Kunakila dalili ya nchi yetu kulipuka katika machafuko!

majata

JF-Expert Member
Oct 7, 2010
431
179
ukiangalia kwa kina mwenendo wa nchi yetu kwasasa unaweza kukubaliana na mimi kwamba hali ya taifa letu imefika pabaya, nasema hivyo kutokana na mambo yanayoendele nchinichini.
Mfano: mgomo wa madaktari, migomo ya walimu, migomo ya wafanyakazi, kuporomoka kwa shilingi yetu, na hali ngumu ya maisha kwa asilimia kubwa ya watanzania.

Ukiangalia kwa kirahisi mambo haya yanaonekana ni madogo kwani mara kadhaa yametokea lakini yamekuwa yakizima yenyewe bila sababu za msingi na serikali inajisahau kutafuta suruhu ya kudumu pindi yanapokuwa yameisha, hii inafanana na kupuuzia volcano hai eti kwasababu inaunguruma tu na haijawahi kulipuka.

Itafika wakati migomo hii itapata mafuta baada ya kuungwa mkono na wananchi kwani wananchi wengi wamechoshwa na yanayoendelea katika nchi yao, watawala hasa rais na wabunge wamewasaliti raia waliowapa kura(hasa wabunge wa ccm) hata inapobidi kujadili mambo yenye maslahi ya taifa wao wanaangalia wasikiudhi chama.

Kuliepusha swala hili viongozi hasa wabunge wajadili mambo yenye maslahi
Kwa taifa kama wabunge huru na sio kama watumwa wa vyama vya siasa.

"Viongozi nafasi iliyopo kutuepusha na machafuko ni sasa, msidharau matatizo ya wenzenu wakati yakwenu mnatatua maramoja"
 
Jambo hilo ni sawa na mtu anayeota huku anatembea barabarani, never narudia tena haiwezekani hilo jambo kwa Tanzania hii, labda kama ujitolee wewe kumfunga paka kengele.
 
Hata kwa Muamar Gaddaffi walisema haiwezekani!! Je uliwahi kudhania hata siku moja Hosni Mubarak angefikishwa kizimbani?
 
Hapa kwetu TZ bado saaana!!
Mazingira yetu ni tofauti sana na Benghazi
Hapa kwetu watu wanasema maoni yao bila woga, kuna chaguzi, vyombo huru vya habari,
Pia malezi yetu ni tofauti na huko penye machafuko, mpaka leo tyunaitana ndugu..
hali kama hii iliwahi kutokea mara baada ya vita vya Kagera, lakini hakuna machafuko
yaliyotokea japo maisha yalikuwa magumu...TUVUMILIE KAMA TULIVYOZOWEA...HEWALA SI UTUMWA
 
wanajua na wanajali mabadiliko ni hawa wachache wa JF na sie wengi ni waoga. Wakati Misri yanatokea hayo tayari wameelimika sana. Wako ndugu zetu huko kijijini ukiwaambia tu hili litaleta vita wanaogopa. Sie tunajali tumekula tumelala. Ila ipo siku ambayo siyo mwaka huu au hivi karibuni hayo yanaweza kutokea. Ngoja tutoe vijana vyuoni, shule za kata wasiokuwa na ajira ndo watakataa tena kuwa manamba kwenye nchi yao.
 
Nimeshangaa pamoja na serikali kuchelewesha ajira za walimu kwa madai eti walisubiri kutuma pesa kwenye halmashauri waajiriwa wasipate tabu leo kuna ndugu yangu mmoja grade a kapelekwa Kwimba cha ajabu ananambia badala ya kupewa hela ya siku7 wao wamepewa ya siku 4 tena wamekopeshwa na halmashauri eti kisa serikali haijatuma pesa

Nimeshindwa kujiuliza na nikaifikiria serikali hii kama mwendo ndo huu kila kona basi tusubiri tuone hii serikali ya kishikaji itazua nini,si huku si kule kila mahala panafuka moshi kwa sahvi
 
Kikwete aliishaona dalili mapema nasikia aliisha andaa makao kule texas kwa ajili ya familia yake na baadhi ya wana familia waliisha ripoti na wanaishi. Nasikia ilipo nyumba yake hapo awali lilikuwa eneo la w. Bush the former us president
 
Back
Top Bottom