Jumapili siku ya tarehe 10 mwezi huu kituo kimoja maarufu cha redio kilirusha kipindi kikimuhoji dada mmoja muathrika wa ukimwi aliyeombwa damu na mama mmoja ambaye anafahamiana nae. Lakini kwa kujua kuwa si sahihi yeye kutoa damu yake ikatumike kumuathri mtu mwingine alikataa na wakati huo tayari alikuwa ameshafikishwa hospitali fulani ya binafsi.
Huyo mtu wa maabala alitumia muda mwingi kumbembeleza huyo dada akubali ili hali yule mama aliyempeleka pale akiwasiliana na watu wengine kwa simu akilalamika kwamba yule dada amekataa. Yule dada (muathrika) anaamini kuwa ule ni mtandao si kwamba yule mama alikuwa peke yake. Pia walikuwa wanajadili kumuongezea hela kama hiyo laki moja anaiona ndogo na wakamwahidi bado wataendelea kumpa deal kwani wanahitaji sana damu yake!
Pia katika kipindi hicho kulikuwa na kijana mmoja ambaye yeye ni kibaka anayetumia hiyo damu kuchoma watu wanaokuwa wabishi kutoa walichonacho wakiingia katika mitego ya huyo kijana na wenzake.
Je ni kweli serikali haiwezi kuwatafuta hao watu wakasaidia katika uchunguzi?
Au ni wazo zuri - to do nothing?
Source: J2 - Radio ya watu.
Huyo mtu wa maabala alitumia muda mwingi kumbembeleza huyo dada akubali ili hali yule mama aliyempeleka pale akiwasiliana na watu wengine kwa simu akilalamika kwamba yule dada amekataa. Yule dada (muathrika) anaamini kuwa ule ni mtandao si kwamba yule mama alikuwa peke yake. Pia walikuwa wanajadili kumuongezea hela kama hiyo laki moja anaiona ndogo na wakamwahidi bado wataendelea kumpa deal kwani wanahitaji sana damu yake!
Pia katika kipindi hicho kulikuwa na kijana mmoja ambaye yeye ni kibaka anayetumia hiyo damu kuchoma watu wanaokuwa wabishi kutoa walichonacho wakiingia katika mitego ya huyo kijana na wenzake.
Je ni kweli serikali haiwezi kuwatafuta hao watu wakasaidia katika uchunguzi?
Au ni wazo zuri - to do nothing?
Source: J2 - Radio ya watu.