Kuondolewa kwa Lowassa, Chenge na RA - CCM na hatima yake na yao

Chama kitabaki tu watoke bwana. Nani kasema hatuna wafanyabiashara wazuri wasiotajwa na wananchi wanaoweza kutusaidia tukashinda 2015 bila tabu? Si bora tuendelee na utaratibu wa kusaka misaada ya kampeni nje ya nchi tu?
 
Nguvu ya CCM ni wenye fedha tena fedha chafu. Wanapokomaa na Mafiga matatu ya fedha ndani ya chama chao na kutaka kuharibu, maana yake nini?

Ushindi wao utatoka wapi? Watapewa fedha na nani?

Naona CCM bila Rostam, Lowassa na Chenge ni sawa na chai bila sukari.

let it collapse slowly but surely!
 
Unaweza kuwa una hoja hapa. Mgombea Urais wa JMT kwa tiketi ya CCM muda wote huu amekuwa akiteuliwa kutoka Kamati Kuu hii. Lakini kwa nguvu mpya ya pesa sasa hivi yeyote anaweza kuteuliwa.
 
No! Mwelekeo wa kutoa gamba si wa kubeza jamaa wanajipanga kwa sababu yaonekana kelele za cdm wamezifanyia kazi kiaina wamefahamu tatizo si walipoangukia bali walipojikwaa.Mwenzako akinyolewa wewe tia maji!!!

Wisdom is the reward for listening overlifetime!!!Watch-out!!!:disapointed:
 
Suala la "kuvua gamba" ndani ya CCM ni suala nyeti na muhimu ili kurejesha heshima ya Chama hiki kikongwe. Hata hivyo watu waliotuhumiwa kuwa "vitimbakwiri" (mafisadi) si hao tu waliotuhumiwa wapo wengi. Kwa hiyo, kwa mtazamo wangu bado Chama tawala kina kazi kubwa ya kujivua gamba. Mbali na ukitimbakwiri yapo magamba mengi ambayo viongozi wengi wa CCM wanahitaji kuyavua kisha wavae mavazi mapya kama wana nia thabiti ya kuwaongoza Watanzania. Magamba wanayohitaji kuyavua ni pamoja na ukitimbakwiri wenyewe, kutokuwa na uwezo wa kuongoza, fitina, chuki binafsi, uwongo, wivu, ushirikina, uvivu wa kufikiri na ubinafsi uliojaa ndani ya fikra na mioyo yao. Wakiweza kujigambua hayo magamba niliyoyataja na kuuvaa mavazi ya uzalendo, utu wema, upendo kwa Watanzania kuliko nafsi na familia zao pekee, kumtegemea Mungu badala ya waganga, taaluma na utaalamu, weledi badala ya uwongo, ujanja ujanja na hila katika kuwaongoza Watanzania basi watakuwa wamejivua gamba na dhana nzima ya Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete itakuwa na maana na tija kwa Watanzania. Tatizo la baadhi ya viongozi wa nchi hii ni kuvaa barakoa (kinyago) cha kondoo huku ndani ni mbwa mwitu wenye nia ya kuirarua Tanzania na tasilimali zake na Watanzania na rasilimali zao kwa faida yao na watoto wao bila kujali walio wengi. Viongozi wa namna hii wanafikiria nini? Au hawajui hawakuja na kitu duniani na hawatoka na kitu? Inakuwaje hata wanapohudhuria maziko ya rafiki na ndugu zao hawagundui kwamba "sanda" haina mfuko! Unajua sanda haishonewi mfuko kwa sababu mtu anapokufa hatahitaji TZS 500/= za kununulia soda njiani kuelekea ahera! Huko hakuna kiu wala njaa ni ama motoni milele ama paradiso milele! Hivi hawa hawajui haya na kama hawawezi kujua haya watawezaje kutuongoza? Mtu msafi akichafuka hatangoja kuambiwa kaoge!
 
Suala la "kuvua gamba" ndani ya CCM ni suala nyeti na muhimu ili kurejesha heshima ya Chama hiki kikongwe. Hata hivyo watu waliotuhumiwa kuwa "vitimbakwiri" (mafisadi) si hao tu waliotuhumiwa wapo wengi. Kwa hiyo, kwa mtazamo wangu bado Chama tawala kina kazi kubwa ya kujivua gamba. Mbali na ukitimbakwiri yapo magamba mengi ambayo viongozi wengi wa CCM wanahitaji kuyavua kisha wavae mavazi mapya kama wana nia thabiti ya kuwaongoza Watanzania. Magamba wanayohitaji kuyavua ni pamoja na ukitimbakwiri wenyewe, kutokuwa na uwezo wa kuongoza, fitina, chuki binafsi, uwongo, wivu, ushirikina, uvivu wa kufikiri na ubinafsi uliojaa ndani ya fikra na mioyo yao. Wakiweza kujigambua hayo magamba niliyoyataja na kuuvaa mavazi ya uzalendo, utu wema, upendo kwa Watanzania kuliko nafsi na familia zao pekee, kumtegemea Mungu badala ya waganga, taaluma na utaalamu, weledi badala ya uwongo, ujanja ujanja na hila katika kuwaongoza Watanzania basi watakuwa wamejivua gamba na dhana nzima ya Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete itakuwa na maana na tija kwa Watanzania. Tatizo la baadhi ya viongozi wa nchi hii ni kuvaa barakoa (kinyago) cha kondoo huku ndani ni mbwa mwitu wenye nia ya kuirarua Tanzania na tasilimali zake na Watanzania na rasilimali zao kwa faida yao na watoto wao bila kujali walio wengi. Viongozi wa namna hii wanafikiria nini? Au hawajui hawakuja na kitu duniani na hawatoka na kitu? Inakuwaje hata wanapohudhuria maziko ya rafiki na ndugu zao hawagundui kwamba "sanda" haina mfuko! Unajua sanda haishonewi mfuko kwa sababu mtu anapokufa hatahitaji TZS 500/= za kununulia soda njiani kuelekea ahera! Huko hakuna kiu wala njaa ni ama motoni milele ama paradiso milele! Hivi hawa hawajui haya na kama hawawezi kujua haya watawezaje kutuongoza? Mtu msafi akichafuka hatangoja kuambiwa kaoge!

maneno ya hekima haya...

kumbe gamba halijavuliwa; ila linaendelea kuvuliwa.

tusubiri tuone.
 
mimi nawashauri Chadema wawachukue wakina EL, AC na RA , LAKINI kwa MASHARTI. Kwamba hawatapewa wadhifa wa juu kwenye Chama NA waje na wakati wanapokea kadi za uananchama WAKABIDHI DOCUMENTS ZOTE dhidi ya madudu ya serikali na chama tawala.
 
kila nikifirki juu ya ukaribu wa JK na EL sioni atamtosa vipi !Tutakuja kusikia Mwakyembe katulizwa, na kuja kutuambia kwamba report ya RICHMOND haikusema Waziri Mkuu EL amehusika ! kwa hiyo EL sio fisadi ! hapo ndio mchezo utaanza rasmi!
 
Ccm walivyo wanafiki wataka waondoke tu kwenye vyeo vya ccm lakini waendelee na ubunge huu ni upuuzi................wangefukuzwa kabisa hata ubunge km kweli wanataka kujivua magamba................ccm wanaklumbuka shuka saaizi kukiwa kweupeeeeee.............

anatakiwa kuvitema vyeo vyote hivyo.
 
Nguvu ya CCM ni wenye fedha tena fedha chafu. Wanapokomaa na Mafiga matatu ya fedha ndani ya chama chao na kutaka kuharibu, maana yake nini?

Ushindi wao utatoka wapi? Watapewa fedha na nani?

Naona CCM bila Rostam, Lowassa na Chenge ni sawa na chai bila sukari.

Sir R, ni upungufu wa kufikiri, kama unafikiri uhai wa chama chochote unategemea mtu mmoja au wawili, sembuse RA, EL na Chenge.
Sasa wewe mwenyewe jiulize kama TANU hatimaye CCM vilianza 1954 na 1977, hao unao wataja walikuwa wapi hadi chama kikakua na kuimarika.
Ni vizuri ukaelewa kuwa hawa walidandia chama kwa maslahi yao binafsi na wenye chama(wananchi) walitishia kuchukua maamuzi mazito kwa ridhaa au bila ridhaa ya viongozi.Tishio la kukitosa chama lilikuwa dhahiri na linaonekana wazi.
Ushahidi ni matokeo ya uchaguzi 2010.
CCM wamegutuka, wamezisoma alama za nyakati na wamechukua hatua madhubuti kudhibiti kundi la wana CCM maslahi.
Ni uamuzi mgumu , lakini kama operation, hiyo ni dawa ya kukiokoa chama.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom