndani ya Katiba hiyo hiyo.