Kunuka kikwapa: Fahamu chanzo, tiba na namna ya kuepuka tatizo

Jamani naombeni msaada kwenye hili suala kutoa harufu makwapani. Nina uhakika kwamba, hakuna mtu miongoni mwetu, ambaye ameishafikia balehe, na hajawahi kukumbwa na tatizo hili la kunuka KIKWAPA. Wengi wetu tunakabiliana na hali hiyo kwa kutumia DEODORANTS za aina mbalimbali na PODA kwa wakina dada. Lakini maelfu, hususani kwa huko nyumbani, aidha kwa sababu ya hali ngumu ya maisha au kutokuwa aware na hali hii au kwamba kuna vitu unavyoweza kutumia ili kukabiliana na hali hii, basi suala hili limepuuzwa.

Mpaka miezi miwili iliyopita, nilikuwa nafanya kazi kwenye NGO moja hapa Ughaibuni, ambayo inayojishughulisha na kuwa-integrate the newly arrived immigrants katika mambo ya Lugha (English/French), local culture, na Employment. Hivi karibuni tulipokea wageni kadhaa kutoka Zimbabwe na Congo, na ambao baada ya kuwakaribisha na kuwaonyesha sehemu mbalimbali za kupata huduma (Hospital, School, na Metro Transportation), tuliwapeleka sehemu mbalimbali ili kuanza ajira. Sasa, katika kufuatilia maendeleo yao huko makazini, hakukuwa na malalamiko kuhusu utendaji wao wa kazi. Malalamiko makubwa kutoka kwa ma-supervisors wao ni kwamba baadhi ya hawa jamaa wanatoa harufu kali sana (Kikwapa), haswa wakati wa kupiga boksi. Wakatuomba tuwashauri hawa jamaa wawe WANAOGA kila siku. Nimejaribu kuwafahamisha hawa jamaa kwamba hawa wageni wanaoga kila siku, isipokuwa hawajazoea kutumia Deodorant. Supervisors hawaamini kwamba mtu anayeoga kila siku atakuwa ananuka kikwapa kiasi hicho.

Kivumbi kilichonipata ni kwamba, nilipowashauri hawa jamaa kuhusu tatizo hili na kuhusu matumizi ya Deodorants, baadhi yao hawakufurahishwa na ushauri wangu. Moja wao (kutoka Congo- Kinshasa) kanishutumu kwamba nimeishabadilika kimaadili kwa kuiga tabia za wazungu!!!

Sasa swali ni je, ni kweli kwamba Waafrika peke yao ndio wenye kunuka KIKWAPA? Pili, utamshauri vipi mtu kuhusu suala personal kama hili? Na mwisho kabisa, je dada zetu wanadeal vipi na hali kama hii katika mahusioano yao? Haswa tukizingatia kwamba mke au rafiki lazima anajuwa kilema cha mume au boyfriend wake.

Je, wakina dada wanawaambia ukweli waume na marafiki zao ili kukabiliana na hili TATIZO? Nasita kutumia neno AIBU kwa sababu nafahamu kwamba kuna baadhi ya jamii na makabila ambayo yanatumia zaidi harufu zao (Olfaction) kuliko kuona au kugusa katika maisha yao ya kawaida. Lakini nimeishashuhudia mara kadhaa Wazungu na makabila mengine wakiwanyanyasa watu weusi kwa sababu ya tatizo la KIKWAPA. Msemo kwamba WAAFRIKA WANANUKA ndio imekuwa joke kwenye sehemu nyingi za kazi.

Things in Perspective:
Suala la kutoa harufu (yoyote) linaweza kuangaliwa katika sehemu kuu mbili au tatu muhimu: 1. Power 2. Classs, 3. Racism kama inavyoelezwa na Ruth Finnegan (2007): Odour is a peculiarly emotive basis for social inclusion and exclusion, often invoked by powerful groups to both distinguish and stigmatised those they classify as inferior or alien (Finnegan 2007).

Mfano:-England wakati wa Industrial Revolution; the Bourgeoisie class waliwashutumu the Proletariat class kwa kutoa harufu mbaya.

-Britons walipokuwa wanaitawala India waliwashutumu Wahindi kwa harufu mbaya.
Racism/Discrimination: Nchini Marekani, haswa wakati wa UTUMWA, wakati wa Civil Rights Movement na mpaka leo wanawashutumu Wamarekani weusi kwa kutoa harufu mbaya.

-German (Third Reich) iliwashutumu European Jews kwamba wanatoa harufu mbaya, pengine kuliko binadamu yoyote yule Duniani.

-Wakati huohuo kuna baadhi ya makabila au jamii ambazo hutumia harufu katika maisha yao ya kila siku. Kwa mfano, The Desana- Amazon Rain Forest, the Umeda- Papua New Guinea, na the Dassanetch- Ethiopia. Kwa tamaduni za haya makabila; harufu ya kila kitu ni muhimu kuliko kuona (Smell outdistance sight).:A S 39:
 
Huo ni unyanyapaa tu wa wazungu. Mbona waafrika ni wasafi kuwazidi hao wazungu ambao wanaweza kumaliza hata wiki bila kugusa maji. Kwao mapafymu tu. Mnuko unatumiwa kama silaha ya dharau, ubaguzi, nk kama ulivyoitoa hapo juu. Si kweli kwamba waafrika wote wana kikwapa, japo yawezekana wachache wakawa wachafu.
 
Huo ni unyanyapaa tu wa wazungu. Mbona waafrika ni wasafi kuwazidi hao wazungu ambao wanaweza kumaliza hata wiki bila kugusa maji. Kwao mapafymu tu. Mnuko unatumiwa kama silaha ya dharau, ubaguzi, nk kama ulivyoitoa hapo juu. Si kweli kwamba waafrika wote wana kikwapa, japo yawezekana wachache wakawa wachafu.

Umesema kweli Babu, hao wazungu wanaojiona wasafi wanategemea ma'cosmetics lakini ni wachafu wachafu.
 
Tena asikuambie mtu....Hakuna mtu anaeyenuka kama hawa weupe.....wavivu kuoga na wanajipulizia sana manukato na sometymz unakuta yeye mwenyewe ananuka na kisha anajipulizia manukato murua (Harufu nzuri + Mbaya = ............) Unyanyapaa usio na msingi.....
 
Mh jamani hii kweli haitokani na imani kuwa njemba haitakiwi kunukia? Hili lalamiko ni la kawaida sana. Nimeliskia mara nyingi nilipokuwa USA.

Nadhani kwa miaka ya nyuma watu hawakupenda kunukia nukia, nafahamu watu ambao hata kuogea sabuni kama lux ana Rexona walikuwa wanaona ni marashi ati sabuni ya mwanaume ni lifebouy.

Naomba msamaha kama nimekosea, lakini ni kweli atu wa umri fulani walikuwa hawapendi kutumia deodorant. Vijana wetu siku hizi wanajitahidi.
 
.... Wakatuomba tuwashauri hawa jamaa wawe WANAOGA kila siku. Nimejaribu kuwafahamisha hawa jamaa kwamba hawa wageni wanaoga kila siku, isipokuwa hawajazoea kutumia Deodorant. Supervisors hawaamini kwamba mtu anayeoga kila siku atakuwa ananuka kikwapa kiasi hicho.

Kivumbi kilichonipata ni kwamba, nilipowashauri hawa jamaa kuhusu tatizo hili na kuhusu matumizi ya Deodorants, baadhi yao hawakufurahishwa na ushauri wangu. Moja wao (kutoka Congo- Kinshasa) kanishutumu kwamba nimeishabadilika kimaadili kwa kuiga tabia za wazungu!!!

Sasa swali ni je, ni kweli kwamba Waafrika peke yao ndio wenye kunuka KIKWAPA? Pili, utamshauri vipi mtu kuhusu suala personal kama hili? Na mwisho kabisa, je dada zetu wanadeal vipi na hali kama hii katika mahusioano yao? Haswa tukizingatia kwamba mke au rafiki lazima anajuwa kilema cha mume au boyfriend wake.

Je, wakina dada wanawaambia ukweli waume na marafiki zao ili kukabiliana na hili TATIZO? Nasita kutumia neno AIBU kwa sababu nafahamu kwamba kuna baadhi ya jamii na makabila ambayo yanatumia zaidi harufu zao (Olfaction) kuliko kuona au kugusa katika maisha yao ya kawaida. Lakini nimeishashuhudia mara kadhaa Wazungu na makabila mengine wakiwanyanyasa watu weusi kwa sababu ya tatizo la KIKWAPA. Msemo kwamba WAAFRIKA WANANUKA ndio imekuwa joke kwenye sehemu nyingi za kazi.
Things in Perspective:

Huo ni unyanyapaa tu wa wazungu. Mbona waafrika ni wasafi kuwazidi hao wazungu ambao wanaweza kumaliza hata wiki bila kugusa maji. Kwao mapafymu tu. Mnuko unatumiwa kama silaha ya dharau, ubaguzi, nk kama ulivyoitoa hapo juu. Si kweli kwamba waafrika wote wana kikwapa, japo yawezekana wachache wakawa wachafu.

.Tukubali kukosoana.

Unaposhauriwa harufu ya mwili wako ni kero kwa wenzako, fanya jitihada kusawazisha hitilafu hiyo. Kunuka mdomo, kikwapa, na hata sehemu za siri sio sifa... ni karaha. Haijalishi wewe ni Muafrika, Mzungu au mhindi. Personal Hygiene ni muhimu.

Huenda wenyewe tunastahmiliana kutokana na ugumu wa hali za maisha, lakini harufu mbaya haimpendezi kila mmoja wetu, iwe ni Tanzania au hata huko ugenini. Jifikirie umo kwenye taxi yenye kiyoyozi halafu dereva ananuka kikwapa!

Tujitahidini jamani.
 
Nina rafiki yangu mmoja wa kizungu, yeye anatoka na wanawake weusi tu, nilipomuuliza kwanini anapenda pussy nyeusi, akanijibu weusi ni wasafi sana kuliko weupe, kwasababu tunajihisi tunanuka kwahiyo tuna kuwa na extra care kuhusu usafi wa miili yetu. Wa IRISH wanaoga once a week tena Friday, sasa sijui hapa nani ananuka. Wao wananuka ndio maana wakagundua ma deodorant na maperfume ili kuficha harufu.
 
Nina rafiki yangu mmoja wa kizungu, yeye anatoka na wanawake weusi tu, nilipomuuliza kwanini anapenda pussy nyeusi, akanijibu weusi ni wasafi sana kuliko weupe, kwasababu tunajihisi tunanuka kwahiyo tuna kuwa na extra care kuhusu usafi wa miili yetu. Wa IRISH wanaoga once a week tena friday, sasa sijui hapa nani ananuka.
wao wananuka ndio maana wakagundua ma deodorant na maperfume ili kuficha harufu

LOL, what a sarcastic remark from your friend!
 
...tukubali kukosoana.

Unaposhauriwa harufu ya mwili wako ni kero kwa wenzako, fanya jitihada kusawazisha hitilafu hiyo. Kunuka mdomo, kikwapa, na hata sehemu za siri sio sifa... ni karaha. Haijalishi wewe ni Muafrika, Mzungu au mhindi. Personal Hygiene ni muhimu.

Huenda wenyewe tunastahmiliana kutokana na ugumu wa hali za maisha, lakini harufu mbaya haimpendezi kila mmoja wetu, iwe ni Tanzania au hata huko ugenini. Jifikirie umo kwenye taxi yenye kiyoyozi halafu dereva ananuka kikwapa!
Tujitahidini jamani

Ulichosema mkuu ni sawa. Hata sisi hatupingi kuambiwa kuwa msafi mwili, kinywa, mavazi. Haya yote ni sawa. Tunachopinga na kukataa ni ku-categorize watu wa rangi fulani kwamba ndo wenye kikwapa. Hii si kweli. Kunuka kikwapa ni uchafu wa mtu binafsi, hauna cha rangi wala kabila.

Mtu yeyote asipojitunza atanuka. Hivyo dhana ya kwamba waafrika tunanuka (kwa sababu tu waafrika) ni dhana potofu, ya kibaguzi, na madharau. Ndo mana mi nikasema mbona hata wao wachafu tu, tena wananuka sana. nasema hivi kwa vile niliwahi kukaa nao mpaka kwenye familia zao: wengi hawaogi hata kwa wiki zima. Wanabaki na kazi ya kujimwagia rashi tu.
 
Kwa maoni yangu Wazungu ni wachafu sana kuliko weusi kwenye kila kitu kuanzia mavazi, miili yao na hata majumbani mwao ambapo si ajabu kukuta wale wenye kupenda mbwa kulala nao vitandani.
 
Ulichosema mkuu ni sawa. Hata sisi hatupingi kuambiwa kuwa msafi mwili, kinywa, mavazi. Haya yote ni sawa. Tunachopinga na kukataa ni ku-categorize watu wa rangi fulani kwamba ndo wenye kikwapa. Hii si kweli. Kunuka kikwapa ni uchafu wa mtu binafsi, hauna cha rangi wala kabila. Mtu yeyote asipojitunza atanuka. Hivyo dhana ya kwamba waafrika tunanuka (kwa sababu tu waafrika) ni dhana potofu, ya kibaguzi, na madharau. Ndo mana mi nikasema mbona hata wao wachafu tu, tena wananuka sana. nasema hivi kwa vile niliwahi kukaa nao mpaka kwenye familia zao: wengi hawaogi hata kwa wiki zima. Wanabaki na kazi ya kujimwagia rashi tu.

Babuyao,
huenda mimi nimesoma vibaya, lakini nikim quote m_kishuri... nakutana na tafsiri hii tofauti na hiyo generalization unayoisema isipokuwa ya huyo mkongoman aliye generalize kuambiwa 'ukweli' ni "tabia za kizungu!";

Malalamiko makubwa kutoka kwa ma-supervisors wao ni kwamba baadhi ya hawa jamaa wanatoa harufu kali sana (Kikwapa), haswa wakati wa kupiga boksi. Wakatuomba tuwashauri hawa jamaa wawe WANAOGA kila siku. Nimejaribu kuwafahamisha hawa jamaa kwamba hawa wageni wanaoga kila siku, isipokuwa hawajazoea kutumia Deodorant. Supervisors hawaamini kwamba mtu anayeoga kila siku atakuwa ananuka kikwapa kiasi hicho.

Kivumbi kilichonipata ni kwamba, nilipowashauri hawa jamaa kuhusu tatizo hili na kuhusu matumizi ya Deodorants, baadhi yao hawakufurahishwa na ushauri wangu. Moja wao (kutoka Congo- Kinshasa) kanishutumu kwamba nimeishabadilika kimaadili kwa kuiga tabia za wazungu!!!

Hao supervisors walisema baadhi tu ndio waliokuwa wanatoa harufu kali. Kwanini kila tukiambiwa udhaifu tuliokuwa nao haraka haraka tunakimbilia kusema ni ubaguzi, au tunanyanyasika? Binafsi nishakutana na wazungu wengi tu wenye kunuka vibaya mno, tena kipindi hiki cha summer kwenye hizi Public transports ndio usiseme.

Tukubali kubadilika.
 
Nakwambia kama jamaa wamenyoa hayo makwapa na kuyasugua hayo makwapa mara mbili asubuhi na jioni wakati wa kuoga hayo yasingetokea. Nimesoma primary mpaka university sikuwahi kutumia hiyo kitu hata (zaidi ya rays vimafuta fulani kutoka jua kali Kenya).

Hakika Jasho + Nywele kwapani=Kikwapa=kero kwa wengine
 
Kwa maoni yangu Wazungu ni wachafu sana kuliko weusi kwenye kila kitu kuanzia mavazi, miili yao na hata majumbani mwao ambapo si ajabu kukuta wale wenye kupenda mbwa kulala nao vitandani.

.Kabisa kabisa, wengine hutumia mouthwash tu, akishapiga pafu mbili tatu za sigara na kahawa huyoooo hana hata haja ya kupiga msawaki.
Lakini, haiondoi ukweli kwamba kuna watu vikwapa vyao hunuka kupitiliza.

Heri ya anayekoga lakini anajipulizia deodorants au kupaka roll-ons kuliko yule anayekoga lakini hajisugui kikwapa (hata kwa limao), ukimfunua kwapa limejaa minywele na rangi imegeuka ya kahawia...
 
Hata wachina wana dhana hiyohiyo kwamba tunanuka. Na sababu ni kwamba hatuogi. Kunuka kwapa tunanuka kweli ila sidhani ni kwa sababu hatuogi may be madaktari hapa ukumbini watuambie ni kwa nini tunanuka.Na weupe wapo wanaonuka. Mchina joto lipo more 37oC anakuuliza je kuna joto leo ukimwambia ndiyo anadhani una-pretend tu. wanachukulia sisi weusi tulishaunguzwa na jua hatusikii kitu tena.
 
Hata wachina wana dhana hiyohiyo kwamba tunanuka. Na sababu ni kwamba hatuogi. Kunuka kwapa tunanuka kweli ila sidhani ni kwa sababu hatuogi may be madaktari hapa ukumbini watuambie ni kwa nini tunanuka.Na weupe wapo wanaonuka. Mchina joto lipo more 37oC anakuuliza je kuna joto leo ukimwambia ndiyo anadhani una-pretend tu. wanachukulia sisi weusi tulishaunguzwa na jua hatusikii kitu tena.

Safi sana. Hatua ya kwanza kwenye utatuzi wa jambo ni kukubali tatizo.
Na abishe hapa mtu ambaye hajawahi msikia mwananchi mwenzie asiyenuka kikwapa.

Mfano; Pale Dar es salaam Airport, sehemu ya kuchukulia mizigo kuna kaharufu kakali sana, sijui ni kwasababu hakuna mzunguko wa hewa ya kutosha au wale porters na baggage handlers ni wengi mle, sijui!
 
Harufu anayoitoa binadamu inategemea na misosi unayopiga, usafi kwa ujumla wa mwili na nature ya mwili. Sio suala la rangi kwa asilimia 100.
 
Mambo ya kunuka ni kwa races zote, si wao na wengine pia!!! ni mambo ya usafi na afya, samtaims harufu nyingine zinaashiria magonjwa

Ila kusema waafrika wananuka si sahihi.... sis tunafanya kazi na dada wa kizungu, aisee anatema ni balaa, kuanzia nywele [zina harufu yake], kwapa [lina harufu yake] na mdomo ndo usiseme
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom