Rugas
JF-Expert Member
- Jan 8, 2009
- 1,048
- 196
Siku za karibuni watanzania tumeanza kusikia kuwa sasa dada zetu wanaweza kuongeza makario,maziwa na kubadili mionekano yao kwa kutumia madawa yanayopatikana kwenye maduka ya vipodozi.Swala hili limezua mjadala hasa pale Mamlaka za umma km vile MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA kuanza kuzuia madawa hayo na kusema yana madhara kwa binadamu.
Hapo ndipo yanapozuka maswali mengi miongoni mwa watanzania;
1.Je hapo mamlaka na vyombo vya habari vinazuia au vinawafahamisha
wadau kuwa sasa mnaweza kujibadilisha na kupendeza?
2.Je mbona hizi mamlaka hazijazuia madawa ya kuongeza ukubwa wa
uume,ambayo pia yanasemekana kuwa na madhara na yanatangazwa
mpaka kwenye maTV? Huku si kupendelea upande mmoja na kuacha upande
mwingine uangamie?
3.Je madawa haya yanapita wapi,mpaka yasambae nchi nzima?Kuna udhibiti
hapo kweli?
4.Njia hizi si zinatumika pia kuzuia madawa ya kulevya na vingine
haramu,mbona hakuna mafanikio?
5.'UVUTAJI WA SIGARA UNAZURU AFYA YAKO' basi pia tuandike UTUMIAJI WA CREAM HII UNAZURU AFYA YAKO,turuhusu watu watumie km tulivyoruhusu sigara huku tukijua zina madhara makubwa..
6........................
7.........................
8.......................
Maswali ni mengi,yakijibiwa tutakuwa tumefanikiwa katika hili..