Ndallo
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 7,619
- 4,292
Kitendo kilichojitokeza katika jiji la Arusha kuchafuka kutokana na vurugu za kisiasa kati ya wananchi na polisi yote haya ni kulazimisha ushindi usiokubalika na wananchi wa leo Tanzania kutokana na sasa kila Mtanzania aliyefikisha umri wa kupiga kura anajua haki yake ya msingi ya kumchagua na sio kumchagulia kiongozi asiekubalika katika jamii hii ya leo ndani ya nchi hii. Narudia tena ile kauli ya aliyekua waziri mkuu kwenye serikali ya awamu ya kwanza raisi akiwa baba wa taifa (Mungu amrehemu na amuweke mahali pema peponi) muheshimiwa Joseph Sinde Warioba alihawahi sema nanukuu: WATANZANIA NI WAPENDA AMANI SANA NA WASIZARAULIWE! NA SIKU WATAZARAULIWA ITAFIKA SIKU WATASEMA BASI! mwisho wa kunukuu. Sasa natumaini watanzania wameshaelewa usemi huu wa kiongozi huyu katika taifa hili na tumeshayaona na yametokea kuanzia kumalizika kwa uchaguzi mkuu hadi hapo majuzi watu hadi kupoteza maisha na huu naona ni mwanzo tu endapo serikali iliyopo madarakani haitawasiliza wananchi ni nini wanataka au wanataka kiongozi gani kweli damu za watu wasiokua na hatia itaendelea kumwagika na ile sifa aliyotuachia baba wa taifa itatoweka na nnchi hii kupoteza ile sifa ya Tanzania ni nnchi ya amani. Ili muafaka na amani irudi tena Arusha hakuna budi CCM na CHADEMA kurudia uchaguzi wa Umeya ili haki ipatikane na atakayeshindwa ayakubali matokeo na sio kulazimisha. Natanguliza hoja hii mbele yenu enyi wapenda amani.