IsangulaKG
JF-Expert Member
- Oct 14, 2010
- 706
- 386
Madaktari kila siku wanashuhudia vifo.
vya aina mbili:
Moja:Kuna watu wanaokuja hospitalini wakikaribia kufa,lakini si lazima wafe kwa sababunkuwepo kwa basic medicines na utaalamu wa daktari watunhao hupona, lakini kama hakuna basic medicine kama kwa mgonjwa wa pressure au anayepoteza damu, mgonjwa huyo hufa.
Mbili: Kuna wanaokuja wazima kabisa, wala hawako katika hali ya kufa, lakini kutokana na kukosekana kwa vifaa na dawa za kutoa matibabu sahihi watu hawa hufa
Madaktari wanashuhudia vifo hivi, ni kama injinia anayeona daraja au jengo linataka kuanguka na ana uwezo wa kuzuia lisianguke, lakini hana vifaa.
Madaktari wamekuwa ni mashahidi, wa kushuhudia vifo vya ndugu zetu, uwezo wa kuvizuia wanao, Ila hawana nyenzo.
Nani atawasemea hawa marehemu?
Madaktari wamejitahidi sana kuzuia vifo kwa kufoji nyenzo sizizostahili,ili kuzuia vifo.
Walimwokoa mjomba wangu, wakamtengezea waya wa drip kama mrija wa chakula kupitia puani..je kwa nini mirija haikuwepo? Wajinga hawajui...
....Mpwa wangu akafariki ati kale kakishikio ka sindano , wanakaita 'Kipepeo' kamekosekana, hata ndugu waliporejea kutoka dukani kukanunua, dogo alishakata roho..wajinga hawajui!
Ni wananchi wangapi wameshuhudia mtu anafariki?
Nani amewahi kumwona mtu anayekufa anavyohangaika? taswira hizi ndizo wanazobaki nazo madaktari kila wanaporudi majumbani mwao.
Taswira za watu wakikata roho tena wanajua kuwa wangeweza kuzuia vifo hivyo!
Nani atawasemea hao marehemu wanaokufa kila siku?
Ninyi ndugu si mwawaachia madaktari ndo wawe mashahidi wa vifo?
Hata ukienda hospitali una bima ya afya lakini unaambiwa hakuna dawa..
Unaenda kununua wadhani ni wajibu wako kufanya hivyo?
Hujiulizi kodi yako kuanzia kwenye mshahara mpaka bidhaa zote inaenda wapi?
Yes, watu wasioelewa madaktari wanadai nini ni 'wajinga' Mojawapo ya sifa ya mjinga ni uwezo mdogo wa kuelewa mambo hata aeleweshwe namna gani.
Madaktari wameeleza kuwa, japo mshahara ni mojawapo ya hoja, hoja kuu ni mazingira ya kufanyia kazi na vitendea kazi!
Hawa wajinga wamerubuniwa na serikali inayoongelea mishahara tu huku hoja kuu ya mazingira ya kazi na vitendea kazi haiguswi wajinga hawa , wameingia ktk mtego wa propaganda za serikali,
Wanaharakati wameihoji Serikali, 'Madaktari wametaja 3.5 milioni, je ninyi mtalipa shilingi ngapi? Serikali haijajibu kwanusahihi, wajinga wanashabikia tu!
Hawa wajinga, hawajui kuwa misamaha ya kodi ya hovyohovyo, matumizi ya anasa na mabovu ya serikali, ubadhilifu wa fedha za umma kama ungethibitiwa hiyo milioni 3.5 angekuwa analipwa dereva....
Wajinga hawajui...
vya aina mbili:
Moja:Kuna watu wanaokuja hospitalini wakikaribia kufa,lakini si lazima wafe kwa sababunkuwepo kwa basic medicines na utaalamu wa daktari watunhao hupona, lakini kama hakuna basic medicine kama kwa mgonjwa wa pressure au anayepoteza damu, mgonjwa huyo hufa.
Mbili: Kuna wanaokuja wazima kabisa, wala hawako katika hali ya kufa, lakini kutokana na kukosekana kwa vifaa na dawa za kutoa matibabu sahihi watu hawa hufa
Madaktari wanashuhudia vifo hivi, ni kama injinia anayeona daraja au jengo linataka kuanguka na ana uwezo wa kuzuia lisianguke, lakini hana vifaa.
Madaktari wamekuwa ni mashahidi, wa kushuhudia vifo vya ndugu zetu, uwezo wa kuvizuia wanao, Ila hawana nyenzo.
Nani atawasemea hawa marehemu?
Madaktari wamejitahidi sana kuzuia vifo kwa kufoji nyenzo sizizostahili,ili kuzuia vifo.
Walimwokoa mjomba wangu, wakamtengezea waya wa drip kama mrija wa chakula kupitia puani..je kwa nini mirija haikuwepo? Wajinga hawajui...
....Mpwa wangu akafariki ati kale kakishikio ka sindano , wanakaita 'Kipepeo' kamekosekana, hata ndugu waliporejea kutoka dukani kukanunua, dogo alishakata roho..wajinga hawajui!
Ni wananchi wangapi wameshuhudia mtu anafariki?
Nani amewahi kumwona mtu anayekufa anavyohangaika? taswira hizi ndizo wanazobaki nazo madaktari kila wanaporudi majumbani mwao.
Taswira za watu wakikata roho tena wanajua kuwa wangeweza kuzuia vifo hivyo!
Nani atawasemea hao marehemu wanaokufa kila siku?
Ninyi ndugu si mwawaachia madaktari ndo wawe mashahidi wa vifo?
Hata ukienda hospitali una bima ya afya lakini unaambiwa hakuna dawa..
Unaenda kununua wadhani ni wajibu wako kufanya hivyo?
Hujiulizi kodi yako kuanzia kwenye mshahara mpaka bidhaa zote inaenda wapi?
Yes, watu wasioelewa madaktari wanadai nini ni 'wajinga' Mojawapo ya sifa ya mjinga ni uwezo mdogo wa kuelewa mambo hata aeleweshwe namna gani.
Madaktari wameeleza kuwa, japo mshahara ni mojawapo ya hoja, hoja kuu ni mazingira ya kufanyia kazi na vitendea kazi!
Hawa wajinga wamerubuniwa na serikali inayoongelea mishahara tu huku hoja kuu ya mazingira ya kazi na vitendea kazi haiguswi wajinga hawa , wameingia ktk mtego wa propaganda za serikali,
Wanaharakati wameihoji Serikali, 'Madaktari wametaja 3.5 milioni, je ninyi mtalipa shilingi ngapi? Serikali haijajibu kwanusahihi, wajinga wanashabikia tu!
Hawa wajinga, hawajui kuwa misamaha ya kodi ya hovyohovyo, matumizi ya anasa na mabovu ya serikali, ubadhilifu wa fedha za umma kama ungethibitiwa hiyo milioni 3.5 angekuwa analipwa dereva....
Wajinga hawajui...