Njia ya mwongo siku zote ni fupi. Pia wa kukosa atakosa tu. Toka kelele za Nape zianze dhidi ya Mh. Edward Lowassa inaonesha kelele hizo zinampaisha EL toka utukufu hadi utukufu. Akiwa kiongozi ndani ya umoja wa vijana ccm-UVCCM Nape alimtuhumu E.L. juu ya ufisadi wa mkataba wa ujenzi wa maghorofa pale kwenye viwanja vya UVCCM - barabara ya Morogoro DSM. Kelele zile hazikufua dafu.
Mara alipoteuliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM, Nape akadhani kuwa amepata uwanja mpana wa kushindana na E.L. Bahati mbaya, akatutumka kwa nyodo na ngebe akajiaminisha kuwa atamsambaratisha E.Lowassa. Kumbe kelele za chura hazimtishi mteka maji. E.Lowassa anazidi kuyateka maji mbele ya chura; kibaya zaidi anayanywa maji hayo mbele ya huyo chura. Vikao vinavyomsafisha E. Lowassa, mfano CC na NEC msemaji wake ni Nape, Juzi kamtangaza E. Lowassa kupita mchujo wa wagombea u-NEC tokea Monduli. masikini Naapeee!...
Na si hivyo tu, hata wale wanaosemwa kuwa wafuasi na mashabiki wa E.Lowassa ndani ya chama wanaonekana kama ni maarufu kuliko huyo Nape. Hapo ndipo ninapodhani, ukitaka kumzibia mtu itakubidi upande juu kujenga zege kuziba mafanikio yake.
Edward Lowassa kweli ni mpambanaji ambaye huwageuza wabaya wake miguu juu vichwa chini, Nape kashageuzwa kichwa chini miguu juu, humsikii tena akibwabwaja juu ya mafisadi na ufisadi. Juzi hapa, ndani ya jamiiforums kuna mada ilisema usiku wa manane Nape alionekana akiwa pamoja na jopo lililotoa mlungula kwa mmoja wa waliokuwa madiwani wa CDM katika hoteli ya La Cairo jijini Mwanza. Kama ndivyo ilivyo, ni heri E. Lowassa asiyesema lolote juu ufisadi kuliko mnafiki nape; anakemea rushwa huku akitoa rushwa na hongo. HONGERA Edward Lowassa kwa kushinda vita dhidi ya unafiki wa Nape.
Katibu Mwenezi ni mkristo, akumbuke imeandikwa: utatoaje kibanzi kwenye jicho la mwenzio wakati wewe jichoni kwako kuna boriti?
ADIOS!
Mara alipoteuliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM, Nape akadhani kuwa amepata uwanja mpana wa kushindana na E.L. Bahati mbaya, akatutumka kwa nyodo na ngebe akajiaminisha kuwa atamsambaratisha E.Lowassa. Kumbe kelele za chura hazimtishi mteka maji. E.Lowassa anazidi kuyateka maji mbele ya chura; kibaya zaidi anayanywa maji hayo mbele ya huyo chura. Vikao vinavyomsafisha E. Lowassa, mfano CC na NEC msemaji wake ni Nape, Juzi kamtangaza E. Lowassa kupita mchujo wa wagombea u-NEC tokea Monduli. masikini Naapeee!...
Na si hivyo tu, hata wale wanaosemwa kuwa wafuasi na mashabiki wa E.Lowassa ndani ya chama wanaonekana kama ni maarufu kuliko huyo Nape. Hapo ndipo ninapodhani, ukitaka kumzibia mtu itakubidi upande juu kujenga zege kuziba mafanikio yake.
Edward Lowassa kweli ni mpambanaji ambaye huwageuza wabaya wake miguu juu vichwa chini, Nape kashageuzwa kichwa chini miguu juu, humsikii tena akibwabwaja juu ya mafisadi na ufisadi. Juzi hapa, ndani ya jamiiforums kuna mada ilisema usiku wa manane Nape alionekana akiwa pamoja na jopo lililotoa mlungula kwa mmoja wa waliokuwa madiwani wa CDM katika hoteli ya La Cairo jijini Mwanza. Kama ndivyo ilivyo, ni heri E. Lowassa asiyesema lolote juu ufisadi kuliko mnafiki nape; anakemea rushwa huku akitoa rushwa na hongo. HONGERA Edward Lowassa kwa kushinda vita dhidi ya unafiki wa Nape.
Katibu Mwenezi ni mkristo, akumbuke imeandikwa: utatoaje kibanzi kwenye jicho la mwenzio wakati wewe jichoni kwako kuna boriti?
ADIOS!