Kupatwa kwa satellite (satellite eclipse)

GM7

JF-Expert Member
Jun 26, 2009
492
24
Wana JF wote,

Mara chache sana tumekuwa tukishuhudia tukio la kupatwa kwa jua (Solar eclipse) na vile vile kupatwa kwa mwezi (Lunnar eclipse).

Je unafahamu kuwa kuna kupatwa kwa Satellite?

Napenda kuwajulisha kuwa tukio la kupatwa kwa satellite huwa linatokea wakati jua la utosi linakuwa katika mstari wa Equator (During Equinox). Kwa wale tuliosoma Geography tunakumbuka kuwa jua la utosi hupita katika mstari wa Equator kila tarehe 21 March na 23 September kila mwaka.

Tukumbuke kuwa Satellite zilizo nyingi zinaelea juu ya mstari wa Equator. Kwa mfano Satellite inayoitwa IntelSat ambayo iko degree 64.5"E inatumiwa na mawasiliano ya Radio na Tv karibu zote hapa Tanzania kama vile ITV, EATV, Star Tv, TBC1, Channel ten, Capital TV. na Radio kama vile RFA, TBC taifa n.k.

Wakati wa tukio hili la kupatwa kwa satellite Vituo vyote hivi vya Radio na TV hukata kabisa matatangazo yake kwa muda wa dakika kadhaa au saa nzima hasa tunaopata matangazo kwa njia ya satellite dishes hasa hasa mikoani hususan Mbeya.

Tukio hili naendelea kulishuhudia hivi sasa na mara nyingi hutokea kati ya saa 3:45 asubuhi na saa 5:00 asubuhi. Tukio hili huanza takriban wiki moja kabla ya Equinox. Kwa sasa toka juzi hadi tarehe 28 September kuanzia saa 3:45 asubuhi hadi saa 5:00 asubuhi hvi waweza kushuhudia tukio kwa kuangalia TV na Radio nilizotaja hapo juu.

What is a satellite eclipse period?
Since GOES is in a geosynchronous orbit, the sun will yearly traverse a +/- 23.5 degree angle perpendicular to the Earth's equator (GOES orbit plane). As a result, near the Vernal and Autumnal Equinoxes the Earth disk will periodically occult the sun, from a GOES perspective. Essentially, there are two eclipse seasons for each GOES spacecraft. Each eclipse season spans a 48-day period, symmetric around the equinox and the sun occultation lasts for a maximum of 72 minutes/day during the equinox. Each GOES spacecraft utilizes a solar array that converts sunlight into electricity in order to power the satellite. Each day during the eclipse season the sun is blocked by the Earth and sunlight is not available to the GOES solar array. Therefore, the energy needed to power the instruments is not available and the instruments are powered off. There is typically a 0-3 hour outage of imagery each day as GOES progresses through eclipse season. The maximum outage of 3 hours will occur at or near the equinox.

Pia ningependa vyombo vya habari hasa TV na Radio kuelimisha wananchi kuhusu tukio hili maana wenyewe huendelea kurusha matangazo wakati wa tukio hili maana hatuwapati kabisaaaa. Je wanafahamu kuhusu tukio hili?

Sasa tusiandikie mate wakati wino upo. Kesho saa 3:30 asubuhi hebu tushuhudie tukio hili kwa pamoja.
 
Tukio hili ndio muda huu liko live, Naona Tv zote za Tanzania tunazoangalia kupitia kwenye madishi muda hazionyeshi kabisa hii pia ni kwa baadhi ya Radio hasa huku mikoani ambazo hupokea matangazo yake kupitia kwenye satellite ya nyuzi 64 mashariki.

Tutaendelea kushuhudia tukio hili kwa takribani siku tano hivi. Tukio hili hutokea wakati ambapo jua la utosi linakuwa kwenye mstari wa Ikweta yaani MARCH 21 NA SEPTEMBA 23. kwa hiyo siku tatu au nne kabla na baada ya tarehe hizo ndipo utaweza kushuhudia tukio hili kila mwaka. Hutokea kati ya saa 4:00 ashubuhi na saa a 4:30 au saa 5:00 asubuhi kwa saa za Afrika Mashariki.

Naomba vyombo vyote vya habari viliweke wazi suala hili ambalo naona bado ni geni kwa baadhi ya watu.
 
Wana JF wote,

Mara chache sana tumekuwa tukishuhudia tukio la kupatwa kwa jua (Solar eclipse) na vile vile kupatwa kwa mwezi (Lunnar eclipse).

Je unafahamu kuwa kuna kupatwa kwa Satellite?

Napenda kuwajulisha kuwa tukio la kupatwa kwa satellite huwa linatokea wakati jua la utosi linakuwa katika mstari wa Equator (During Equinox). Kwa wale tuliosoma Geography tunakumbuka kuwa jua la utosi hupita katika mstari wa Equator kila tarehe 21 March na 23 September kila mwaka.

Tukumbuke kuwa Satellite zilizo nyingi zinaelea juu ya mstari wa Equator. Kwa mfano Satellite inayoitwa IntelSat ambayo iko degree 64.5"E inatumiwa na mawasiliano ya Radio na Tv karibu zote hapa Tanzania kama vile ITV, EATV, Star Tv, TBC1, Channel ten, Capital TV. na Radio kama vile RFA, TBC taifa n.k.

Wakati wa tukio hili la kupatwa kwa satellite Vituo vyote hivi vya Radio na TV hukata kabisa matatangazo yake kwa muda wa dakika kadhaa au saa nzima hasa tunaopata matangazo kwa njia ya satellite dishes hasa hasa mikoani hususan Mbeya.

Tukio hili naendelea kulishuhudia hivi sasa na mara nyingi hutokea kati ya saa 3:45 asubuhi na saa 5:00 asubuhi. Tukio hili huanza takriban wiki moja kabla ya Equinox. Kwa sasa toka juzi hadi tarehe 28 September kuanzia saa 3:45 asubuhi hadi saa 5:00 asubuhi hvi waweza kushuhudia tukio kwa kuangalia TV na Radio nilizotaja hapo juu.



Pia ningependa vyombo vya habari hasa TV na Radio kuelimisha wananchi kuhusu tukio hili maana wenyewe huendelea kurusha matangazo wakati wa tukio hili maana hatuwapati kabisaaaa. Je wanafahamu kuhusu tukio hili?

Sasa tusiandikie mate wakati wino upo. Kesho saa 3:30 asubuhi hebu tushuhudie tukio hili kwa pamoja.

Kuna pia swali hapa mkuu if dont you mind you may answer as well. Je kuhusu international phone calls vipi? I am trying to call from oversea siwapatai kabisa watu. Je na hili pia lahusika/
 
ebwanaaee. .. nikweli hadi baadhi ya satelite nyingine zinaathirika, sasa cjui kwa mawacliano ya cmu inakuaje .
 
Back
Top Bottom