Kuoa au kuoelewa na mtu mwenye watoto...kanuni zake ni zipi?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
[h=6]Ni kweli kwamba wanaume wa KiTZ hawawi wepesi sana kuwa na mahusiano na mtu mwenye watoto kutoka mume wa awali aumwanamme mwingine? Yaani siyo uhusiano wa kimapenzi tu bali uhusiano wa hata kufikia ndoa? Ni kwa kiasi gani uhusiano wa namna hiyo unaweza kujengwa vizuri bila kuleta mgogoro kati ya huyo mwanamme na watoto? Kwanini katika jamii za wenzetu - hapa natumia mfano wa Marekani - watu wanaonekana kuwa na utamaduni wa kawaida wa "old husband na new husband"? Kweli mwanamme unaweza kuwa na amani na mke mwenye watoto ambaye mume/bwana wake wa zamani yupo hai na angependa kuwa na mahusiano na watoto wake?

Kama una mpenda kweli mtu huyo ni kanuni gani ziwaongoze katika mahusiano ya wewe na watoto wake au na ex wake?

Maoni Please.
[/h]
 
Divorce za kibongo ni za hisia na makali yake ni short lived!

Hivyo kama unaishi jirani na mtalaka wa mkeo, kuwa makini sana maana any time wanalianzisha la zamani!...tena worse ni kwamba kwa vile jamaa anajua hana msalaba mkubwa(yaani hana binding responsibilities na huyo mtalaka wake), basi kwenye hii second chance ataonyesha penzi la Next Level na kum'allure na vitu kibao ili kumwonyesha huyo mwanamke kuwa mumewe wa sasa hana jipya!

Kwa habari ya watoto... ,well, hawana shida, kama mtu ana silika ya kupenda watoto atawapenda tu hata watoto wa kuja!
 
Ngoja niwape clip hii inaongelea kidogo wenye watoto na mdada anasema ni kwa nini siyo preference yake akidai kuwa wataharibu budget kuwatunza (though hii ni US could be less relevant to TZ situation but one can find a lesson)

It is a fun clip kwa wale wanaofikiria online dating; wanashauri watu waangalie profile then background kuona kama a person is telling the truth; mfano mtu anasema I like traveling wakati hana hata picha za places jua ni muongo.

Na wanasema usiangalie sura kabla ya profile na background check kwani utaja fall kwa sababu ya sura ukijachemsha utabaki ooh I loved him cause he was gorgeous. lol

On-Line Dating Tips



 
Ni upendo na uvumilivu kwa mkeo na wanawe! Pia uwe tayari kuwahudumia hao utakaowakuta, nadhani hapo maisha yatakuwa poa kwako.
 
Tatizo ni wivu..ubinafsi...kutokujiamini na kutokuaminiana.

Sioni kama swala la mwenye watoto kutaka kuwa na mahusiano na wanawe lina ubaya wowote ikiwa kila kitu kinafanywa kwa makubaliano.
Ni muhimu wenye mahusiano wakajadiliana pamoja kila kitu kuhusu watoto...watakaa wapi..watasoma wapi...wataishi vipi nyumbani...mawasialiano na baba yao yatakua vipi na kwa kiasi gani na mambo kama hayo. Yani kabla mama hajakaa chini na mwenye watoto na kuwekeana mipaka na makubaliano mama awe ameshaongea na mwenzake.
Niliona sehemu mtu anasema eti ''utajisikiaje amani wakati mwanaume mwingine anaweza kuja kwako wakati wowote kwa kisingizio cha watoto?'' well hii inaweza kutokea tu ikiwa mawasiliano ya mke na mume sio mazuri au hawajaweka masharti. Na kwanini huyo mtu akitaka kuwaona watoto aende kwa mwanaume mwenzake??Hana kwake watoto wakamsalimie huko au haaminiki kiasi cha kushindwa kupewa watoto hata kwa masaa matatu atoke nao??Kwasababu tu mtu ana watoto na mpenzi/mkeo haina maana kwamba atakua shemu ya maisha YENU...bali atakua sehemu ya maisha ya MTOTO na inawezekana ikawa hivyo bila kuingilia mahusiano yenu wawili.

Kwahiyo mwisho wa siku muhimu ni mwanaume awe anapenda watoto naturally...amwamini mwenzake (kama hana sababu ya kutokufanya hivyo)...wajadiliane kuhusu malezi ya mtoto na uhusiano wake na baba mtu bila kusahau kujiamini.Ukiachilia mbali wale sitaki/nataka ambao hata wakiachana na mtu bado wanajihusisha nae jua kwamba huyo unayemwita mwenzako aliachwa , wewe ndie mwenye mali sasa....ACT LIKE IT.
 
Km umeolewa ukakuta watoto wamwenzio ishi nao km wa kwako coz huna maagano na mungu kuwa uatakuwa hai na kuwalea wa kwako mpaka wakue,mwamini mmeo na kukotroo wivu na hisia mbaya juu yake na mzazi mwenzie,km umeoa na kukuta watoto wa mwenzio hali kadhalika mwamin mkeo na kutoruhusu hisia mbaya kuuteka moyo wako kwan ww na yy ndio mpango wa mungu muwe pamoja maishani.
 
Back
Top Bottom