Kupima uwezo wa Rais Jakaya Kikwete??

Kikwete ni tumaini lililopotea. Wasaidizi wake ni ushahidi tosha na kigezo kizuri cha kupimia uwezo wake kwani udhaifu unapogeuka na kuwa sifa kuu ya kiongozi, ujue utawala wake uko rehani. Kiongozi dhaifu hukwepa majukumu na si ajabu wanafiki wakamsifia huku wakitoa lawama lukuki kwa wapambe - hapana tatizo ni Kiongozi mwenyewe, period.
Labda ni style yake..wengine wanaiita tolerance wewe unasemaje?, wanafiki wanaomsifia ni kina nani? wakati tunaongelea vitu vinavyonekana kwa macho yenu kila siku...kila mahali unaweza kuficha barabara? unaweza kuficha watuhumiwa wanaohaha mahakamani na kesi?..
 
Rais anasifiwa matokeo yakionekana, hauwezi kulazimisha sifa zisipostahili.
- Rais amefanya ziara bandarini, kuna uozo wa hali ya juu pale, akaishia zake. hamna maagizo wala nini. Watu bado wanapitisha mizigo Mombasa kusiko na rushwa.Sasa alienda bandarini kufanya nini?
- Alifanya ziara Magereza, hamna mabadiliko yoyote.
- Alifanya ziara moja USA akapata msaada wa $ 2 million akaitisha press conference na kutaja hiyo kama mafanikio ya ziara, wakati EPA zimeibiwa hela mara 70 ya hizo alizoopewa.
- Ardhi takribani ya ukubwa wa kisiwa cha Unguja amepewa mwekezaji na kufukuza wazawa Loliondo, hii ni mwaka huu.
- Alitembelea TRA akasema "nina majina ya wala rushwa wote hapa", sasa alifanyia nini majina yale?
- Amechagua baraza la mawaziri limejaa vihiyo na "wezi" haya ni maneno ya naibu waziri wa fedha juzijuzi , siyo yangu.

Rais wetu siyo decisive.
Mkuu wangu mifano kama hii ndio huniacha hoi kabisa! Lakini yanibidi kukubali kwamba sikutegemea kabisaaa na bado siamini..Ama kweli kila kitu kina sura mbili,
Wadhungu wanasemaga Don't judge a book by it's cover!
 
Kwa maoni yangu Kikwete uongozi umemshinda na mimi sioni chochote cha kumpongeza. Alipata ushindi wa “kishindo” kwa kuahidi kuipitia mikataba upya ya uchimbaji madini yetu ambayo ilisainiwa na Mkapa hadi hii leo pamoja na kuunda kamati ya madini bado mapendekezo yaliyotolewa na kamati hiyo hadi hii leo bado tunaendelea kupata 3% ya mapato yote ya dhahabu na kuwaachia wageni 97% ya mapato. Pamoja na bei ya dhahabu kuongezeka kwa kiasi kikubwa sana (Wakati Mkapa anasaini Bei ya dhahabu ilikuwa ni dola 233 na sasa ni zaidi ya dola 1,100. Kwa kifupi bado tunaliwa kwenye rasilimali zetu.

Aliahidi Maisha bora kwa kila Mtanzania, sijui kama alikuwa na mikakati ya kuhakikisha hili analifanikisha vipi kama kiongozi au ilikuwa na kauli tu ambayo haikuwa na mikakati yoyote bali ni katika kupata kura nyingi toka kwa Watanzania.

Kwenye swaala la ufisadi mpaka sasa hivi ameshindwa katika kila ufisadi uliofanywa dhidi ya nchi yetu. Tukianzia Kiwira ambayo Mkapa alijiuzia kiwiziwizi mgodi ule wenye thamani ya shilingi bilioni 7 kwa shilingi milioni 700 tu na kulipa shilingi 70 millioni. Hadi leo Mkapa hajachunguzwa iliWatanzania tufahamu ni nani aliyeidhinisha uuzwaji wa mgodi ule. Mkapa pia alichukua mkopo wa shilingi bilioni 7 toka NSSF na hadi hii leo hakuna anayefuatilia mkopo huo ili Mkapa na Yona waanze kuurudisha. Pia si ajabu Mkapa na Yona wanaweza kulipwa mabilioni ya shilingi na Serikali eti kuwafidia katika “gharama” walizoingia kuhusiana na Kiwira.

Tukija EPA kitendo cha kutwambia kwamba wahusika wa EPA wamerudisha shilingi bilioni 70 na wakati huo huo kushindwa kuyaweka majina ya watuhumiwa hao hadharani na kiasi kilichorudishwa na kila mmoja kwa maoni yangu ni usanii wa hali ya juu. Na mimi siamini kama watuhumiwa wa EPA wamerudisha hata senti tano vinginevyo sioni ugumu wowote wa majina yao na kiasi walichorudisha kuwekwa hadharani. Kesi za EPA nazo zimejaa usanii mtupu hili siyo siri kabisa wote tunalijua. Balozi wa Marekani nchini wakati ule aliahidi nchi yake kuisaidia Tanzania kumrudisha nchini mhusika mkuu Balalli kama Serikali ingewaomba msaada huo, lakini Kikwete akaamua kukaa kimya bila ya kuchangamkia msaada ule mpaka Balalli “akafa”

Tukija kwenye ufisadi wa Kagoda wa $40 millioni tunajua fika kwamba muhusika na ufisadi wa Kagoda papa fisadi Rostam hawezi kabisa kuguswa hivyo hadi hii leo hakuna uchunguzi wowote unaofanywa ili Watanzania tuweze kufahamu nini kilichojiri katika ufisadi wa Kagoda ambapo zilichotwa

Tukija kwenye Rada yule mtuhumiwa Vithlani alikuwa nchini anahojiwa na vyombo vya dola, lakini kwa kuwa ufisadi ule unawagusa vingune wengi katika awamu ya tatu na ya nne basi wakampa upenyo akimbie nchi ili kuwasitiri wahusika wa ufisadi ule wa $12 millioni


Kwenye Richmond/Dowans nako mapendekezo ya kamati iliyoundwa na Bunge mpaka leo Kikwete na Serikali yake imeshindwa kuyafanyia kazi bila kuwa na sababu zozote zile za msingi na wahusika waliochota $172 millioni bila kuzifanyia kazi bado wanapeta mtaani na huku mjadala wake ukiendelea kwa mwaka wanne sasa

Meremeta ambapo $155 millioni zilichotwa, hii tumeambiwa kwamba inahusiana na usalama wa Taifa na wizi wowote unaohusiana na usalama wa taifa haustahili kujadiliwa popote pale!!! Mhhh!

Rukia “Mipasho” Simba anasema hawezi kujiuzulu hadharani. “Mzee wa Vijisenti” Chenge “Mnyunyizaji” anatamka hadharani kwamba hakuna anayemchunguza kama yupo amfuate jimboni kwake. Papa fisadi Rostam kwa mara ya pili anaomba uchunguzi wa Richmond ufanyike tena kwa sababu hakubaliani na ripoti ya kamati ya Bunge mara ya kwanza alitaka uchunguzi mpya ufanywe na majaji. Haya yote yanaonyesha kwamba hawa wameshafahamu fika kiongozi wa nchi ambaye ana madaraka makubwa aliyokabidhiwa na Watanzania baada ya kumchagua kwa “kishindo” hana kabisa ubavu wa kuyatumia madaraka aliyokabidhiwa. Hawa kila mtu anaropoka kivyake vyake tu maana wanajua hakuna athari yoyote itakayowapata kutokana na kuropoka huko.

Mashule yetu bado mengi majengo yake hayana hata hadhi ya kuitwa ****** wachilia mbali madarasa, asilimia kubwa ya Wanafunzi bado wanakaa chini walimu ndiyo wa kubahatisha na wakti mwingine hawako kabisa, huko CCM kutokana na uongozi wake dhaifu migongano chungu nzima isiyokwisha na kuonyeshana ubabe hadharani, na mipasho ya hali ya juu na wengine hata kutishiwa maisha yao!!

Mimi kwa maoni yangu ukitilia maanani ufisadi wa Richmond, $172, EPA $133 millioni, Rada $12 millioni, Meremeta $155 millioni Kagoda millioni $40 basi ni haki kabisa kutumia ufisadi kama kigezo cha kumpima Kikwete na hata tukitumia vigezo vingine vyovyote vile hakuna hata kigezo kimoja ambacho anastahili kupewa pongezi.

Sasa tukitilia maanani hayo yote niliyoyaandika hapo juu tutaona kwamba Kikwete siyo tu hastahili pongezi zozote bali pia hastahili kugombea tena 2010. . Tumeshaona Kikwete kama kiongozi alivyo dhaifu katika mambo mbali mbali na hii kwa maoni yangu ni sababu tosha kabisa ya kuhakikisha tunapata kiongozi mpya 2010 ambaye atakuwa tayari kuyatumia madaraka aliyonayo bila kumuogopa yeyote yule.
Kama kiongozi mwenye mediocre perfomance kiasi hiki anashindwa kuambiwa kwamba kazi tuliyokupa imekushinda hivyo kaa pembeni ili tumtafute kiongozi mpya basi Tanzania tuna matatizo makubwa sana

Mchango wangu wa thumni huo
Mkuu mchango mzuri ila majibu yake kwa ufupi
1. Matumaini > kuliko matokeo hii ni kila mahali hata Obama wamerakani walitagemea makubwa lakini mara nyingi reality is always different from the expectations
2. Maisha bora hii ndugu very subjective kuna improvement kwa watu mbalimbali sehemu tofauti mfano:- walio pata JK loans, waliopata barabara na walienda shule kwa level zote Primary mpaka chuo kikuu nafasi ambazo hawakutegemea kabla....watu wenye access na dispensary kwa kila kata ni maisha bora hayo..usisahau financial crisis lakiniJK amaejitahidi japo anapita kwenye tanuri..lol
3. Ufisadi..gosh! waulize kina yona, mgomja, mramba wanavyohaha kwasababu ya dhambi hiyo ya ufisadi..najua unatamani sana RA,EL awemo kwenye list lakini rais si DPP wala AG hao ndio wataalamu wenye dhamana ya kushitaki au kuacha ...kutegemeana na ushahidi??? get your record right
JK amefanikiwa kwa vigezo vingi japo si vyote...next?
 
..............
Tuangalie mambo mengine mengi anayoyafanya na kufanikiwa mfano:

Kabla ya yote wewe ni mwanasiasa???? au?

a) Kuongezeka kwa enrollment kuanzia primary mpaka university kwa miaka ya ke minne --kielimu siyo mafanikio hayo??


Kuongezeka huko kumeleta manuufaaa gani tupe tasmini kila jambo alilolitenda kwenye elimu na wanafunzi wametoka na kitu gani???? we wasemea enrollment! Je lack of facilities kuwafanikishia masomo yao yaende vyema, hebu nijibu kwa elimu ipi Form 4 anaweza kujiimalisha kiuchumi ktk nchi hii au hata uyo aliyetoka University??? yani usitake niseme namachungu sana mie

b) Kuna program za kujenga zahanati kila kata..kusogeza huduma za afya karibu na wananchi---siyo mafanikio??


Zahanatiiii!!!!!!! teh teh teh teh mkulu mfano Mwananyamara Hospital tu inakasheshe nchi zima inaongoza kwa bad service kikubwa tu vifo vya wamama wajawazito wanapojifungua, hiyo tu tatizo no.1 kwa iyo scandal! wameshindwa kutunga tu sheria na utaratibu wa kumsaidia mtanzania mwenye kipato cha chini ya dolla mmoja na kumpa huduma tu yakumsikiliza nini shida yake???? nurse anataka kujua kama ana hela au raaaah jamani???? Hiyo ni mfano tu hapo ni JIJINI Dar inatokea hiyo tena its not even more than 15Km mahali anapo ishi Rais i mean Nyumbani kwa JK,Iweje leo unategemea huo mpango wa Zahanati utafanikiwa hata japo kwa 30%???? Je huko kijiji Kyela, Mureba,Mpanda, Makete? waambie warekebishe mfumo wa uongozi kwanza na ndio wataweza hilo.


c) Kuongezeka kwa utalii na watalii tangu ashike nchi..siyo mafanikio hayo???


Teh teh Utaliiiiiii unajua nini kuhusu utaliii mpwa wangu? wajua tuna mbuga ngapi weye?Do u know how much Nationa Parks zetu zina earn??? Na ni mikakati gani wanaboresha hizo Parks zetu????? Per Annum twaingiza ngapi??? Uliza South Africa Per Annum wanaingiza ngapi??? Hata tangazo la world Cup kwenye DSstv tu tumeshindwa kuliweka kama kweli kwenye utalii tume perform better,
Mkulu ar u joking au??

d) Barabara za lami mpaka kigoma.rukwa nasikia dodoma-arusha :confused:is on track..siyo mafanikio hayo?? kwa miaka minne


we kijana tembea uyaone acha porojo za kusikia kwa Radio au misafara ya hao viongozi. Dodoma Arusha its almost 490km kipande tokea minjingu kwenda babati ovyo tupu na ukitoka babati ndio wamekudanganya na hata kama ikijengwa ni kwaaajili ya siasa kwani uchaguzi ni 2010 walikuwa wapi iyo 4yrs???? na watuambie ni lini watatoka Dar Kuamia DODOMA?????Miundombinu ya DODOMA wataikarabati lini?? Dodoma haiwagharimu chochote mkuuu bali ni urasimu tuuuu, kwanini DAR yani watu hampumui mwang'ang'ania weeee kunani?? yania kiajana achana na ndoto za hao eti watakupotezea ramani zaidi mpwa, Chalinze mzeee ukipita kidogo tu kuelekea segera-tanga wanashindilia rami kama nini badala ya kuipanua kama Chalinze Moro wao wanaongezea rami, nisehemu chache sana tena za kuhesabu ndizo wanazo panua esp maeneo ya vitongoji au makazi ya watu huko porini kupishana tu esp usiku utaogopa mbaya.

e) Uhuru wa habari and tolerance of our president to the freedom of expression..zitto ameliona hili naye..


Hapo sina uhakika sana maaaan uhuru wa kujieleza umepewa nafasi na umejawa na siasa na ahadi za uongo mie kwangu naona ni wanafiki na waaandishi wa habari kila kukicha ni habari za wanasiasa na siasa tuuuuuu hawazungumziii maendeleo hata hayo wewe unayoyadai ati yapo sasa, huo ni ushahidi tosha free media press inaongelea nini sasa??? Au Umedanganyika na PADEPU ile miladi inasimamiwa na UN mkuu na ndio maaana inakwenda sisi tu wenyewe mbinde.

Bana ye mnyonge mnyogeni haki yake mpeni...mlitaka awafanyeje? wana JF mbona hamna shukrani hasa wewe mwanakijiji.


MKJJJ anakuhusu nini wewe umetumwa nini????? defend ur point dnt point fingers tu others Jiulize wewe umeifanyia nini serikali yako mkulu. Nanni mnyonge sasa hapa??????

Pole mpwa
 
Na kweli hivi kwa nini Makao makuu hadi leo hayajahamia Dodoma?

Mpwa upooooo teh teh,

Yani serikali ikulizwa nini kimewafanya mpaka sasa wasi hamie Dodoma hawna jibu hata kidogo mie sioni shida pale. 90's wakati wa Malecela as MP alikuwa anakaaa japo hata kidogo pale Dom sasa sijui yale majengo ni masafi mpaka sasa??

Dom kuna ikulu ya Rais na PM sasa siju wao wanataka nini majumba yapo ya kumwaga viwanja vipo wazi vingi tuuuu.

Tatizo la maji waitafutie sababu hapo kama Pius Mwandu aliweza divert mradi wa maji Shinyanga mjini na akaupeleka Maswa na mpaka leo maswa wanamaji mazuri zaidi ya Dodoma, iweje serikali ishindwe kuweka mitambo ya maji Dodoma?????

Jamani Ivi MUSTAKABALI WA NCHI YETU KTK SEKTA ZOTE ZA SERIKALI NI UPI???

maaana kila kiongozi ajae huja na mustakabali wake sijui huwa wanaufichaga wapi, maaana akija tu ana plan zake amezitoa huko siju hewani mtajionea vituko yaaani umejaaa siasa na si utekelezaji.

Yani
MUSTAKABALI WA NCHI YETU ulitakiwa kuwepo iwe ameingia kiongozi wa CUF,CHADEMA,TLP,CCM etc watakachotakiwa ni kufanya maboresho tuuu ya kiuchumi na kimaendeleo, kielimu na etc ili inchi iende faster wazidiane mbinu za kifikla na sio siasa zisizo na kichwa wala miguuu

hebooooooo

 
Statistics zipo kaka..hivi vyote ni vitu unaona kwa macho yako yote mfano:-
1. Watu wanaotuhumiwa wako mahakamani (baadhi) hilo nalo huoni?? rais gani amewahi kufanya acha tanzania hata hapo karibu kenya...ambayo ni 20 most corrupt country in the world
2. Barabara zote nilizosema nimeziona na kupita kwasababu ya kazi zangu..Rukwa-mbeya, rukwa-kigoma, dodoma-singida, Aursha-Dodoma (inaendelea), Arusha- singida (inaendelea) jamani kwa miaka minne ..he has done something worth ...
3. Shule na Zahanati zimeanza kujengwa kila kata..shule ofcourse imeanza wakati wa mkapa..lakini zahanati ni Kikwete iniative, vyuo vikuu vimejengwa (state university of dodoma for example)..enrollment kuanzia primamry mpaka chuo kikuu ni kubwa kupita wakati wowote nchini..need more..ni mafanikio hayo???

Mkuu mambo ya kuangalia na kuona hayapo tena mkuu. Kiongozi yoyote mafanikio yake hupiwa na facts siyo kwa kuangalia tu. Hao wanao tuhumiwa kwenda mahakamani kesi zote ni kiini macho tu. Wangapi umeona wame hukumiwa kwa makosa yao? Ditopile kaua wakaifanya manslaughter. Zombe yuko wapi?

Hizo barabara mkuu pia lete data. Kama kweli zime fanyika haku kosekani data. kajenga barabara ngapi? Ngapi zilikua initiatives zake? Haya mambo ya kuona tu yana danganya sana. barabara zinaweza hata kujengwa bila initiative ya raisi.

Mkuu UDom siyo Kikwete kabisa. That was all Mkapa. Ime kuja kumalizika tu wakati Kikwete ni raisi. Na kuhusu hizo enrollment mtu utaonaje kwa kuangalia tu mkuu? kama kweli zimeongezeka una shindwake kuweka data kwamba kabla ya Kikwete ilikua hivi na baada ya Kikwete imekua hivi? Unataka kuniambia enrollment unaweza kuona imeongezeka kwa kuangalia tu bila data?
 
Mkuu mambo ya kuangalia na kuona hayapo tena mkuu. Kiongozi yoyote mafanikio yake hupiwa na facts siyo kwa kuangalia tu. Hao wanao tuhumiwa kwenda mahakamani kesi zote ni kiini macho tu. Wangapi umeona wame hukumiwa kwa makosa yao? Ditopile kaua wakaifanya manslaughter. Zombe yuko wapi?

Hizo barabara mkuu pia lete data. Kama kweli zime fanyika haku kosekani data. kajenga barabara ngapi? Ngapi zilikua initiatives zake? Haya mambo ya kuona tu yana danganya sana. barabara zinaweza hata kujengwa bila initiative ya raisi.

Mkuu UDom siyo Kikwete kabisa. That was all Mkapa. Ime kuja kumalizika tu wakati Kikwete ni raisi. Na kuhusu hizo enrollment mtu utaonaje kwa kuangalia tu mkuu? kama kweli zimeongezeka una shindwake kuweka data kwamba kabla ya Kikwete ilikua hivi na baada ya Kikwete imekua hivi? Unataka kuniambia enrollment unaweza kuona imeongezeka kwa kuangalia tu bila data?

Umeshasahau kwamba Wanazuoni wa TZ bado wanatumia vigezo hivyo hivyo (bila ya facts) kumsifia Nyerere? Let's look the "history from below" and see who was a better leader between Kikwete, Mkapa, Mwinyi and Nyerere.
 
....... Let's look the "history from below" and see who was a better leader between Kikwete, Mkapa, Mwinyi and Nyerere.

JK Nyerere was the best pamoja na mapungufu yake yaliyokuwepo enzi zake still uchumi ulikuwa pazuri tu pamoja alikwenda vitani. serikali ilikuwa inamiliki sekta au nyanja nyingi za uchumi na kilimo. duh baaada ya kuachiwa mzeee wa ruksa na akafuatia Ben na b ro JK nae mmmhh yetu macho

Thnxk mpwa


 
Pole sana kaka na wewe nadhani unatoa hizi habari kwa wototo wa miaka 10.
Mie ni mtu wa miaka 50's sidanganyiki.
Mwinyi aliacha nchi haina kabisa pesa kwenye consolidated fund hizo pesa aliziomba wapi? Nchi ilikuwa na hali mbaya sana.
Tupe data ku Substantiate hoja yako hizo pesa alizipata wapi Mwinyi bwana.
Tunajua mpango mahususi wa mkapa wa kujenga barabara zetu kutokea katika internal funds alianzisha yeye na utekelezaji ulifanyika, na Mwinyi hastahili sifa yoyote kwa hili.
Narudia sisi ni watu wazima hatudanganyiki kwa kitu mkuu tumeshuhudia mengi ya uongo yakitolewa na watu kama nyinyi.
MF
Crystal and clear good one
 
Pole kaka, na pia asilimia kubwa ya barabara za Mkapa, zilikuwazishapangwa na kutafutiwa wafadhili na Mwinyi.

So kuna issue ya kupokezana vijiti mzee, ukiona mkandarasi yuko site, ujue kazi ya ujenzi na uchoraji ilianza miaka mitatu nyuma... okay!!!

So do not expect... unasanifu mwaka huu, unatoa tenda mwaka huu, ujenzi unaanza mwaka huu na unaisha mwaka huu... tulia kidogo ufikiri kaka... kujenga barabara sio sawa na kununua ndizi sokoni tandale.

..acha kupotosha ukweli wewe! barabara gn zilishatafutiwa fedha na kupangwa kutengenezwa,wakati nchi ilikuwa muflisi hoi bin taaban! inflation apprx.49% nchi ina madeni imeshindwa kulipa na hivyo kutokuaminiwa tena na wabia wa maendeleo!!

wewe unaona upangaji wa kujenga highway chalinze-segera badala ya kimara - chalinze ni wa watu wenye akili timamu???

..He s absolutely a failed leader!! labda tuhoji tu na uwezo wake wa kufikiri na kuamua kama kiongozi kwa ngazi ya rais kama bado anao!!
 
Nimechoka na vigezo vinavyotumika kupima uwezo na mafanikio ya rais wetu kwa muda wote katika JF forums je
1. Si halali kupima uwezo wa rais kwa kigezo kimoja tu cha kuzibiti ufisadi ..yaani EPA, Richmond..etc after all watuhumiwa wako mahakamani wengi tu..ala..
Tuangalie mambo mengine mengi anayoyafanya na kufanikiwa mfano:-
a) Kuongezeka kwa enrollment kuanzia primary mpaka university kwa miaka ya ke minne --kielimu siyo mafanikio hayo??
b) Kuna program za kujenga zahanati kila kata..kusogeza huduma za afya karibu na wananchi---siyo mafanikio??
c) Kuongezeka kwa utalii na watalii tangu ashike nchi..siyo mafanikio hayo???
d) Barabara za lami mpaka kigoma.rukwa nasikia dodoma-arusha is on track..siyo mafanikio hayo?? kwa miaka minne
e) Uhuru wa habari and tolerance of our president to the freedom of expression..zitto ameliona hili naye..
Bana ye mnyonge mnyogeni haki yake mpeni...mlitaka awafanyeje? wana JF mbona hamna shukrani hasa wewe mwanakijiji.

hivi unajua maana ya shule wewe?
shule inaweza kuwa hata chini ya mti wa mwembe na wanafunzi wakapatikana na kufaulu vile vile!
 
1. Ndugu, hakuna shida yeyote wananchi wa bagamoyo kupata barabara..ni maendeleo hayo?
2. Kuna barabara ya kwenda Handeni kutokea mkata inajengwa kiwango cha lami na kutokea korogwe kwenda handeni kiwango cha lami..ni maendeleo hayo...???
3. Kuna barabara ya Arusha -Dodoma, Arusha -singida kiwango cha lami..maendeleo hayo??
4. Barabara ya Rukwa-Kigoma, Rukwa -Mbeya kiwango cha lami..maendeleo hayo??
Hizi zote ni project za awamu ya nne?? miaka minne kafanya kazi bana ..acheni hizoo??
Kuna ndugu anasema mipango ya awamu ya tatu NO NO, Kuna mambo vile awamu ya tatu iliyakuta kutoka awamu ya pili..mfano barabara ya kusini (rufiji) ilishasainiwa na mwinyi na wafadhili kutoka kuwait lakini baadaye ilionekana kama ya Mkapa vile...tuwe wakweli bana!


kamanda unapoteza sana maana ya program kwa ujumla, kujenga barabara ni mipango ambayo huwa ya muda mrefu sana, somtimes huchukua hata miaka mitano kuanza ujenzi, so ukiona sasa kuna barabara za kwenda Dodoma-singida, Arusha-Dodoma na nyinginezo, watu walikaamuda mrefu na kuweka hiyo mipango, so akifanyacho Raisi wetu ni ile implementation ya hizo program, so far mimi naweza kusema kafanya jambo kubwa la freedom of speech, make wakati wa mzee Kipara kulikuwa hakuna kitu hicho, ilikuwa ni mabavu tu, na by this time Tanzania tunahitaji sana freedom of expression ili watu wote waliokuwa wakila bila kufanya kazi basi ukomo ufikie, watambae zao turudi vijana wachapa kazi, wenye vision ya kuindeleza nchi yetu iwe better place for all and not for few kama ilivo kwa sasa.
 
Tumaini, Institution zote hizo PCB (now PCCB), CAG office, Banking systems, investment climate, Macro ecomomic stability etc za utawala wa Ben, to this he deserve his credit. The incurmbent kakuta structures na istutirions ziko in place so much was expected.
 
Tumaini, Institution zote hizo PCB (now PCCB), CAG office, Banking systems, investment climate, Macro ecomomic stability etc za utawala wa Ben, to this he deserve his credit. The incurmbent kakuta structures na istutirions ziko in place so much was expected.

Prior Master, umezungumzia point muhimu sana... rais wa sasa amekuta everything on track including structures, institutions with surplus.. hivi leo nchi tena ina madeni na haina surplus... huyu hafai kusifiwa .... mi nasema both in macro and micro economics JK has failed, ila his loyal followers wako busy doctoring the figures lakini sasa imefika mahali ukweli haufichiki tena.
 
Tumaini, Institution zote hizo PCB (now PCCB), CAG office, Banking systems, investment climate, Macro ecomomic stability etc za utawala wa Ben, to this he deserve his credit. The incurmbent kakuta structures na istutirions ziko in place so much was expected.
Ndio maana ya vijiti kupokezana ndugu..Mkapa kakuta mambo kibao kwa mwinyi..na yeye JK ataacha vitu kibao ...kwa rais wa awamu ya tano...ndio tunaijenga nchi hivyo..
 
Tumain,

..JK ameikuta serikali ikiwa na hali nzuri kifedha kuliko mwaka 1995 wakati Mkapa anaingia madarakani.

..kwa kweli mimi nilitegemea JK atafanya mambo makubwa sana kuliko Mwinyi na Mkapa kwa kuzingatia kwamba alichukua nchi ikiwa na afueni ya kiuchumi/kifedha kuliko Maraisi hao wawili waliomtangulia.
 
Julius Nyerere will be remembered as a maverick who stood to the west. Shujaa wa mwisho Tanzania baada ya historia ndefu ya kina mkwawa

Ali Mwinyi will be remembered as a man who endorsed embezzlement within the government.

Benjamin Mkapa will be remembered as a man who welcomed foreign investement to make his quick buck.

And Jakaya Kwikwete will be remembered has a man who sold us back to colonial masters, rob us our land, destroyed future prospects by endorsing land reform (EAC) due to his naivity.

The man should step down quickly for the sake of our Tanznania. A coward can never take us anywhere. May be he should have been a foreign affairs minister for the passion he has on flying, but not our president.

The next one should be a well schooled patriot for the sake of our land and freedom.
 
Prior Master, umezungumzia point muhimu sana... rais wa sasa amekuta everything on track including structures, institutions with surplus.. hivi leo nchi tena ina madeni na haina surplus... huyu hafai kusifiwa .... mi nasema both in macro and micro economics JK has failed, ila his loyal followers wako busy doctoring the figures lakini sasa imefika mahali ukweli haufichiki tena.

Wewe ulimpigia (kama ulipiga kura) nani kura mwaka 2005?
 
Umeshasahau kwamba Wanazuoni wa TZ bado wanatumia vigezo hivyo hivyo (bila ya facts) kumsifia Nyerere? Let's look the "history from below" and see who was a better leader between Kikwete, Mkapa, Mwinyi and Nyerere.

So according to the facts you have who was the better leader? Nyerere, mwinyi, Mkapa or Kikwete? Just curious.
 
Back
Top Bottom